DavidDaudiMollel
Member
- Jan 20, 2014
- 32
- 49
Kumekuwa na watu wengi ambao wamekuwa wakilalamika simu zao kuwa slow wakiwa wanatumia na hivyo kushindwa kufurahia simu zao..
leo nitajitahidi kuelezea njia za kuweza kuzitumia kuwezesha simu yako kutokuwa slow pasipo kujali ukubwa wa uwezo wa simu ama udogo wa simu.
1. Epuka kupakua program ambazo sio muhimu na zisizotambulika.
kwamfano kupakua program za keyboard ilihali simu inakeyboard yake maalum na program zenye matangazo ya popup (ads).. unashauriwa kuwa program chache na muhimu katika simu yako.
2. Epuka kuwa na vitu vingi katika simu
ukitaka kufurahia simu yako siku zozote hakikisha vitu havizidi robo tatu ya uwezo wa simu yako katika uhifadhi.. yani kama storage yako ni GB 8 hakikisha vitu visijae hadi kufikia labda GB 6.5.
3. Kufuta kumbukumbu za muda (Clear Cache data)
kila unachokifanya katika simu yako huifadhiwa hapa kwa muda maalum na uhifadhi huo hutumia uwezo wa simu katika kujihifadhi kwake hivyo unashauriwa kuifuta mara kwa mara.
4. Punguza idadi za homescreen na widgets katika kioo cha simu yako
nivyema homescreen ya simu yako ikawa nimoja na ikawa na program chache tuu na muhimu katika matumizi yako.
5. Futa / stopisha program zinazofanya kazi wakati wewe huzitumii (Delete Running Progams)
unaweza kufanya hivyo kwakubinya kitufe cha menyu kuu (Home key) kisha utaona neno swipe data.
6. Epuka kutumia wallpaper zinazozunguka.
7. Update simu yako mara kwa mara.
hii husaidia kuongeza uimara katika simu yako na kuifanyia marekebisho na pia update programs zako mara kwa mara.
8. Epuka kutouch simu yako / kuitumia mikono ikiwa michafu.
uchafu wa screen yako mfano mafuta/maji hutatiza simu yako nakuiweka katika wakati mgumu wa kimaamuzi kwa kuwa uchafu kama mafuta na maji husababisha simu kupokea amri ya kimatumizi (Commands) na hivyo kuifanya simu kustuck(kusimama kufanya kazi)
siku zote hakikisha simu yako iko katika hali ya usafi na mikono yako nimisafi wakati unaitumia.
8.Restart simu yako mara kwa mara
hii husaidia kwakiasi kikubwa.
samahani nimechanganya lugha kwakuwa kuna ambavyo nashindwa kuelezea kwa kiswahili ila hata kama sijaelezea vyema natumai utakuwa umepata mawili matatu..