Mhabarishaji
JF-Expert Member
- Oct 5, 2010
- 1,007
- 601
Rais Kikwete hatimaye amekomesha kigugumizi cha Viongozi wengi ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakishindwa kutamka waziwazi hadharani kwamba, nchi ya Tanzania kwa sasa siyo nchi inayoongozwa na sera ya Ujamaa na Kujitegemea. Ingawa kwa miaka mingi Ujamaa umezikwa katika nchi yetu, bado Katiba ya nchi imeendelea kutamka kuwa nchi yetu ni ya Ujamaa. Alipokuwa akizungumza na wazee wa Dar hapo jana, uzalendo ulimshinda JK na akatamka waziwazi kwamba anapokwenda nje kutafuta wawekezaji huwa anawaambia,"Ujamaa haupo siku hizi Tanzania", hivyo hakuna tena masuala ya kutaifisha mali za wawekezaji.