Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
Ni ukweli unaouma,hapo ndo inapokuja tofauti ya kusoma na kwenda shule..wakati 'graduates' wa nchi mbalimbali ndo chachu ya mabadiliko wa hapa hata kuzungumzia siasa anaona taabu ataonekana mshamba.,, ni wachache mno wanaojishughulisha hata kuangalia/kusikiliza taarifa ya habari...laiti wangesoma na kujua role played na siasa katika maisha yetu labda wangeamka..
Jamani.. uchaguzi una matokeo yake. Binafsi sitaki kabisa kusikia mwana CCM au mtu yeyote aliyeunga mkono JK kurudi madarakani analalamikia iwe mafuta au dawa ya vipodozi. Watu lazima wajifunze kuishi na maamuzi waliyoyachukua.
Gesi (15kg) from 45,000 to 70,000
Sadolin ya mkaa iliyokuwa inauzwa 1500 sasa ni 3000
kwa sisi wajenzi nondo zile za 12,000 sasa ni 17,000! kwa kifupi vifaa vya ujenzi vimepanda sana! kama hujajenga kihalali....
Mechi inaendelea natamani hali hii iendelee ifikie watu kushindia maji tu! shida zikiongezeka haya yatatokea:
1. Akili ya kuchagua viongozi bora itakuja tu!
2. watu watakuwa sensitive na hali ya nchi na sio kukurupuka tu
3. Mijadala ya kidini haitakuwepo, maana woote wamakonde, wamalira, wanyakyusa, wachaga, wangindo, wapogo wote wana suffer the same. waislamu na wahindu, wakristo na wapagani watapata shuruba ile ile! tutaona kama akili hazitakuja kichwani,
4. wale wasomi 'graduate' wanaotembelea magari ya mikopo na kupanga Sinza, huku wakiwa weredi wa vikao vya harusi na kushinda kuchoma mafuta yaliyopanda bei HUKU WAKIWA HAWANA MPANGO NA ISSUE ZA KITAIFA wataamka!!
we need same platform ili TUELEWANE!!, shida tu zitawakomboa watanzania, kelele tumepiga watu bado wanawachagua CCM!!!
Acha maisha magumu yaongezeke JK kanyaga twende!!!!
Hakuna nchi duniani ambayo bei za bidhaa zimeshuka.
Jamani.. uchaguzi una matokeo yake. Binafsi sitaki kabisa kusikia mwana CCM au mtu yeyote aliyeunga mkono JK kurudi madarakani analalamikia iwe mafuta au dawa ya vipodozi. Watu lazima wajifunze kuishi na maamuzi waliyoyachukua.
Osama aliwauliza vijana wake:
"Kwa nini kutumia panga kukata mti wakati shoka lipo......???"
Msihangaike na kupanda kwa bei ya vitu. Hiyo siyo tija sana.
Watu kama Mapolisi, TISS, JWTZ, Waalimu, Magereza, nk wanasaidia sana CCM.
Hawa dawa yao ni HAZINA IKOSE PESA.
YES, naombea HAZINA ya TANZANIA Ishiiwe FEDHA.
Hapo tutawaona hao FFU na Wauwaji Mapolisi wa Tz wakihaha................
Mkuu Tropical,
nakuon tayari uko ndani ya ukumbi hapa sebuleni JF, jana ulifadhaishwa na posti fulani hivi na baadaye nikakutolea ufafanuzu juu ya hilo, vipi hata ukaamua kuendelea na ukimya kana kwamba maelezo hayokutosheleza??
Kama vipi basi leo hii katutolee tathmini ya bei za bidhaa na huduma, mwaka mmoja tangu uchaguzi umalizike mwaka jana huku tukisikia Mkullo na mkutano wa dharura kuhusi shilingi yetu kuelekea 1,700 kwa dola moja ya ki-Marekani - ambayo tafsiri yake unaifahamu vema.
Unafikiri JK ndio anapandisha bei ya mafuta na kushusha bei ya mafuta
Kama unafikiri hivyo there two things involved
Either you are blind or deceived...
If no, then your are pretending
Wakati ntegemea Mzee Mwanakijiji yeye atakujibu tu kwa nafasi yake baadaye, mimi labda nichukue tu fursa hii kukukumbusha ya kwamba uchumi nawirishi ni matokeo ya ubora wa uongozi wa taifa husika katika kipindi fulani.
Ila kinyume na hapo, sikweli kwamba mazingira ya BORA UONGOZI nao hauna mguso wake katika maendeleo ya uchumi wa nchi - laa hasha!! Siku zote, katika mazingira ya BORA UONGOZI matokeo yake huwa ni UCHUMI UNAONAWIRISHA kwa wateule tu.
Sasa mpaka hapo mkuu, hebu tupe maoni yako zaidi kama bado hoja yako ni kwamba shilingi yetu kutitia hadi kufikia thamani ya 1,700 kwa dola moja bado tu haina uhusiano na uongozi wa leo?
Hili nalo neno! Hao unaowaita wasomi ni tatizo kupita maelezo. Hakuna cha usomi wala nini. Nitakupa mfano, walioko vyuoni watagoma kwa kukosa mikopo lakini hawatagoma kupinga Dowans kulipwa....huo ndio usomi wao! Sina zaidi maana nataka kujichoma moto!
Ubora wa kiongozi haupimwa kwa thamani ya shillingi tu..
Kuna mambo lukuki hapa tukianza kuweka tutaharibu thread ambayo JK amefanya kiuchumi kupita rais yeyote bongo
Kwenye mada niambie ni wakati gani bei ya vitu iliwahi kushuka popote duniani?
1961-----1985 (bei ilikuwa ikipanda tu)
1985----1995 (bei za bidhaa ilikuwa ikipanda tu)
1995----2005 (bei ya bidhaa ilikuwa ikipanda tu)
2005----2015 (bei ya bidhaa itapanda tu)
2015---- above (bei ya bidhaa itapanda tu hadi system ya paper money i burst ..(huu uzi wewe huwezi kuuelewa !
Huo uchumi ulisomea chini ya mwembe wakati wa mvua