GuDume
JF-Expert Member
- Jan 18, 2015
- 6,652
- 14,268
Katika moja ya tabia ambazo nimekuwa nikipambana nayo ni hii ya kutaka kujua ulimwenguni kumekuwa na nini kikiendelea. Asubuhi sana napoamka najikuta naangalia CNN,BBC,AL JAZEERA,VOA,SKY NEWS,CBN, na local channels kwa habari za kitaifa. Lakini Zaidi Zaidi ni kuangalia channels mbali mbali za gunduzi za kisayansi na historia.
Katika haya yote nimegundua binadamu tunafanya juhudi kubwa sana ya kugundua namna ya kujiangamiza.. kwa marifa mengi,elimu na gunduzi nyingi bado mwishowe hatufanyi maisha kuwa rahisi isipokuwa magumu Zaidi na yenye kuogofya. Tunapambana katika kupambana na sisi wenyewe kuliko kupambana na kila kinachotaka kuangamiza binadamu hapa ulimwenguni.
Ugunduzi na matumizi ya Drones.
Kiukweli binafsi huu ni moja ya ugunduzi wenye kuogofya hasa…. Ashakum si matusi kuwa ni kama binadamu kwa sasa “we https://jamii.app/JFUserGuide ourselves” sasa hizi ndege ambazo zinajiendesha zenyewe zimekuwa na uwezo wa kwenda kushambulia kijeshi kwa masafa ya mabli pasipo kuwepo na rubani ndani yake. Ukiangalia kirahisi utasema huu ni ugunduzi wenye manufaa makubwa sana hapa duniani. Lakini kaa fikiria ndege hizi zinaenda kumshambulia nani? Binadamu mwenzetu ..ila zinapunguza madhara kwa anayezituma kwa sababu sasa hazitakuwa na rubani ambaye anaweza dhurika. Lakini je kiuchumi haziathiri nchi husika kutokana na mamilion ya pesa yanayotumika?zina athari yake kubwa tu.
Afrika miaka yote tumejikuta tunaangukia katika makundi makuu mawili… kwa kufuata itikadi,mila na tamaduni husika tunajikuta tukisifia na kuponda upande flani. Lakini swali ambalo kama afrika hatujiulizi maendeleo haya yana tuweka katika mustakabali gani? Nini uelekeo wetu miaka kadhaa ijayo? Afrika tunakuja kutawaliwa. Gunduzi hizi na maendeleo haya tunaweza dhani sisi hayatuhusu na hayana athari kwetu. Lakini tunasahau kuwa hata sasa tunatawaliwa kwa njia moja ama nyingine.
Drones ni kama jini. Hizi ni ndege majini ambazo zinatumwa kwenda sehemu kufanya uharibifu. Kwa kiwango kikubwa zimekuwa precisely kwa sababu zinaelekezwa ziende wapi na kurudisha feedback kwa kutumia camera ndogo zenye uwezo mkubwa kuhusiana na sehemu husika.hii inazipa uwezo wa kupiga kuua pasipo mhusika kujua nini kimemsibu. Zimeundwa pia na uwezo mkubwa wa kuweza kujificha kuonekana katika rada. Hii ni teknolojia ambao anayekushambulia anakuwa amekaa ofisini anakunywa kahawa huku miguu kapandisha mezani
Maendeleo ya kutisha katika matumizi ya Drones
Kumeendelea kuwepo majaribio ambayo yanaaelekea kuleta mrejesho mzuri juu ya maboresho yanayofanyika.sasa drone inaweza wekewa bunduki ili iwe na uwezo wa kupiga risasi kwa ajili ya kufanya mauaji. Hivyo hii itatumwa kuja kumuua mtu husika…. Ikishafanya mauaji itarudi ilikotoka au hata kama itakamatwa bado aliyeituma hatojulikana na haiwezi kutoa ushahidi.piazimeundwa na uwezo wa kujiipua yenyewe baada ya kufanya shambulio.
Fikiria unatembea sehemu halafu zinakuja risasi kadhaa zinapigwa kutoka kwenye drone. (hakutakuwa tena na haja ya kuwa na watu wasiojulikana kwa ajili ya kazi za mauaji ) Unaanguka na kufa. Na drone yenyewe inalipuka. Basi ….unaokotwa na kuwahishwa hospital.. unafika ukiwa DOA (Dead on Arrival) na kama ulijeruhiwa basi inawezekana bado ukafia njiani kutokana na foleni kubwa zinazotuandama nchi zetu hiz za dunia ya tatu.haya ni maendeleo tunayoyashabikia. tunakoelekea ni hatari zaidi kuliko tulipo.
