John Mnyika kupitishwa kwa hila Ubungo

John Mnyika kupitishwa kwa hila Ubungo

Hoyce,
mimi na wewe tunaijua hiyo katiba kanuni na vifungu vyake.tunachohoji hapa ni kwa nini double standard?
kurugenzi ya habari waweke taarifa hapa ni wangapi walichukua fomu kuomba uenyekiti mkoa. wangapi wamerudisha fomu na ambao hawakurudisha ni kwa nini?
 
Plato unaweweseka kama mwalimu aliyeenda benko mwisho wa mwezi akakuta Mshahara haujatoka
 
Unamdhalilishsa Plato. Ni mwansfilosofia mkubwa ulimwenguni. Kama haumuwezi acha kutumia jina lake mkuu.
 
Msukule Wa ufipa utahangaika Sana hicho kibabu chenu kisichopenda ukubwa

Mwaka huu magamba mtajinyonga,ngoja uchaguzi ukamilike tuanzishe mpera mpera hadi magogoni! Wasaliti wote kushinei
 
Wakuu,
Sasa ni dhahiri CHADEMA kimeanza kuwa kama CCM.

John mnyika amekuwa akisema kinafiki kuwa hagombei uenyekiti wa chama Ubungo. Ajabu ni kuwa juzi na jana viongozi wa chama na wabunge maarufu kama Mdee na Lema, wametumika kutishia watu wajitoe ili mnyinka apite bila kupingwa. Wamembambikiza agombee na Renatus Pamba Diwani wa Sinza.
Hapo ni mbali na mizengwe aliyofanyiwa katibu mwenezi aliyeshinda, ila akaambiwa hakupata zaidi ya nusu ya kura. Lakini kuna wengine wameshinda bila asilimia 50 na wameachwa.

Hapa ACT TANZANIA ikijipatia wanachama, tusilielie, tunayataka wenyewe.

Uchaguzi unaendelea.


Ukiuchambua huu uzi kwa makini utagundua Plato, ni muasi ndani ya Chadema au ni ccm/Act.

Kwa mtu yeyote anaekitakia chama chake mambo mema hawezi kuandika umbea humu ndani,atatafuta watu wazima na kuweka mambo sawa.

Plato, kwa nini umeshindwa kulitendea haki jina la mwanafalisafa huyo walau kwa kuandika kifalisafa! Pole sana nakufananisha na masalia ndani ya Chadema vile. Umenyimwa cheo mipango yako imekufa.

Kama ni mwanachadema hufai kuwa Chadema katafute chama kinachokufaa kuliko kuitesa nafsi yako. Unazidiwa na sisi ambao tuko nje ya vyama lakini ni wapenzi wa mabadiliko tu.
 
Hoyce,
mimi na wewe tunaijua hiyo katiba kanuni na vifungu vyake.tunachohoji hapa ni kwa nini double standard?
kurugenzi ya habari waweke taarifa hapa ni wangapi walichukua fomu kuomba uenyekiti mkoa. wangapi wamerudisha fomu na ambao hawakurudisha ni kwa nini?

kamuulize MM1. Ya chadema yanakuhusu nini wewe gamba? Mbafu wewe
 
Wewe Plato gani usiyejua hiki kifungu cha 6.3.1.(c) cha Katiba ya Chadema?

6.3 Uchaguzi wa Viongozi na Muda wa Uongozi
6.3.1 Utaratibu wa Uchaguzi
(a) Uchaguzi wa viongozi utazingatia taratibu na sifa za uongozi kama
zilivyofafanuliwa katika kanuni za Chama.
(b) Maombi ya uongozi yatafanywa kwa maandishi kwa kujaza fomu maalum
zilizoidhinishwa na Baraza Kuu la Chama.
(c) Majina ya wagombea wote wenye sifa zilizotakiwa yatapigiwa kura za siri na kikao
kinachohusika na mshindi atapatikana kwa uwingi wa kura usiopungua 50% ya
wapiga kura halali waliohudhuria kikao cha uchaguzi.

Labda hapo utakapotutajia wale (wengine) waliopitishwa kwa kura chini ya asilimia 50.
Naomba chadema ipite salama katika kipindi hiki kigumu. Hili ni zoezi lake mara ya kwanza, kuna mengi ya kujifunza.
 
Acha kilia lia wewe kwani hujui kazi za Mnyika, nani asiye mjua Mnyika kama ni zaidi ya kiongozi na amefanya mambo makubwa sana ambayo yanazidi hata umri wake. Mnyika ni internationally recognized ambaye kila taasisi ingependa kufanya nae kazi. Nani anaweza kusimama na Mnyika akategemea ushindi kwenye nafasi za kuchaguliwa ndani ya chama
 
Wakuu,
Sasa ni dhahiri CHADEMA kimeanza kuwa kama CCM.

John mnyika amekuwa akisema kinafiki kuwa hagombei uenyekiti wa chama Ubungo. Ajabu ni kuwa juzi na jana viongozi wa chama na wabunge maarufu kama Mdee na Lema, wametumika kutishia watu wajitoe ili mnyinka apite bila kupingwa. Wamembambikiza agombee na Renatus Pamba Diwani wa Sinza.
Hapo ni mbali na mizengwe aliyofanyiwa katibu mwenezi aliyeshinda, ila akaambiwa hakupata zaidi ya nusu ya kura. Lakini kuna wengine wameshinda bila asilimia 50 na wameachwa.

Hapa ACT TANZANIA ikijipatia wanachama, tusilielie, tunayataka wenyewe.

Uchaguzi unaendelea.

Tangulia ACT huna maana yeyote wewe...
 
Mnyika hakugombea na wala hakushiriki kwa namna yoyote ile kwenye uchaguzi wa jimbo la Ubungo. Mwenyekiti wa jimbo la Ubungo ni Diwani wa Kata ya Ubungo kamanda Boniface Jacob ambaye alichaguliwa Kidemoksia baada ya kufikia 50% ya kura. Nafasi ya Katibu mwenezi itarudiwa kwa sababu mshindi hakupata 50% kwa kuzingatia matakwa ya katiba ya chama kama ilivyokuwa kwenye nafasi ya mwenyekiti kabla ya kurudiwa juzi... Nakushauri uachane na siasa za aina hii kwa sababu zinakudhalilisha wewe na chama chama chako!
 
Wakuu,
Sasa ni dhahiri CHADEMA kimeanza kuwa kama CCM.

John mnyika amekuwa akisema kinafiki kuwa hagombei uenyekiti wa chama Ubungo. Ajabu ni kuwa juzi na jana viongozi wa chama na wabunge maarufu kama Mdee na Lema, wametumika kutishia watu wajitoe ili mnyinka apite bila kupingwa. Wamembambikiza agombee na Renatus Pamba Diwani wa Sinza.
Hapo ni mbali na mizengwe aliyofanyiwa katibu mwenezi aliyeshinda, ila akaambiwa hakupata zaidi ya nusu ya kura. Lakini kuna wengine wameshinda bila asilimia 50 na wameachwa.

Hapa ACT TANZANIA ikijipatia wanachama, tusilielie, tunayataka wenyewe.

Uchaguzi unaendelea.

Anza wewe kwenda ACT...alafu mbona vyama vya siasa vipo vingi tu!wewe umeona ACT tu ndio pakutimukia?????????????? utakuwa nzi wa ACT ALIYEVAA MAGWANDA YA CHADEMA
 
Back
Top Bottom