Jibu la prof Sheriff kwa prof Tibaijuka

Watu kama Zakia (waliozaliwa znz) na kiushi bara wako wengi bara. Vile vile Wabara (waliozaliwa Tanganyika ) na wanaishi Zanzibar . Watu wa aina hii hawawakilishi serikali za mahala alipozaliwa. Niliwahi kuishi jimbo la Amaan Zanzibar 80s, wakati huo mbunge wetu alikuwa mzaliwa wa Tanganyika Mh, Justus Issak na aliwakilisha jimbo letu kama mbunge kutoka Zanzibar.

Baraza la mapinduzi kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa kutoka baraza la wawakilishi halikua na taarifa officially kuhusu nini kinaombwa na ujumbe wa pr.A. Tibaijua UN. Kama Baraza la Mapinduzi lingekuwa na taarifa basi maelezo yote yengejibiwa na Balozi Seif Iddi. Baada ya Shamuhuna kukiri kama yeye binafisi alijua lakini baraza la Mapinduzi halijui. Hapa ilichezwa deal kwa makusudi . Kwasababu Tanganyika walijua Baraza la Mapinduzi au Baraza la wawakilishi lina wajumbe wa chama cha upinzani.

Kwahiyi mambo yalipitishwa kinyume cha sheria ilikufanikisha agenda zao. Tibaijuka alisema yeye alipewa ruhusa na boss wake kwenda UN. Lakini hukukua na taarifa ya mjumbe aliyetoka Zanzibar kwenye baraza la Mapinduzi ila Shamuhuna yeye ndio aliyemtuma . Baraza la Mapinduzi ndio chombo kikuu cha maamuzi yote ya serikali ya UMK.



Ndugu yangu Takishi sasa hapo tumlaumu nani? Shamhuna aliyesuka mpango na hata kumteua mwakilishi au Prof. Tibaijuka aliyeshirikiana na Shamhuna? Ingekuwa vituko kama Prof Tibaijuka hata baada ya majadiliano na waziri mwenziwe apande boti na kuwaeleza wawakilishi juu ya kile walichofikia! Na hapa ndio napata wasiwasi kwa nini mashambulizi yanakuwa kwa waziri wa bara na sio kwa upande wa Zanzibar? Muulizeni Shamhuna alishauriana nani?
 
Baraza la mapinduzi kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa kutoka baraza la wawakilishi halikua na taarifa officially kuhusu nini kinaombwa na ujumbe wa pr.A. Tibaijua UN. Kama Baraza la Mapinduzi lingekuwa na taarifa basi maelezo yote yengejibiwa na Balozi Seif Iddi. Baada ya Shamuhuna kukiri kama yeye binafisi alijua lakini baraza la Mapinduzi halijui. Hapa ilichezwa deal kwa makusudi . Kwasababu Tanganyika walijua Baraza la Mapinduzi au Baraza la wawakilishi lina wajumbe wa chama cha upinzani..

Hivi nyinyi Wazanzibari mbona mna vichwa vigumu kuelewa. Ngoja nirudie kile walichojaribu kusema wenzangu. Kama ilivyo kwa BLW pia bunge la JMT halikushirikishwa kwenye jambo hili. Sio kila jambo lazima liende kwenye bunge JMT au BLW. Serikali zote mbili ile JMT na SMZ vilihusishwa kikamilifu.

Hili jambo lilipita kwenye baraza la mawaziri wa JMT ambamo wapo wajumbe kutoka ZNZ, kama Dr. Shein (waziri asiye na wizara maalumu), Dr. Bilal (VP), Shamusi Vuai Nahodha, Omari Nundu etc. Hawa wote ni Wazanzibari.