HARAKATI ZA KUTENGENEZA shambulio la ki EMP
Mfano wa shambulio la kinyuklia la EMP. mfumo wa umeme wote unakuwa hatari na hatimaye kufa na kuua pia.
Unafaham kuwa kuna silaha ambayo imekuwa ikitengenezwa miongo kadhaa ya nyuma ambayo iana kifaa kinachoweza kuzalisha EMP? ( Elecromagnetic pulses) hii inaweza shambulia grid za umeme nchini kwa kuzifanya zikate umeme. Kufanya giza na kutokuwa na umeme kwa nchi nzima kwa kipindi flani.hii inaweza ua mifumo yote ya bank,simu zikafa na computers pia.kila kitu kikavurugika ndani ya muda mfupi tu ukajikuta umeshika Iphone yako ambayo ni useless. mifumo yote ya umeme unauliwa kila aina ya umeme... na tayari Korea kaskazini inasemakana wanalo Bomu kama hili na walitoa Tishio kuwa wanaweza kulitumia dhidi ya USA. ambao wao walishakuwa nalo kwa siri na wakajiongeza zaidi kuanza kutengeneza counter attack yake.fikiria Umepakata Apple yako ambayo ni useless sababu imekufa,mawasiliano yoote kwa njia ya umeme yaathirika huku wenzio wakiwa na uwezo wao kama kawaida tayari kukushambulia.heri kwa wenye tecno hawataumia sana kwa shambulio kama hili.
Unafaham RDD inawezaje kuangamiza binadamu? (Dirty Bomb) bomu chafu
Radio Logical Dispersal Device (RDD) ambayo inakuw ana milipuko iliyopangiliwa kitalam kama vile baruti inaua kwa kupitia mionzi. Kwa kuachia monzi mikali ambayo inaweza sababisha maumivu,mateso na vifo kwa binadamu katika sehemu husika kuliko hata miale inayofahamika kama radioactive. Aina hii ya bomb wenyewe wanaita Dirty Bomb
Robot za Mauaji.
Hizi si Drones. Huu mradi umekuwa ukiendelea kufanyika huko Northrop ,El Sagundo,CA ukifahamika kama X-47b UCAS ( Navy Unamanned Combat Air System Demonstration) au UCAS- D . ni mradi ambao unasimamiwa kwa usiri mkubwa na serikali ya marekani. Inafanana sana na kile ambacho umewahi kukiona kwneye “skynet” hii teknolojia si drones.. ni kitu kingine kabisa. Hii ni mashine ya kuulia. (KILLING MACHINE) hakuna anayekaa sehemu kui control kama ilivyo kwa drones. Ina akili kubwa ya kufanya kile ambacho umeaiambia pasipo tena wewe kuifuatilia na joy stick kama ilivyo kwa drones.ukisha iambia basi inaenda kufanya ulichoiambia pasipo tena wewe kui control na huwezi tena kuiingilia sababu tayari inakuwa imeshafanya maamuzi ya kile ambacho umeiambia.
1. Inajiendesha kwa kujitegemea
2. Inatua na kupaa yenyewe
3. Inaweza kutua kutoka kwenye ardhi au manowari yenyewe
4. Inaweza jijaza mafuta yenyewe
5. Inaweza kuendelea na next target baada ya kumalizana na target ya kwanza
Hii ni robot ambayo imeundwa kumuua binadamu. Imeundwa kwa dhamira hiyo na ipo tayari kabisa katika maabara za wenzetu. Hii robot imesimamishwa uzalishaji Zaidi kwa sababu hata walioitengeneza wameshtuka kuwa inafanya kazi kwa ubora kuliko walivyotegemea. Hii ni predator. Project X-47Bs ilifanyiwa majaribio ambayo yaliwaogopesha waliyoitengeza. Kuwa kama ni mtu tungesema imekuwa fit kuliko alivyotegemewa. Imepitiliza.
Mauaji kupitia Virusi hatari Zaidi kwa maisha ya binadamu
watu waliofariki kwa mafua haya wakienda kuzikwa.
Mwaka 1918 kulikuwa na mafua ya Hispania.. . kama sasa tunaposikia habari za mafua ya ndege. Mwaka huo yalikuwepo mafua ya Hispania ambayo yaliua watu kati ya Mill 50- 100. Mafua haya yalisababisha vifor vya watu karibia 70,000 USA peke yake na mwaka 2009 mlipuko kama huo uliua tena watu karibia 284,000. Mwaka 2011 Ron Fouchier na Yoshihiro waliangalia toleo lingine la H5N1 ambalo ni kama Mafua ya Nguruwe na kuchapisha matokeo yake.
