Sijui nani kamponza nani,... Labda ni Kikwete aliye mponza Lowasa au vice versa.
Lakini binafsi, baada ya kuchomwa jua mda mrefu nikisubiri kumuona Museveni pamoja na wenzangu,sikutegemea kusikia niliyoyasikia,ingawa nilikua na hamu kweli kujua wana UDSM wata react vipi baada ya viongozi hawa kufika.
Ilikua hivi:-
Nikiwa mbali kidogo nilisikia kilele za kushangilia,... Na mara nikasogea karibu,lakini niliye kuta akishangiliwa huku anaingia ukumbini ni Prof.Shivji.
Baada ya mda mrefu sana aliingia JK na team yake ya viongozi (akiwemo Lowasa),...ndipo nilipo ishiwa nguvu ghafla ingawa sikuwa mlengwa wa kelele hizo.
Zilisikika kelele za "mafisadi,mafisadi",...."miaka 50 tunalala nje",....
"tunataka mabadiliko",....mara JK alisimama kwa sekunde kadhaa kusoma moja ya mabango yaliyo kuwa yame kamatwa na wanachuo (sijui liliandikwa vipi, bango lilikua upande sawa na wangu ila mbali kidogo).
Yeah,nilihisi aibu na kuhisi sina nguvu.
Niliingia kwenye viatu vya JK,ila sidhani kama ame feel nilivo feel.
Ni aibu sana raisi kupokelewa nchini kwako kwa dhihaka kiasi hiki.