Siamini kama twiga wametoroshwa na kusafirishwa kwenda nje ya nchi bila serikali kujua.
Kinachonifanya nisiamini ni maswali haya:
1. Ni dhahiri kuwa maeneo ambako twiga wanaishi (mbugani) serikali imeweka watumishi mbalimbali wanaohusika na ulinzi na usalama.
2.ni dhahiri pia kuwa viwanja vya ndege vyote vinalindwa na maofisa na maafisa wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama yaani polisi, usalama wa taifa, takukuru, uhamiaji nk.
3. Ni dhahiri pia kabla ya mgeni yeyote kutoka nje kuingia nchini pasi yake ya kusafiria inakaguliwa na wenzetu wa uhamiaji.
4. Ni dhahiri kuwa mgeni husika lazima atakuwa ameeleza nini amekuja kufanya hapa nchini.
Sasa mimi sijui kutokana na maswali hayo hapo juu kwanini suala la kutoroshwa twiga wetu anahukumiwa maige peke yake.
Sijui pia vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vilikuwa wapi hadi wanyama warefu kuliko wote wanakimbizwa uarabuni bila mkuu wa nchi kupata taarifa na hata mzee nahodha, hussein mwinyi nao hawakumweleza mkuu wa kaya juu ya hilo?
Haya hao mbali, mkuu wa usalama wa taifa, igp, na mkurugenzi mkuu wa uhamiaji nao walikuwa wapi?
Mimi nahisi hao twiga walitoroshwa kwa maelekezo ya mkuu zaidi ya hao mawaziri na wakuu wa taasisi za ulinzi na usalama. Maana bado tunakumbuka wale mbuni walivyoisha pale mjengoni ikulu wakati fulani. Walipungua taratibu hadi kuisha. Au twiga wameondoka kwa mtindo huo huo lakini lawama zote kwa maige? Kidumu chama cha mapinduziiiiiiiiiiiiii.
Tena mabaya zaidi walichukuliwa kwa ndege ya jeshi je watu wakitengo cha anga walikuwa wapi ndege ya jeshi inaingia kwenye anga letu inashuka na inachukua twiga wao bila kuhoji??Hapa nikuwa kila kitu kilikuwa kimekuwa organized na document zote zilionyesha uhalali wakuchukua twiga!!Maige kaangukiwa na jumba bovu!
Maige alifanya nini baada ya kujua twiga na wanyama wengine wameporwa? alitakiwa kujiuzulu siku ya kwanza alipogundua kuwa wenzake wamemzunguka; angekuwa shujaa!
Siamini kama twiga wametoroshwa na kusafirishwa kwenda nje ya nchi bila serikali kujua.
Kinachonifanya nisiamini ni maswali haya:
1. Ni dhahiri kuwa maeneo ambako twiga wanaishi (mbugani) serikali imeweka watumishi mbalimbali wanaohusika na ulinzi na usalama.
2.ni dhahiri pia kuwa viwanja vya ndege vyote vinalindwa na maofisa na maafisa wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama yaani polisi, usalama wa taifa, takukuru, uhamiaji nk.
3. Ni dhahiri pia kabla ya mgeni yeyote kutoka nje kuingia nchini pasi yake ya kusafiria inakaguliwa na wenzetu wa uhamiaji.
4. Ni dhahiri kuwa mgeni husika lazima atakuwa ameeleza nini amekuja kufanya hapa nchini.
Sasa mimi sijui kutokana na maswali hayo hapo juu kwanini suala la kutoroshwa twiga wetu anahukumiwa maige peke yake.
Sijui pia vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vilikuwa wapi hadi wanyama warefu kuliko wote wanakimbizwa uarabuni bila mkuu wa nchi kupata taarifa na hata mzee nahodha, hussein mwinyi nao hawakumweleza mkuu wa kaya juu ya hilo?
Haya hao mbali, mkuu wa usalama wa taifa, igp, na mkurugenzi mkuu wa uhamiaji nao walikuwa wapi?
Mimi nahisi hao twiga walitoroshwa kwa maelekezo ya mkuu zaidi ya hao mawaziri na wakuu wa taasisi za ulinzi na usalama. Maana bado tunakumbuka wale mbuni walivyoisha pale mjengoni ikulu wakati fulani. Walipungua taratibu hadi kuisha. Au twiga wameondoka kwa mtindo huo huo lakini lawama zote kwa maige? Kidumu chama cha mapinduziiiiiiiiiiiiii.
Unachosema kimesemwa na watu wengi sana hapa JF. Hakuna waziri mwenye nguvu ya kutorosha wanyama hai bila kupata go-ahead ya Ikulu. It's a known fact. Kitu watu wengi walichokuwa wanataka ni kumwona waziri mhusika anachukua responsibility hiyo ya kutoroshwa hao wanyama kwa sababu wamechukuliwa kwenye "watch" yake. Most people know who the main player is and now that the minister has been tossed, we hope he will become bitter enough to name the culprit(s). Actually kama wabunge wataendelea kupress kuwajibishwa kwa hawa wezi kisheria, nahisi hii serikali haitafika 2015. Naona hii soap opera yetu imeanza rasmi. Sit back, grab a drink and keep your eyes peeled!