Kifo kibaya cha mateso makali kutokana na mafua haya mwaka 1918 huko Hispania
Hii ilifungua mlango kwa watu wenye kuw ana roho mbaya juu ya binadamu wenzao kuanza kufikiria kutengeneza mabombu ya kikemikali.. kwa miaka mingi iliaminiwa kuwa makundi ya kigaidi hayawezi kuja kupata nafasi au uwezekano wa kumiliki mambo ya hatari kama haya. Lakini ISIS inakadiriwa kuwa na mapato ya karibia USD million 85- 400 na kuwa na umiliki wa vituo kadhaa vya kitabibu. Na inafahamika kuwa Syria imewahi kutumia silaha za kikemikali na wataalamu walioko Syria wanaweza kutumika kutengeneza Virusi hatari kama hao wa Mafua ya Hispania. Hi dunia si sehemu salama tena na ndo maana wenzetu wengine wameshaamua kwenda kuishi sayari nyingine. Unapoangalia Tv series kama The 100 n.k unaweza amini ni mambo ya kufikirika .. lakini kuna kitu ambacho dunia inaambiwa ijiandae nacho. Kuna siku watu watahama hii dunia ,kuna watu wameshajiandalia makazi chini ya ardhi.. kuna watu tutakuja kufutika usoni pa dunia. Binadamu anayafanya haya kwa binadamu mwenzie. Wala si kwa fisi,chui na nyoka.
Madhara ya silaha za Kibayokemikali huko Syria. (biochemical)
Hili ndilo linalooumiza Zaidi. Kuwa haya yote yanafanywa na binadamu dhidi ya binadamu mwenzie. Sasa mimi na wewe tuendelee kukaa hapa na kuwaza style mbalimbali za kuwaridhisha wanawake na wanaume katika ngono. Tuendelee tu kushabikia vigodoro, tukutane kule forums ya mambo yetu pendwa. mambo rahisi na laini laini tu. tuwekeze katika style hizi za katerero, punda afe,mbuzi kagoma, kitambaa cheupe n.k tuendelee kufuatilia msanii gani anatembea na nani.
Tuendelee kusumbuana kwa mambo ya kipuuzi. Siku ikifika hatujui hata jinsi ya kutengeneza mask… tutakufa kama kumbikumbi. Hapo ndipo ninapojisia uvivu wa kuwaza. Naukunyata moto tu na kuugua moyoni. Unajua nini? Najivunia kuwa mwafrika ila nasikitika sana kuzaliwa afrika.
Katika haya yote nimegundua binadamu tunafanya juhudi kubwa sana ya kugundua namna ya kujiangamiza.. kwa marifa mengi,elimu na gunduzi nyingi bado mwishowe hatufanyi maisha kuwa rahisi isipokuwa magumu Zaidi na yenye kuogofya. Tunapambana katika kupambana na sisi wenyewe kuliko kupambana na kila kinachotaka kuangamiza binadamu hapa ulimwenguni.
Ugunduzi na matumizi ya Drones.
Kiukweli binafsi huu ni moja ya ugunduzi wenye kuogofya hasa…. Ashakum si matusi kuwa ni kama binadamu kwa sasa “we https://jamii.app/JFUserGuide ourselves” sasa hizi ndege ambazo zinajiendesha zenyewe zimekuwa na uwezo wa kwenda kushambulia kijeshi kwa masafa ya mabli pasipo kuwepo na rubani ndani yake. Ukiangalia kirahisi utasema huu ni ugunduzi wenye manufaa makubwa sana hapa duniani. Lakini kaa fikiria ndege hizi zinaenda kumshambulia nani? Binadamu mwenzetu ..ila zinapunguza madhara kwa anayezituma kwa sababu sasa hazitakuwa na rubani ambaye anaweza dhurika. Lakini je kiuchumi haziathiri nchi husika kutokana na mamilion ya pesa yanayotumika?zina athari yake kubwa tu.
Afrika miaka yote tumejikuta tunaangukia katika makundi makuu mawili… kwa kufuata itikadi,mila na tamaduni husika tunajikuta tukisifia na kuponda upande flani. Lakini swali ambalo kama afrika hatujiulizi maendeleo haya yana tuweka katika mustakabali gani? Nini uelekeo wetu miaka kadhaa ijayo? Afrika tunakuja kutawaliwa. Gunduzi hizi na maendeleo haya tunaweza dhani sisi hayatuhusu na hayana athari kwetu. Lakini tunasahau kuwa hata sasa tunatawaliwa kwa njia moja ama nyingine.
