pepsin
JF-Expert Member
- Apr 23, 2015
- 3,486
- 6,172
Kati ya watu waliopambana kukemea uzembe wa CCM ni katibu mkuu wa CCM, bwana Kinana. Ukiacha kashfa ya meli yake kukutwa na nyara za serikali isivyo halali, yaani meno ya tembo, bado bwana huyu alihangaika sana kuiokoa CCM.
Alijaribu kila namna kujishusha na kushiriki na sisi watu wa hali ya nchi ili chama chake kiaminiwe tena lakini wenzake hawakumuunga mkono itoshavyo. Wakati yeye anahangaika huku chini,viongozi wenzake wanakwea ndege na kutembea aghaibuni bila kujali.
Ilifikia mahali akakemea utendaji mbovu wa viongozi wa serikali kutoka chama chake lakini aliishia kupuuzwa na kukejeliwa.
Sasa na yeye amekaa kimya, amekata tamaa na kufanya chama chake kikaribie kaburi la kisiasa kiurahisi zaidi.
Wana CCM wa kweli, mtamkumbuka sana mzee wenu huyu baada ya Oktoba. Alitaka sana kukisaidia chama lakini hamkumjali.Wakati yeye anashiriki na wananchi kwenye shughuli mbalimbali, hamna kiongozi yeyote kuanzia Taifa, mikoa, wilaya, tarafa, kata mpaka kijiji aliyemwelewa na kumuunga mkono.
Sasa jua la CCM linachoea, mtamkumbuka mzee Kinana sana.
Alijaribu kila namna kujishusha na kushiriki na sisi watu wa hali ya nchi ili chama chake kiaminiwe tena lakini wenzake hawakumuunga mkono itoshavyo. Wakati yeye anahangaika huku chini,viongozi wenzake wanakwea ndege na kutembea aghaibuni bila kujali.
Ilifikia mahali akakemea utendaji mbovu wa viongozi wa serikali kutoka chama chake lakini aliishia kupuuzwa na kukejeliwa.
Sasa na yeye amekaa kimya, amekata tamaa na kufanya chama chake kikaribie kaburi la kisiasa kiurahisi zaidi.
Wana CCM wa kweli, mtamkumbuka sana mzee wenu huyu baada ya Oktoba. Alitaka sana kukisaidia chama lakini hamkumjali.Wakati yeye anashiriki na wananchi kwenye shughuli mbalimbali, hamna kiongozi yeyote kuanzia Taifa, mikoa, wilaya, tarafa, kata mpaka kijiji aliyemwelewa na kumuunga mkono.
Sasa jua la CCM linachoea, mtamkumbuka mzee Kinana sana.