Akili za kwako changanya na za mbayuwayu, TAFAKARI, Hivi unafikiri huyo Shamuhuna alitoraka kwenda UN? Ndiyo maana nikakwambia changanya akili. Ukweli dhahiri shahiri ni kwamba serikari ya JMT ilikuwa ikifahamu jambo hili, SMZ ilifahamu vizuri jambo hili, ndiyo maana akimutuma Shamuhuna kwenda UN kuiwakilisha. BLW kutofahamu that is another cup of tea. Luckily enough SUK ZNZ inao wajumbe wa CUF.

Ndiyo maana CDM mojawapo ya mapendekezo yao ktk katiba mpya ni kupunguza madaraka ya Rais, kwa kudhibitiwa na bunge. Kama hao mawaziri wote amewateua yeye single handed nani ana ubavu wa kumakatalia matakwa yake ndani ya baraza la mawaziri?! Lakini kama jambo hili lingekuwa linapelekwa bungeni kuidhinishwa inabidi Rais ajishauri mara mbili mbili, hasa kama ni shauri controversial au la kipumbavu.

Huu mgongoro wote umelala kwenye mambo makuu mawili 1. MUUNDO MBOVU WA MUUNGANO na KATIBA MBOVU YA JMT. Next time tieni akili vichwani, Tundu Lissu ataka powaeleza huo ukweli. Achaneni na huyo Moyo mnaye muona leo shujaa, ni "nunga yembe" jingine, muulizeni alifanya nini kurekebisha hizo kasoro alipokuwa madarakani?.

Kwa ujinga wenu, no wonder mnaongozwa na Rais ambaye in the first place hakutakiwa kuwemo hata kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi. Dunia yote inafahamu kwamba 2010, Dr. Shein alikuwa hajakaa Zanzibar kwa miaka mitano mfululizo ili ku qualify kupata kitambulisho cha "Mzanzibari mukaazi" Kigezo hicho ndiyo kinampatia haki Mzanzibari kuchagua au kuchaguliwa kuwa kiongozi. Lakini Shein hakuwa na Sifa hiyo lakini bado mukauziwa mbuzi kwenye gunia!
 
Je Prof. Sheriff amepambanua manufaa ya kuongeza ukanda wa bahari kwa URT na SMZ?. Je unapopeleka mshenga unamchangua mtu goigoi au mtu anayeweza kukuwakilisha vema?? Je Prof. anahoji uhalali wa mamlaka ya Rais ya kuchagua Prof. Tibaijuka?? Nini mzizi wa hoja yake. Je hajui kama Prof. Tiba alikuwa DG wa UN Habitat kwa hio anaenda kuongee na watu wanaomfahamu???.
 
Kama hali ni hii, sioni sababu ya kuwa na wazanzibari kwenye serikali ya muungano, wala hakuna haja ya kuwa na wabunge wa zanzibar kkwenye bunge. Maana kama maamuzi yeyote lazima uwasiliane na Baraza la wawaikilishi na SMZ, sasa hii gharama mkulima na mfanayakazi wa bara anabebeshwa ya nini kwa watu hawana hata mwamana?

Waondoke, ili tujue na waku deal naye kwisha.
 
Mkono ukikukosea unatakiwa kuukata uutupe!!!. Ni wakati wa kuwatupa wazanzibar ili tuconcestrate na nambo yetu
 
Eti Zakia sio Mzanzibar! Hamjui ndie angekuwa Makamu Rais wa JMT tangu 2005 kwa uraia huo wa Zanzibar?
 
Hawa watu waajabu sana, Wakati wa hotuba ya Tundu Lisu bungeni akichambua mikanganyo ya muungano walipiga kelele sana hawa watu kumpinga, leo yanajitokeza mambo haohao wana piga tena kelele kama kundi la wehu. Ajabu sana.

mwehu sio lazima avue nguo hadharani hata matendo yake na maongezi yake utamgundua tu waacheni wapige kelelee weeee! usiku utakuja na asubuhi itafika tumewazoea hao walalamishi kama watoto wa kambo
 
Kinachotufaya tuukumbatie Muungano hata wanapotukanwa mawaziri ni hizi mali za asili "black Gold".