Drones ni kama jini. Hizi ni ndege majini ambazo zinatumwa kwenda sehemu kufanya uharibifu. Kwa kiwango kikubwa zimekuwa precisely kwa sababu zinaelekezwa ziende wapi na kurudisha feedback kwa kutumia camera ndogo zenye uwezo mkubwa kuhusiana na sehemu husika.hii inazipa uwezo wa kupiga kuua pasipo mhusika kujua nini kimemsibu. Zimeundwa pia na uwezo mkubwa wa kuweza kujificha kuonekana katika rada. Hii ni teknolojia ambao anayekushambulia anakuwa amekaa ofisini anakunywa kahawa huku miguu kapandisha mezani
Maendeleo ya kutisha katika matumizi ya Drones
Kumeendelea kuwepo majaribio ambayo yanaaelekea kuleta mrejesho mzuri juu ya maboresho yanayofanyika.sasa drone inaweza wekewa bunduki ili iwe na uwezo wa kupiga risasi kwa ajili ya kufanya mauaji. Hivyo hii itatumwa kuja kumuua mtu husika…. Ikishafanya mauaji itarudi ilikotoka au hata kama itakamatwa bado aliyeituma hatojulikana na haiwezi kutoa ushahidi.piazimeundwa na uwezo wa kujiipua yenyewe baada ya kufanya shambulio.
Fikiria unatembea sehemu halafu zinakuja risasi kadhaa zinapigwa kutoka kwenye drone. (hakutakuwa tena na haja ya kuwa na watu wasiojulikana kwa ajili ya kazi za mauaji ) Unaanguka na kufa. Na drone yenyewe inalipuka. Basi ….unaokotwa na kuwahishwa hospital.. unafika ukiwa DOA (Dead on Arrival) na kama ulijeruhiwa basi inawezekana bado ukafia njiani kutokana na foleni kubwa zinazotuandama nchi zetu hiz za dunia ya tatu.haya ni maendeleo tunayoyashabikia. tunakoelekea ni hatari zaidi kuliko tulipo.
HARAKATI ZA KUTENGENEZA shambulio la ki EMP
Mfano wa shambulio la kinyuklia la EMP. mfumo wa umeme wote unakuwa hatari na hatimaye kufa na kuua pia.
Unafaham kuwa kuna silaha ambayo imekuwa ikitengenezwa miongo kadhaa ya nyuma ambayo iana kifaa kinachoweza kuzalisha EMP? ( Elecromagnetic pulses) hii inaweza shambulia grid za umeme nchini kwa kuzifanya zikate umeme. Kufanya giza na kutokuwa na umeme kwa nchi nzima kwa kipindi flani.hii inaweza ua mifumo yote ya bank,simu zikafa na computers pia.kila kitu kikavurugika ndani ya muda mfupi tu ukajikuta umeshika Iphone yako ambayo ni useless. mifumo yote ya umeme unauliwa kila aina ya umeme... na tayari Korea kaskazini inasemakana wanalo Bomu kama hili na walitoa Tishio kuwa wanaweza kulitumia dhidi ya USA. ambao wao walishakuwa nalo kwa siri na wakajiongeza zaidi kuanza kutengeneza counter attack yake.fikiria Umepakata Apple yako ambayo ni useless sababu imekufa,mawasiliano yoote kwa njia ya umeme yaathirika huku wenzio wakiwa na uwezo wao kama kawaida tayari kukushambulia.heri kwa wenye tecno hawataumia sana kwa shambulio kama hili.
Unafaham RDD inawezaje kuangamiza binadamu? (Dirty Bomb) bomu chafu
Radio Logical Dispersal Device (RDD) ambayo inakuw ana milipuko iliyopangiliwa kitalam kama vile baruti inaua kwa kupitia mionzi. Kwa kuachia monzi mikali ambayo inaweza sababisha maumivu,mateso na vifo kwa binadamu katika sehemu husika kuliko hata miale inayofahamika kama radioactive. Aina hii ya bomb wenyewe wanaita Dirty Bomb
Robot za Mauaji.
Hizi si Drones. Huu mradi umekuwa ukiendelea kufanyika huko Northrop ,El Sagundo,CA ukifahamika kama X-47b UCAS ( Navy Unamanned Combat Air System Demonstration) au UCAS- D . ni mradi ambao unasimamiwa kwa usiri mkubwa na serikali ya marekani. Inafanana sana na kile ambacho umewahi kukiona kwneye “skynet” hii teknolojia si drones.. ni kitu kingine kabisa. Hii ni mashine ya kuulia. (KILLING MACHINE) hakuna anayekaa sehemu kui control kama ilivyo kwa drones. Ina akili kubwa ya kufanya kile ambacho umeaiambia pasipo tena wewe kuifuatilia na joy stick kama ilivyo kwa drones.ukisha iambia basi inaenda kufanya ulichoiambia pasipo tena wewe kui control na huwezi tena kuiingilia sababu tayari inakuwa imeshafanya maamuzi ya kile ambacho umeiambia.
