Jk anarudia kosa la ghadafi? Mie ningemshauri!

kweleakwelea

JF-Expert Member
Nov 29, 2010
3,066
1,535
CCM ILIPOfika sasa japo kumekuwa na upokenazaji wa madaraka hauna tofauti na ufalme wa ghadafi, aliyekuwa na nguvu nyingi lakini akauawa katika kalvati....

ufanano wapo upo pale

1. ni familia zile zile zenye kuamua hatma ya wananchi wote

2. ni familia hizo hizo zimezidisha mipaka na kudhani tanzania ni shamba la bibi yao

3. ni familia zilizojisahau na kufanya ufujaji wa rasilimali za umma...kisha kuajiri dola kukandamiza mawazo mbadala

4. ni familia zinazotumia vikosi vya majeshi kufyatua risasi na kuua wananchi wake

ningekuwa kikwete:

1. ningetambua kuwa demokrasia ni mama ya yote. ningeiacha ikue.......

2. ningetambua kuwa watu wengi hata wasaidizi wake hawafurahishwi na jinsi mambo yanavyokwenda na kisha kuporomoka kwa uchumi

3. ningetambua kuwa CCM sasa haina itikadi hivyo wanachama wake hawana common interest na hivyo kuna makundi

4. ningetambua kuwa kuna makundi ndani na nje ya ccm yanapigania kukamata dola haya yanaweza kusababisha turbulence katika nchi. makundi haya yana influence kuanzia ofisini kwake, usalama, bungeni, chamani, polisi, mahakamani nk......

5. ningetambua kuwa mazingira haya hayanitofautishi sana na sana na ghadafi aliyefia mtaroni

HIVYO NINGEFANYA NINI:

1. Ningeruhusu mjadala huru wa katiba.mjadala huu ungekuwa mwiba kwa mahasimu wangu wa siasa. pia ungevunja makundi yote towards power struggle.

2. ningehakikisha kuwa KATIBA YA WATU inapatikana ndani ya siku 100. hii ingenihakikishia kuendelea kula BATA hewani na kumalizia kipindi changu vyema. hii itanifanya hata nikiwa mzee niendelee kuwa kipenzi cha watu na kuwa baba wa TANZANIA MPYA......

3. sitafia kwenye kalvati! wala kuhangaika kupelekwa the hague!

ni ushauri tu
 
Back
Top Bottom