La sivyo zamani Muungano ungekuwa umeshavunjika. Mali mbaya sana hata utukanwe wewe umo tu.
Baadhi yetu tunaiona Zanzibar inaweza kuwa kama SriLanka nyingine Muungano ukivunjwa. Tamil Tigers unawaona dhahiri sasa.
 
Mnaukumbatia Muungano kwa kuuogopa Uislaam. Waacheni Wazanzibari na nchi yao, kama wana mafuta, hawana, hayo ni yao. Mpaka wanawatukana nyie mmo tu. Kwa nini zaidi? mnatutukanisha nchi nzima wengine hatuna haja na huu Muungano.

Mama FF hatukumbatii muungano kwa Sababu unazozitaja... Binafsi si mnazi Wa muungano natamani uvunjike hata kesho na wala si suala la serikali 3 nataka kila mtu ashike njia yake.... Kitu tunachotaka wazanzibari wawe wazi wasipindishe mambo na wawe na msimamo ... Wasilete choko choko wakati lengo lao ni kwamba hawataki muungano....
Hii kupinda pinda ndio inayoleta shida zaidi....
 
Mnaukumbatia Muungano kwa kuuogopa Uislaam. Waacheni Wazanzibari na nchi yao, kama wana mafuta, hawana, hayo ni yao. Mpaka wanawatukana nyie mmo tu. Kwa nini zaidi? mnatutukanisha nchi nzima wengine hatuna haja na huu Muungano.

Nani anautaka Muungano? Siku zote muungano huu umekuwa na manung'uniko toka pande mbili lakini yalifumbiwa macho, na wengine wameonekana kama wahaini walipojaribu kubainisha kasoro za muungano. Dawa ni moja kuuvunja, hata mwanaume kama umeoa mwanamke lakini ndani ya ndoa hiyo hakuna maelewano dawa ni talaka tu. Mimi siku huu usanii unaoitwa muungano ukifa nitafanya tafrija kubwa na FF nitakualika.Tuwaache Wazanzibari na mafuta yao na sisi Watanganyika tufanye mageuzi tufute mikataba ya kinyonyaji tufaidi madini yetu yanayoporwa mchana na usiku kwa mgongo wa uwekezaji.Si wachukii Wazanzibari bali nauchukia Muungano huu feki.
 
HABARI ZENU,

The controversy about the extension of the sea boundary has come at the right time when Zanzibaris have shown that they will no longer be hijacked when their vital national interest are at stake, regardless of party affiliation. It was rather disingenuous for Prof Tubaijuka to try to introduce party divisions when she claimed that CUF was claiming that Zanzibar was not consulted.

If she heard the debate in the House of Representatives, it was almost unanimous, and prominent CCM backbenchers made a point of saying that this was not the question of CUF but of the whole of Zanzibar. She should not try to divide Zanzibaris again. We have suffered enough from such tactics.

It seems that mainland leaders feel that if you have a few Zanzibaris in your gang, then Zanzibaris are represented – and it is never difficult to get a few vibaraka, as we know all too well from our history. The question is whether the people in Zanzibar even knew this business was cooking – certainly the House of Representatives, a body that was elected by the whole people of Zanzibar, did not know about it until the professor was in New York presenting the document to the UN. I and many of my friends who try to keep up with events affecting our country were taken by surprise.

Prof Tibaijuka may be right that some people even in the Zanzibar Government may have been aware of this project, but the Minister of Lands in Zanzibar, Mr Shamhuna himself said in the House of Representatives that he know about it, but the Zanzibar Government did not know it officially.

The Executive Summary of Tanzania’s submission to the UN has 2 long lists of institutions and people who were involved in this project, but mentions only Shamhuna’s Ministry of Lands out of 9 institutions, and only one State Attorney from Zanzibar out of 8 members of the Technical Core Group.

Now Professor Tubaijuka mentions a few more names of Zanzibari ‘representative’, including my friend and former student Zakia Meghji, but if my memory serves me right, she used to be an MP for Moshi, and has never pretended to be representing Zanzibar except as a person who was born in Zanzibar. This is definitely a case of desperation in looking for Zanzibari faces.