1. Inajiendesha kwa kujitegemea
2. Inatua na kupaa yenyewe
3. Inaweza kutua kutoka kwenye ardhi au manowari yenyewe
4. Inaweza jijaza mafuta yenyewe
5. Inaweza kuendelea na next target baada ya kumalizana na target ya kwanza
Hii ni robot ambayo imeundwa kumuua binadamu. Imeundwa kwa dhamira hiyo na ipo tayari kabisa katika maabara za wenzetu. Hii robot imesimamishwa uzalishaji Zaidi kwa sababu hata walioitengeneza wameshtuka kuwa inafanya kazi kwa ubora kuliko walivyotegemea. Hii ni predator. Project X-47Bs ilifanyiwa majaribio ambayo yaliwaogopesha waliyoitengeza. Kuwa kama ni mtu tungesema imekuwa fit kuliko alivyotegemewa. Imepitiliza.
Mauaji kupitia Virusi hatari Zaidi kwa maisha ya binadamu
watu waliofariki kwa mafua haya wakienda kuzikwa.
Mwaka 1918 kulikuwa na mafua ya Hispania.. . kama sasa tunaposikia habari za mafua ya ndege. Mwaka huo yalikuwepo mafua ya Hispania ambayo yaliua watu kati ya Mill 50- 100. Mafua haya yalisababisha vifor vya watu karibia 70,000 USA peke yake na mwaka 2009 mlipuko kama huo uliua tena watu karibia 284,000. Mwaka 2011 Ron Fouchier na Yoshihiro waliangalia toleo lingine la H5N1 ambalo ni kama Mafua ya Nguruwe na kuchapisha matokeo yake.
Kifo kibaya cha mateso makali kutokana na mafua haya mwaka 1918 huko Hispania
Hii ilifungua mlango kwa watu wenye kuw ana roho mbaya juu ya binadamu wenzao kuanza kufikiria kutengeneza mabombu ya kikemikali.. kwa miaka mingi iliaminiwa kuwa makundi ya kigaidi hayawezi kuja kupata nafasi au uwezekano wa kumiliki mambo ya hatari kama haya. Lakini ISIS inakadiriwa kuwa na mapato ya karibia USD million 85- 400 na kuwa na umiliki wa vituo kadhaa vya kitabibu. Na inafahamika kuwa Syria imewahi kutumia silaha za kikemikali na wataalamu walioko Syria wanaweza kutumika kutengeneza Virusi hatari kama hao wa Mafua ya Hispania. Hi dunia si sehemu salama tena na ndo maana wenzetu wengine wameshaamua kwenda kuishi sayari nyingine. Unapoangalia Tv series kama The 100 n.k unaweza amini ni mambo ya kufikirika .. lakini kuna kitu ambacho dunia inaambiwa ijiandae nacho. Kuna siku watu watahama hii dunia ,kuna watu wameshajiandalia makazi chini ya ardhi.. kuna watu tutakuja kufutika usoni pa dunia. Binadamu anayafanya haya kwa binadamu mwenzie. Wala si kwa fisi,chui na nyoka.
Madhara ya silaha za Kibayokemikali huko Syria. (biochemical)
Hili ndilo linalooumiza Zaidi. Kuwa haya yote yanafanywa na binadamu dhidi ya binadamu mwenzie. Sasa mimi na wewe tuendelee kukaa hapa na kuwaza style mbalimbali za kuwaridhisha wanawake na wanaume katika ngono. Tuendelee tu kushabikia vigodoro, tukutane kule forums ya mambo yetu pendwa. mambo rahisi na laini laini tu. tuwekeze katika style hizi za katerero, punda afe,mbuzi kagoma, kitambaa cheupe n.k tuendelee kufuatilia msanii gani anatembea na nani.
Tuendelee kusumbuana kwa mambo ya kipuuzi. Siku ikifika hatujui hata jinsi ya kutengeneza mask… tutakufa kama kumbikumbi. Hapo ndipo ninapojisia uvivu wa kuwaza. Naukunyata moto tu na kuugua moyoni. Unajua nini? Najivunia kuwa mwafrika ila nasikitika sana kuzaliwa afrika.