Jinsi ya kupika sambaro

Mwanampuna

Senior Member
Jul 21, 2016
131
80
Mahitaji
1.Viazi mbatata kilo 1
2. Mabamia fungu 1 kubwa
3. Mabiringanya makubwa 2
4. Karoti
5. Mafuta ya kupikia
6. Nyanya
7.Vituungu maji 2
8. Swaumu
9. Ndimu
10. Chumvi

Jinsi ya kupika
1. Chukua viazi vimenye na uvioshe kisha vipasue mara nne kwa urefu kisha uvikate kwa upana kama unakata cripsy weka kwenye chombo chake

2. Kisha chukua biringanya litoe lile ganda lake la juu la kijani lakini usilimenye maganda kisha lipasue kama ulivyofanya kwenye viazi weka kwenye chombo chake

3. Chukua bamia likate vipande vidogo kisha weka kwenye chombo chake
Kisha bandika kikaangio weka Mafuta hadi yapate moto kisha weka vile viazi vikaange kama unavyokaanga chipsi na hakikisha visiwe vitepe kisha weka kwenye bakuli

4. Kisha kaanga mabiringanya hadi yawe brown kidogo (yakizidi brown yanakua machungu) kisha uweke kwa juu ya vile viazi ulivyovikaanga

5. Chukua bamia kaanga hadi ziwe brown kisha weka juu ya zile biringanya na viazi ulivyovikaanga

6. Pika mchuzi mzito kama rosti hakikisha unautia vitunguu swaumu, karoti na ndimu na viungo vyote vya mchuzi. Kisha mwagia mchuzi wako kwenye ule mchanganyiko wako wa viazi ,biringanya na bamia ulizokaanga

Unaweza kula mboga hii kwa chapati au maandazi
1484326067615.jpg
 

Attachments

  • 1484325666792.jpg
    1484325666792.jpg
    85.5 KB · Views: 272
Nlidhani sambaro huwekwa na pilipili, ukiila kwenye birian hatari
 
Mahitaji
1.Viazi mbatata kilo 1
2. Mabamia fungu 1 kubwa
3. Mabiringanya makubwa 2
4. Karoti
5. Mafuta ya kupikia
6. Nyanya
7.Vituungu maji 2
8. Swaumu
9. Ndimu
10. Chumvi

Jinsi ya kupika
1. Chukua viazi vimenye na uvioshe kisha vipasue mara nne kwa urefu kisha uvikate kwa upana kama unakata cripsy weka kwenye chombo chake

2. Kisha chukua biringanya litoe lile ganda lake la juu la kijani lakini usilimenye maganda kisha lipasue kama ulivyofanya kwenye viazi weka kwenye chombo chake

3. Chukua bamia likate vipande vidogo kisha weka kwenye chombo chake
Kisha bandika kikaangio weka Mafuta hadi yapate moto kisha weka vile viazi vikaange kama unavyokaanga chipsi na hakikisha visiwe vitepe kisha weka kwenye bakuli

4. Kisha kaanga mabiringanya hadi yawe brown kidogo (yakizidi brown yanakua machungu) kisha uweke kwa juu ya vile viazi ulivyovikaanga

5. Chukua bamia kaanga hadi ziwe brown kisha weka juu ya zile biringanya na viazi ulivyovikaanga

6. Pika mchuzi mzito kama rosti hakikisha unautia vitunguu swaumu, karoti na ndimu na viungo vyote vya mchuzi. Kisha mwagia mchuzi wako kwenye ule mchanganyiko wako wa viazi ,biringanya na bamia ulizokaanga

Unaweza kula mboga hii kwa chapati au maandazi
View attachment 459604
Kwani hii ni mboga mkuu? Me nikajua ndo tutafute mboga

brain is the beautiful part of the body.
 
Nlidhani sambaro huwekwa na pilipili, ukiila kwenye birian hatari
Inategemea
Kila sambaro na upishi wake.
Wengine huweka pilipili, wengine mapapai mabichi, wengine embe changa, wengine huweka uwatu au mbegu za mgagani.
Alimradi tafarani jikoni.
Sambaro ya kulia biriani mara nyingi huwekwa mapapai mabichi, uwatu na mbegu za mgagani na pilipili ndefu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom