John Malecela alithubutu

Yaya
Hapa umethibitisha kuwa Tanzania ni nchi ya kisanii, mazingaombwe au kiini macho.
Huko mbele ni giza. Tuwaulize wale wa Sudan.

Lakini huu ujanja ujanja katika siasa za Tanzania na muungano ni kwa manufaa ya nani?
 
Mzee Malecela kipindi akiwa waziri mkuu na makamu wa kwanza wa rais alithubutu kutuletea serikali ta Tanganyika akishirikiana na wabunge 55 miongoni mwao Njelu Kasaka na Philip Marmo. Isingekuwa kuingiliwa kati na Mwalimu Nyerere, Malecela angeweza!
Mkuu Crucifix

Hapa unasema alithubutu lakini hakuweza?

Mbona utata mwingi? Umeandika Malecela alithubutu kutuletea Serikali ya Tanganyika.
Alichothubutu ni kuleta mjadala wa kuifufua serikali ya Tanganyika na sio alithubutu kutuletea serikali ya Tanganyika.

Malecela alithubutu kutuletea mjadala na azimio la bunge la kuifufua serikali ya Tanganyika. Si zaidi ya hapo.
 
utu n

Alithubutu na kujikuta akipambana na mwl Nyerere. Isingekuwa hoja ile ya Tanganyika Malecela angekuwa rais baada ya Mwinyi. Nyerere alimpenda lakini Mwinyi alimpenda zaidi...
 
HOJA YA KUDAI TANGANYIKA NDIO HIYO IMEHUISHWA NA RAIS KIKWETE PAMOJA NA PROJECT-MEMBE

Pindi tu unapoviingiza vyombo vya utawala vya Tanzania Visiwani kuja kutunga sheria za muungano na pia kuandika 'Katiba Mpya' ya ikulu bila ya kuweka wananchi wote kushika ushukani kwa vikundi vyetu vya washikadau kama inavyoainishwa kikatiba nchini.

Hakika, SIONI NAMNA YOYOTE AMBAYO ATAWEZA KUKWEPA LAWAMA ZA KUFUNGULIA 'KOPO LENYE WADUDU WA MIAKA NENDA RUDI VUNGUNI' WATU KUDAI TANGANYIKA BILA KUSIKIA CHA MTU WALA KUGEUKA NYUMA SAFARI HII.


Ushauri wa CHADEMA usipozingatiwa kwa dhati, Tanzania kama taifa tutalia sana kwa kuchagua kusamehe busara katika hili.
 
The way nilivyo na negative attitude na CCM naona kila mwanaccm ni feki tu!
 
MUNGI NYAMAZA NA UACHE KULIA SANA JUU YA MCHAKATO NAJISI KWANI MUNGU BADO YUPO UPANDE WETU DHIDI YA MAFISADI NA KUTAFUTA KWAO KWA NGUVU KULINDANA

Afande Mungi acha kulia juu ya Mchakato uliotekwa na kunajisiwa kiasi kile, Mungi ukilia unaliza wengi. Cha msingi kazi iendelee tukiwa na utaifa mbeeelee kama tai mioyoni mwetu!!!

Remember, even in and amongst a hord of 'Devils' there would always exist
LESSER DEVILS (people only smeared with devilish ideal simply because of their being in company of the well established heathens) with whom we can very well work together toward a common national endeavours based on a set of known body of unquestioned principles.


The way nilivyo na negative attitude na CCM naona kila mwanaccm ni feki tu!
 
Hivi Muungano ndio chanzo cha matatizo yetu hili taifa na kwamba ukivunjwa ndio itakuwa solution au kuna something I am missing? - William
 
Kuthubutu mbele ya ccm ya nyerere! Haikuwa kazi rahisi.
 
hivi muungano ndio chanzo cha matatizo yetu hili taifa na kwamba ukivunjwa ndio itakuwa solution au kuna something i am missing? - william

kwa kweli wanasiasa ndani ya chama tawala ndio wajua zaidi, maana sioni kama kuna namna ya kuulezea muungano huu kinyume na matakwa yao na ukapata mashiko.
 
CHADEMA WASIPOSIKILZWA JUU YA UVUNJAJI WA KATIBA YA SASA, SHERIA YA PROJECT-MEMBE KUTUVURUGA ZAIDI KOTE NCHINI

Kuna hatari kubwa sana tena sana kwa watu tukidiriki tu KUVIVUSHA BAHARI Vyombo vya utawala Tanzania Visiwani kuja kutungia KATIBA MPYA Tanzania Bara, mara baada yaa wao kukmilisha ya kwao yapata miaka miwili iliopita, kuna uwezekano mkubwa wananchi wakaona sababu ya KUCHOMOA MSUKULE WA TANGANYIKA kabatini ili akashiri mchakato moja kwa moja naye.


CHADEMA wasiposikilizwa hoja zile za msingi juu ya mjadala huu na pengine kutiwa kapuni shauri ya maelekezo ya fikra za kiitikadi, kazi itakua ni ngumu zaidi tena zaidi!!!
 
Muungano ni one ishu ninakubaliana na Mwalimu, kwamba ulindwe kwa nguvu zote usivunjwe bila sababu zenye manufaa kwa taifa. Otherwise wasioutaka watoe hoja nzito ambazo so far sijaziona, kwenye hoja ya Tanganyika sijaelewa mantiki behind it. - William
 
Hivi Muungano ndio chanzo cha matatizo yetu hili taifa na kwamba ukivunjwa ndio itakuwa solution au kuna something I am missing? - William

Kwamba alithubutu, kwa sasa hakuna anayethubutu!

Back to your comment on the Union; it might be a way to solution, tutakuwa na uwezo wa kuthubutu kufanya maamuzi magumu ambao sasa hatunao.
 

Na wenye kuhuitaji pia walete hoja zao zenye manufaa kwa Tanganyika, so far hakuna Tanganyika inachofaidika nacho kutoka Zanzibar. Sasa muungano wa nini? TANGANYIKA BILA ZANZIBAR (TANGANYIKA) INAWEZEKANA

Mzee Malecela ndiye kiongozi wa juu pekee wa kiserikali aliyewahi kuthubutu kutuletea Tanganyika. Nahisi mwingine atatokea hivi punde
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…