PreGE2025 Jokate Mwegelo aongoza matembezi ya "First Time Voters"

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
843
Reaction score
1,024
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Jokate Mwegelo ameongoza matembezi ya Maelfu ya Vijana ambao pia ni Wapiga Kura wapya katika uchaguzi mkuu mwaka huu 2025 (Samia First Time Voters), ambapo matembezi hayo yameishia Katika ukumbi wa JNICC Jijini Dar es salaam panapofanyika kongamano uzinduzi wa Samia First Time Voters.

Jokate ameongoza matembezi ya Vijana hao leo Aprili 19,2025 Jijini Dar es Salaam ambapo kwa pamoja wamefika kwa wingi katika uzinduzi huo wa programu Maalum ya Vijana hao kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu ambapo Jumuiya hiyo imesema imeweka mikakati mbalimbali itakayofanikisha ushindi wa Rais wa Tanzania Dk.Samia kupitia kundi la Vijana wa Tanzania.

Kongamano hilo limehudhuriwa na Vijana mbalimbali wakiongozwa na Umoja wa Vijana CCM Seneti Ya Vyuo na Vyuo vikuu Mkoa wa Dar es salaam, na Wananchi mbalimbali wa Mkoa wa Dar es salaam ambapo KM Jokate ndiye Mgeni rasmi.

Samia First Time Voters hii ni kampeni mahususi yenye lengo la kuhamasisha na Kuelimisha kundi la Vijana waliotimiza umri wa miaka 18 hivi karibuni na kupata sifa ya kuwa Wapiga kura Kwa mara ya kwanza katika uchaguzi Mkuu wa mwaka huu 2025, kujitokeza kwa wingi kupiga kura


 

Attachments

  • IMG-20250419-WA0437.jpg
    138.3 KB · Views: 32
  • IMG-20250419-WA0441.jpg
    158.1 KB · Views: 30
 
Hivi ccm huwa hofu yao kubwa ni ipi? Maana hata ukifanyika uchaguzi wa huru na haki bado wana asilimia zaidi ya 70 kushinda kwa kishindo. Kuna vijiji huko ndani ndani hawaijui act wala chadema.
 
Hivi ccm huwa hofu yao kubwa ni ipi? Maana hata ukifanyika uchaguzi wa huru na haki bado wana asilimia zaidi ya 70 kushinda kwa kishindo. Kuna vijiji huko ndani ndani hawaijui act wala chadema.
Fita Ni fita muraa!
 
Hivi ccm huwa hofu yao kubwa ni ipi? Maana hata ukifanyika uchaguzi wa huru na haki bado wana asilimia zaidi ya 70 kushinda kwa kishindo. Kuna vijiji huko ndani ndani hawaijui act wala chadema.
Fita Ni fita muraa
Sasa kama mnao wapiga kura wengi kwanini mama Samia asiweke box lenye haki ili ashinde kwa kishindo na wote tumpongeze mama yetu
Ukiwa huna watu wa kukupigia kura unakimbia uchaguzi. Very simple.
 
Je huku siko walikojaa chawa wanaoitafuna na kudidimiza afya na uhai wa taifa hili?
 
MAfisadi ya kodi za umma
 
Zile trillion zisizojulikana matumizi yake ndio haya sasa
 
Tunaendeleza Sana ujinga
 
Inasaidia mzunguko wa hela, lakini si mvuto wa kisiasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…