Jinsi ya kuinstall windows au os ingine kwenye pc bila cd/flash

Jinsi ya kuinstall windows au os ingine kwenye pc bila cd/flash

Joeli

JF-Expert Member
Joined
Apr 25, 2011
Posts
4,941
Reaction score
3,417
kwa muda mrefu nilikuwa napata shida sana kila nnapodownload file lenye extension ya .iso, .daa, .img, na mengine ambayo yanakuwa na image za cd au dvd

ilinibidi kwanza ni extract content via winrar kisha nitumie vilivyomo, au ni burn kwenye cd kisha niitumie na cd natupa nikimaliza, sasa nimejikuta nna cd karibu mia mbili ambazo hata sizihitaji tena, nikaona huu ni ufujaji wa mali, nikawaza, hivi hakuna njia ingine, basi katika ufukunyuku nikagundua kitu,

kuna kitu kinaitwa poweriso, ultraiso na jamii zake , mwanzo nilizitumia kutengenezea bootable cd au images ila nikagundua feature ya muhimu ambayo mpaka leo imenifanya niachane na matumizi ya flash au cd katika kuinstall windows na kufungua mafaili ya .iso, .daa, .img, na mengine,

enough of stories, ngoja niwape nnachotaka kuwapa,

_______________________________________________________________

JINSI YA KUINSTALL WINDOWS AU OS INGINE KWENYE PC BILA CD/FLASH

_______________________________________________________________

1. Install Poweriso au yoyote utakayopenda (naipenda poweriso, ntatumia kuwaelekezea)
ukiinstall itatengeneza virtual drive manager(hii tutaitumia kutengeneza virtual drive)
cha kufanya
a) kwenye taskbar utaona ki cd cha njano, hebu ki click kisha
b) set number of drives,
c) chagua moja tu kwa kujifunzia sio mbaya
baada ya hapo ukienda kwenye my computer utaona kuna drive mpya imeongezeka (eg drive f:/)


2. nenda kwenye file lako la iso mfano "Win.8.Pro.x86.iso" right click kisha kwenye context menu chagua poweriso>mount > kisha chagua iyo virtual drive (eg: drive f:/) sasa ukienda kwenye my computer utaona iyo drive yako ina jina la iyo windows unayotaka kuinstall


3. hebu iclick au right click kisha run setup uone

voilaaaaa, baada ya hapo endelea na utaratibu wa kawaida kuinstall hiyo OS

TAHADAHARI: 1. kama unaformat iyo partition unayotaka kuinstall windows mfano unataka kuinstall windows kwenye c:/ basi hakikisha poweriso umeinstall kwenye parttion ingine eg D:/ na lile file la windows .iso liko kwingine zaidi ya c:/ unaweza liweka pia kwenye D:/

2. hakikisha poweriso virtual drive umetick autostart na automount (nenda options za poweriso kwenye taskbar)



_______________________________________________________


JINSI YA KURUN CONTENT ZA ISO BILA KU EXTRACT IYO ISO

_______________________________________________________

Fuata step 1, 2, na 3

hakikisha una unmount baada ya kumaliza shughuli zako


kwa leo inatosha au sio wadau. kama una maswali, maoni, vya kuongeza waweza tiririka hapo chini
 
Hiyo kitu niliwahi kufanya ila sikukumbuka kuinstall kwenye D bali kwenye C na nilipoanza process ilienda baadaye ikafikia pale ambapo inarestart ili kuendelea na installation lakini ikawa imekula kwangu kwa sababu C tayari imeshakuwa formatted. Sasa swali ni kwamba je, kama nimeinstall hiyo PoweIso kwenye D je wakati itakapo hitaji koboot from hiyo virtual drive ni nini kitakachoiwezesha kuwasiliana nayo kwa sababu ile system ambayo hupatikana kwenye C itakuwa haipo.
 
Hiyo kitu niliwahi kufanya ila sikukumbuka kuinstall kwenye D bali kwenye C na nilipoanza process ilienda baadaye ikafikia pale ambapo inarestart ili kuendelea na installation lakini ikawa imekula kwangu kwa sababu C tayari imeshakuwa formatted. Sasa swali ni kwamba je, kama nimeinstall hiyo PoweIso kwenye D je wakati itakapo hitaji koboot from hiyo virtual drive ni nini kitakachoiwezesha kuwasiliana nayo kwa sababu ile system ambayo hupatikana kwenye C itakuwa haipo.

soma kwenye tahadhari namba mbili, ikirestart tu itakumbuka kuwa ilikuwepo so itaendelea ilipoishia
 
mii naopmba unisaidie nina mac book yangu kwa sasa haifanyi kazi inaboot haimalizi inazimika iliwahi kunitokezea mara moja na nikaiformat kwa kutumia cd ambazo nilinunulia ilikua original mac os x 10.5 zile cd zemepotea nimajeribu ku download
hiyo hiyo mac os x 10.5 nimeipata amabayo imekuja format ya dmg lakini nikitaka ku burn inanikatalia naomba unijuilishe nitumie format gani iso ao dmg mashine yangu ni mac book white 13 katika ku burn nilitumia nero on windows 7
 
hii kitu nilikuwa natumia kitambo sana kumbe kulikuwa na watu hawajui bado... sio mbaya lakini umejitahidi
 
mkuu and hw to install OS computer by USB flash Drive?:A S 39::help:
 
mkuu and hw to install OS computer by USB flash Drive?:A S 39::help:

windows; tumia win2flash

copy contents za cd kwenye hard drive kisha tumia win2flash kuhamisha kwenye flash na kuifanya bootable

linux distros karibu zote; tumia UNetbootin, huitaji kuextract, fuata maelekezo

ios: sijui/sijawahi install kabisa

note; boot order weka usb hdd iwe ya kwanza na ui enable
 
Back
Top Bottom