But all this still does not cover the substantive issue involved. It is well known that Foreign Affairs is a Union matter, and therefore any dealings with the UN has to involve the Minister of Foreign Affairs, even if the exact issue involves only one side of our Union. There are plenty of cases when this has been done about issues concerning non-Union matters of Mainland Tanzania.

Therefore, it is not a favour to Zanzibar that once in a while the Ministry of Foreign Affairs has to take up the case when Zanzibar’s interests are concerned – it is our right, iof we are part of the Union. The same applies to the defence of Tanzania’s territorial boundaries, which include the now extended boundaries in the Indian Ocean – that is its responsibility.


But this does not mean that the Union Government therefore becomes the owner of all the resources within the territorial boundaries of Tanzania. The Articles of Union had defined 11 Union Matters that came under the Union Government, and the sea is not one of them. Since 1964, the Union Matters have been increased to 22, illegally according to Prof.

Shivji, but even in this extended list you will look in vain for the blue seas. It is for this reason that Prof. Tubaijuka is the Minister of Lands, Housing and Human Settlements Development (all non-Union matters), but the seas are not included. Why she was sent and not the Minister of Foreign Affairs is for the Union President to explain.


Therefore, it has to be admitted that since the oceanic resources are not a Union matter, but are of vital concern for the islands of Zanzibar which are surrounded by the sea on all sides, the people of Zanzibar have a direct stake in what is decided about their resources. And here it is not enough to mention a few names, however, highly placed they may be, and say Zanzibaris were represented.


The same argument was used in the case of the first draft of the Constitution Bill. Former Speaker Samuel Sitta claimed that Zanzibaris were consulted, naming the Zanzibar Minister of Good Governance and the AG, but it turned out that they were asked to submit their recommendations, but adopted only two out of 13, and threw the rest in the dustbin, and then went on to add many more without consulting even the Zanzibar Government.

Don’t they ever learn?

What the Representative Ismail Jussa was trying to do was to teach our Big Brother another lesson, and the mainland-based Swahili newspaper dares to ask him to apologise to Prof Tubaijuka?

I think it is Prof Tubaijuka and the Union Government that need to apologise to the people of Zanzibaris for trying once gain to take us for a ride. But as the old politician Hasan Nassor Moyo told Samuel Sitta, the new generation in Zanzibar is not the same as the old generation of the 1960s, and will not say ‘hewallah bwana.’

Abdul Sheriff
Harufu ya karafuu imegeuka kuwa harufu ya uozo!!
 
Kinachotufaya tuukumbatie Muungano hata wanapotukanwa mawaziri ni hizi mali za asili "black Gold".

La sivyo zamani Muungano ungekuwa umeshavunjika. Mali mbaya sana hata utukanwe wewe umo tu.


Kama kweli mafuta yapo kwenye mwambao wa visiwa vyao, hakuna sababu ya kuvunja muungano mpaka tuyanyonye kwanza
 
Baadhi yetu tunaiona Zanzibar inaweza kuwa kama SriLanka nyingine Muungano ukivunjwa. Tamil Tigers unawaona dhahiri sasa.

