Pole sana kwamba ufanyaje usiambukizwe njia ambazo HIV huambukizwa ni kwa tendo la ndoa bila kutumia kinga,kuongezewa damu ya mtu mwenye vidudu vya ukimwi,kuchangia sindano,nyembe nk,kugusa damu,majimaji ya mgojwa wa ukimwi kama una mchubuko au kidonda(yaani contact ya damu yako na ya mgonjwa),mama kuambukiza mtoto wakati wa mimba/wakati wa kujifungua.
<BR><BR>ufanyaje.<BR>kama wewe ndo huwa unamfulia nguo uwe unavaa glove sababu nguo zaweza kuwa na damu au majimaji usigundue na wewe ukawa na mchubuko mikononi bila kujua ukaambukizwa.<BR><BR>Usichangie vyitu nilivyotaja kama nyembe,sindano nk.
kumbuka ukimwi hauambukizwi kwa kukumbatiana,kucheza pamoja,kushikana mikono,kula pamoja wala hauambukizwi kwa njia ya hewa mfano mgonjwa akikohoa nk.<BR><BR>Lakini ni muhimu zaidi kumuonyesha upendo wa hali ya juu na kumtia moyo na usijionyeshe sana kuwa unaishi naye kwa tahadhari sana ya kuogopa atakuambukiza.
<BR><BR>Atumie vyakula kama nyama,matunda kwa wingi,mboga za majani,ndizi,maharage na vyakula vingine vya kumsaidia kujenga mwili.<BR>Usiache kumpeleka kwenye clinic ya wagonjwa wa ukimwi/hosp. huko atapewa msaada zaidi.