Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Makamu Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara, John Wegesa Heche amesema yeye na viongozi wote hawakuachiwa kwa makubaliano maalum wala hakuna mazungumzo waliyofanya wakati alipokamatwa kama ambavyo imekuwa ikidaiwa.
Heche ameyasema hayo leo Novemba 11, 2025 baada ya kutoka kuripoti katika Kituo cha Polisi Kati (Central) Dar Es Salaam.
"Kama tulivyokamatwa ndivyo tulivyoachiwa hakuna mazungumzo na yoyote tuliyofanya na mtu yoyote" amesema Heche.
Heche aliripoti kituoni hapo akiambatana na Wakili Hekima Mwasipu pamoja pamoja na viongozi wengine wa chama hicho ambao walitakiwa kuripoti akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa chama Bara Amani Golugwa, Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani, Boniface Jacob na Mjumbe wa Kamati Kuu Godbless Lema.
Heche ameyasema hayo leo Novemba 11, 2025 baada ya kutoka kuripoti katika Kituo cha Polisi Kati (Central) Dar Es Salaam.
"Kama tulivyokamatwa ndivyo tulivyoachiwa hakuna mazungumzo na yoyote tuliyofanya na mtu yoyote" amesema Heche.
Heche aliripoti kituoni hapo akiambatana na Wakili Hekima Mwasipu pamoja pamoja na viongozi wengine wa chama hicho ambao walitakiwa kuripoti akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa chama Bara Amani Golugwa, Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani, Boniface Jacob na Mjumbe wa Kamati Kuu Godbless Lema.