Na Mohammed Ghassani Nipo nje ya nyumbani kwa wiki moja na kitu sasa, lakini nafuatilia kwa karibu, kupitia mitandao, mambo yanavyoendelea kwetu. Nimeona kuwa kwa mara nyengine tena, Zanzibar imeonekana kwenye magazeti ya Tanganyika. Wenyewe, ukimtoa Mchungaji Christopher Mtikila na kaumu yake, hawataki waitwe Watanganyika. Wanajidai kwamba kuna Tanzania tu. Hata sherehe za jana za uhuru wa Disemba 9, wanaziita ni za uhuru wa Tanzania. Unafiki mtupu! Alaakullihali, turudi kwenye nukta. Zanzibar imetajwa katika magazeti ya Tanganyika
kwa matukio mawili: moja ni lile linalohusiana na kadhia ya Jumuiya ya Kiislam (OIC) na la pili ni la uchimbwaji wa mafuta. Yote mawili yamezishirikisha
serikali, wawakilishi, wanasiasa na wananchi wa kawaida. La kukumbushia Zanzibar kurejesha uanachama wake OIC, liliibuliwa, kama kawaida, na Chama cha Wananchi (CUF). Nasema kama kawaida, maana imekuwa ni ishara ya CUF kuipigania Zanzibar pahala popote pale wanapopata nafasi. Mimi ni katika watu wanaoamini kwamba miongoni mwa mambo makubwa ambayo yamewafanya CUF wafanikiwe Zanzibar, ni kujinasibisha kwao na usemaji na utetezi wa Zanzibar, eneo ambalo wenzao wa Chama cha Mapinduzi (CCM), labda kwa woga na hisia za kulipa fadhila, wako ziro kabisa. Katika semina ya kujadili Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania iliyofanyika Zanzibar mwishoni mwa mwezi uliopita, wawakilishi Said Ali Mbarouk na Rashid Saleh walisema kwamba umeshafika wakati wa Zanzibar kurudi katika jumuiya hiyo ya Kiislam, kwa hoja kwamba sasa sera ya nchi imebadilika kutoka ile ya kuzingatia siasa tu kwenye mahusiano na kuwa ile inayozingatia uchumi. Economic diplomacy, wasemavyo
Waingereza. Kwenye semina hiyo, ambapo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, alihudhuria, jibu la Serikali ya Muungano (SMT), kupitia kwake Waziri Membe, lilikuwa kwamba jambo hilo linajadilika, na akatoa matumaini kana kwamba litajadiliwa kweli. Lakini alikuwa anacheza siasa tu kwa kuwa alikuwa kwenye jukwaa la Zanzibar, mbele ya watu wanaojinasibisha na Uzanzibari wao. Kwa mtu kama yeye, ambaye ametokea kwenye system, anajuwa namna ya kucheza na akili za watu. Na akacheza nazo. Jibu hilo halikuipendeza kaumu ya Mchungaji Mtikila. Na kwa kuwa Makamo wa Rais, Ali Mohammed Shein (mwenyewe Mzanzibari na Muislam), alikuwa ndio kwanza amerudi ziara ya nchi za Misri na Iran, Mtikila akaunganisha yote mawili kuongelea kitu kimoja: chuki binafsi dhidi ya Uislam na Uzanzibari. Halafu, kama mchezo wa kuigiza, Wazanzibari nao wakaingia kichwa kichwa kuelekeza hasira
zao kwa Mtikila kama kwamba ni yeye ndiye anayeizuia Zanzibar kupata haki zake katika kizungumkuti hiki cha Muungano. Kwenye mtandao wa zanzinet.org, jukwaa la Wazanzibari linalojadili mausala mbali mbali kuhusu nchi yao, nilisoma maoni ya wachangiaji wengi wakimtaka Mtikila afumbe mdomo wake panapohusika masuala ya Zanzibar. ’Akosaye la kufanya, azinge mwana akalee’, mchango mmoja ulimwambia hivyo Mtikila ukimfananisha na mtu ambaye hana kazi ya kufanya. Lakini huko kulikuwa, na kumeendelea kuwa, sehemu ya mikakati ya SMT kupindisha hoja muhimu, hasa panapohusika hizi za Zanzibar. Nimesema kwamba Waziri Membe alikuwa akicheza politiki tu kule Zanzibar kuonesha kuwa eti kuna uwezekano wa kulijadili suala la Zanzibar na OIC. Ukweli hasa amekuja kuutoa Hussein Mwinyi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo Rais (Muungano), aliyesema wazi, Alhamis iliyopita, kwamba hakuna suala la mjadala katika hilo. Kwamba inayoweza kujiunga na OIC ni Tanzania, ikitaka, maana ndiyo nchi. Kwamba chini ya Katiba, si sawa kwa Zanzibar kuingia mashirikiano kama hayo. Huo ndio ukweli mkavu kutoka kwenye kinywa cha SMT yenyewe. Lakini katika aliyoyasema Waziri Mwinyi siku hiyo hiyo ni
kwamba mafuta ya Zanzibar hayajaweza kuchimbika kwa kuwa kwenye Tume ya Pamoja wa Waziri Mkuu Edward Lowassa na Waziri Kiongozi Shamsi Nahodha hakujakuwa na makubaliano. Hakusema, hata hivyo, ikiwa kilichokuwa hakijaafikiwa
kinatokana na kukataa kwa nani, ingawa dhana inatwambia kwamba wanaokataa ni
