John Mnyika awasilisha ushahidi wizi BoT !!!

John Mnyika awasilisha ushahidi wizi BoT !!!

Makinda ataukalia huo ushahidi kama kawa.
 
Yule mzinzi wa IRAMBA atulie tu tumnyoe taratibu mshamba mkubwa yule.
 
Join Date : 11th July 2012
Posts : 4
Rep Power : 0
Likes Received 0
Likes Given 0
KARIBU MKUU CHOICE JAMVIN
 
Spika hawezi kukubali maana ataona MwanaCCM mwenzake anaangamizwa. Haya tusubiri tuone matokeo.
 
Mbona yaleyale tu muweka thread anataka kuupaisha the choice yake.

John John Mnyika awasilisha ushahidi wizi BoT !!!



mnyika.jpg
Hatimaye Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, amewasilisha ushahidi wa awali kwa Katibu wa Bunge, kuhusu tuhuma alizozitoa bungeni dhidi ya Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba, kwamba ni mmoja wa watuhumiwa katika kashfa ya ukwapuaji wa mabilioni ya fedha uliofanywa katika Akaunti ya Malipo ya Nje (Epa) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).


Hatua hiyo imechukuliwa na Mnyika kutekeleza maelekezo aliyopewa na Mwenyekiti wa Bunge, Jenista Mhagama, ambaye alimpa siku saba kuwasilisha ushahidi kuthibitisha kauli yake hiyo.

Kauli hiyo ilitolewa na Mnyika katika kikao cha Mkutano wa Bunge unaoendelea hivi sasa mjini hapa, kilichofanyika, Julai 3, mwaka huu, katika mjadala kuhusu makadirio ya mapato ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Siku hizo ziliisha juzi.

Kwa mujibu wa Mnyika, ushahidi huo aliuwasilisha kwa Katibu wa Bunge, mjini hapa juzi.

"Kuhusu tuhuma dhidi ya Mwigulu Nchemba, ushahidi wa awali nilishawasilisha leo (juzi) ndani ya siku saba kama ilivyotakiwa," alisema Mnyika.

Katika mkutano huo uliotawaliwa na mvutano, malumbano, hisia kali na maneno ya kashfa miongoni mwa wabunge, Mnyika pamoja na mambo mengine, alisema Nchemba aliwahi kuwa mtumishi wa BoT, ambayo ilikumbwa na kashfa hiyo na kwamba, naye ni mmoja wa watuhumiwa.

Kauli hiyo ya Mnyika ilimfanya Mhagama kusimama na kumpa Mnyika siku hizo awe amewasilisha ushahidi wa kauli yake.

Kwa upande wake, Nchemba wakati akichangia mjadala wa Bunge, alisema alijiunga na BoT mwaka 2006 wakati huo ukwapuaji wa fedha BoT ulikwishafanyika.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel, alithibitisha kuwasilishwa kwa barua ya maelezo ya Mnyika.

"Ni kweli tumepokea jana barua ya maelezo lakini Spika atawaelezeni kesho (leo)," alisema.

 
someni hiyo barua ya mnyika kuitwa polis
 
Hamna lolote! Jamaa ametumia nafasi ili kuirusha ijulikane hiyo blog yake!
 
Mnyika kachemka big tyme amewasilisha introduction letter spika ndungai kaeleza jioni hii na kuongeza kuwa ni kama kikaratasi cha kufungia maandazi kilichowasilishwa na Mnyika na haelewi ni ushahidi upi aliowasilishwa na mnyika kaiagiza kamati ya kanuni uadilifu na adhabu kukaa na kuijadili karatasi hiyo!!
 
Hawa magamba ndo staili ya kudili nao.
Mahakamani watuhumiwa hawashitakiwi.
Ni kuwaprovoke bungeni, wakija juu na "leta ushahidi" unapelekwa,
bunge linageuka kidogo sehem ya mahakama.
Ni bora kuliko kuunga hoja "mia kwa mia"
 
WHAT???? Au majimarefu kafanya ndumba proof ikageuka "kikaratasi cha kufungia maandazi'??? tujuzeni jameni wengine bado tungali maofisini hatuwezi kutizama tv/bunge.
 
wanajmvi kwani ushahidi wa Lema kuhusu uongo wa Pinda umeishia wapi huko ofisini kwa spika si kutajaa maushahidi? kwa nni wabunge wanaotakiwa kutoa ushahidi wasikatae mpaka ushahidi wa awali haujatolewa?
 
Mnyika kachemka big tyme amewasilisha introduction letter spika ndungai kaeleza jioni hii na kuongeza kuwa ni kama kikaratasi cha kufungia maandazi kilichowasilishwa na Mnyika na haelewi ni ushahidi upi aliowasilishwa na mnyika kaiagiza kamati ya kanuni uadilifu na adhabu kukaa na kuijadili karatasi hiyo!!

kwani mlitaka ziwe karatasi ngapi?


"narudi fb"
 
Ni mchezo wa kama baadhi ya vyuo vya elimu ya juu wakati wa kugombea uongozi wa selikari za wanavyuo ambapo wagombea either wanaandaa mamluki wa kuuliza maswali au watachomeka hoja ya kuvuruga hoja husika daaa
 
Du humu JF kiboko si mlisema MWIGULU kamsamehe MNYIKA? sasa haya mengine yanatoka wapi si km vile sisi wachangiaji ndio tunaliongoza BUNGE Tusijeichanganya nchi km walivyoiendesha Tunisia, Libya na Nchi za kiarabu kwa kusikiliza zaidi maoni ya kwenye Mitandao kuliko uhalisia wenyewe.
Mbona USA, vitu km hivi havi-iingilii Serikali na CHINA wamepiga marufuku mitandao ya namna hii. Basi tuwe wakweli sio wachochezi
 
Naona Ngugai ameamua kudili na Mnyika kwa nguvu zote, utadhani ameagizwa na mkulu maana wote wanamachungu naye!!
 
Back
Top Bottom