akina Waziri Kiongozi Nahodha. Huku nako kulikuwa ni kuweka mizani baina ya
mambo mawili tete. Upande mmoja wa mizani kuna ukweli kwamba suala la Zanzibar na OIC ndio limekwisha,
vyenginevyo Katiba ibadilishwe. Uzoefu unaonesha hakuna kitu kama hicho, yaani kuibadilisha Katiba kwa kufuata matakwa ya Zanzibar, bali kilichopo ni kinyume chake, yaani kuibadilisha Katiba kwa kuikandamiza Zanzibar. Wamefanya hivyo takribani mara 14 tangu
mwaka 1964. Upande huo wa mizani unatwambia wazi kuwa Wazanzibari tumepoteza. Upande mwengine wa mizani umetengenezwa
utuoneshe kuwa eti tuko madhubuti. Si akina Waziri Kiongozi Shamsi, Wazanzibari, ’wameweka ngumu’ na akina Waziri Mkuu Lowassa,
Watanganyika,
wameshindwa
kuyachimba? Si umadhubuti wa viongozi wetu huo? Lakini ukweli, hata kwa hili uko tafauti na hapo. Nitakuwa mtu wa mwisho kuamini kuwa Watanganyika
wameshindwa
kuyachimba mafuta ya Wazanzibari ati kwa kuwa Wazanzibari hao wameonesha ’ukaidi’ wa kuelewa (kama wanavyotwambia).
Siamini ikiwa kweli hawa jamaa wamedhamiria
kuyachimba mafuta yetu, watahitaji ridhaa yoyote kutoka kwetu. Hakuna uzoefu huo, na hauwezi kuwepo sasa. Hawa jamaa wakitaka kufanya leo kwetu hulifanya tu bila ya kujali hisia wala hasira zetu. Hoja ninayojaribu kuiwasilisha mbele yako hapa ni kwamba, panapohusika
Muungano na nguvu za Tanganyika kwa Zanzibar, chini ya utawala wa CCM, hakuna kitu kama hiari. Ni kile kinachoamuliwa na Tanganyika ndicho ’kizuri’ na kinachofanyika
Zanzibar, kutoka kuamua nani awe raisi wetu hadi vipi raisi huyo aiongoze Zanzibar yetu. Na huo nao ndio ukweli mkavu. Siku watakayoamua,
watayachimba. Sababu wanazo, uwezo wanao na nguvu za kufanya hivyo wanazo. Naomba nieleweke, kwamba sizungumzii uhalali wa Tanganyika kuyachimba mafuta ya Wazanzibari, bali nazungumzia kwamba uwezekano wa kufanya hivyo kuwa upo. Labda kwa kuandika hivi kuna watu watakaonichukulia
kuwa ni Mzanzibari niliyekwishavunjika
moyo na hatima ya nchi yangu ndani ya kizungumkuti cha Muungano huu, kwa upande mmoja, na wale watakaonichukulia
nanuka ubaguzi, kwa upande mwengine. Wa mwanzo ni Wazanzibari wenzangu, naamini, na wa pili ni Watanganyika au kaumu yao, nadhani. Kwa makundi yote mawili, mimi si mtu wa kuvunjika moyo kiasi hicho. Nimezaliwa miaka 13 baada ya Muungano wa 1964 ulioichukua Zanzibar kimzobezobe, na tayari nilifumbua macho nikikuta kwamba ’natakiwa kuisahau Zanzibar.’ Ndivyo mfumo
unavyotutayarisha sote. Lakini, kama ilivyo kwa mamia ya maelfu ya Wazanzibari wengine, nimegoma kuisahau nchi yangu na kuuzika Uzanzibari wangu. Tunawaachia wanaokaa
madarakani kuifanya kazi hiyo ya kuizika Zanzibar, lakini sisi tulio nje ya madaraka tumekataa kuhudhuria maziko wala kukaa matanga ya kifo cha Mama yetu, Zanzibar. Bado tuna moyo. Moyo wa kwamba Zanzibar ipo daima, ilikuwepo jana, ipo leo na itakuwepo kesho…… na milele. Akina Mtikila wanatwambia tuache kabisa kufikiria OIC ndani ya Muungano. Kwamba ikiwa tunataka kufanya hilo, labda tujitoe kwenye Muungano. Pamoja na ukweli kwamba hata pale Julius Nyerere alipomlazimisha Salmin Amour kujitoa kwenye jumuiya hiyo kwa kuwa alikiuka Katiba, alikuwa,
yeye mwenyewe Nyerere, anavunja Katiba, maana hadi hapo ushirikiano wa kimataifa haikuwa sehemu ya mambo ya Muungano, bado akina Mtikila wasidhani kwamba ni Wazanzibari wenye shida ya Muungano katika kiwango hicho cha kutwambia, ama tubakie au tutoke. Ni kiwango cha mwisho cha matusi kwetu, Wazanzibari. Hata kama tunajuwa kuwa watawala wetu wanaung’ang’ania
Muungano huu na mfumo wake kwa kuwa ndio wanaoutumilia
kujiweka na kujirejesha madarakani, hilo halitujumuishi sote katika kundi moja. Waingereza
walimwambia Tony Blair alipoamua kushirikiana na George Bush kwenda kuivamia Iraq: ’Not in our name.’ Vivyo ni kwa sisi, Wazanzibari. Ni kosa kudhani kwamba udhalilifu wote unaofanywa na utawala wa Tanganyika dhidi ya Zanzibar mbele ya macho ya hao waitwao viongozi wa Zanzibar, hufanyika kwa baraka zetu. Hapana. Na kwa uelewa huo, basi tusipeane ‘ultimatum’
 
Kelele hizi za muungano hazina tija, zinzkera na zinztupotezea muda kabisa ni bora ipitishwe kurea ya maoni tu wananchi waamue kila mtu achukue chake.
 
Wameanza kumruka Shamhuna pia wanamwita 'kibaraka' sijui mwisho wake utakua nini...nasahuri Shamhuna na wenzie waongezewe ulinzi.:A S-coffee:
 
nadhani kabla ya kutukana sana, ungekuwa msomi mwema kwa kutafuta na kumtambua huyu ni nani ? katika fani za elimu na duniani.

Haijalishi ni nani, na anaheshimika namna gani kokote kule duniani, Point ni kwamba, zaidi ya Kiingereza
kilichotumika kwenye post hii, hapa mpangalio wa hoja zake na mantiki ya kuhoji baadhi ya vitu alivyovihoji
unatufanya wengine tuuhoji uprofesa wake.

Japo sio sahihi kuunganisha mgando wa uprofesa wake na maprofesa wote wa zanzibar, sababu wapo
maprofesa wa zanzibar wamenifundisha mimi, nawakubali kuliko maprofesa wa Havard.

Sikutegemei kumsoma profesa anayehoji kwamba ni kwa nini kaenda huyu badala ya huyu?
Ila leo nimemsoma.

Ni nani kwanza huyu
 
Back
Top Bottom