Ahsante kwa taarifa. Jambo lingine kwa sisi tunaotumia website unapo taka kumtaja mtu kwa kuanza na alama '@' zinakuja suggestions za kutosha(jambo jema)
ila unapo taka ku scroll down ili upate jina unalilitaka ile list ina vanish je kunaweza kuwa na namna nyingine ya kuboresha hilo? Kama sijaeleweka sina nmna nyingine ya kueleza.
Tunatarajia kati ya saa 7 kamili usiku hadi saa 8 usiku wa leo (1:00am - 2:00am) kwa muda wa Afrika Mashariki kutakuwa na downtime (kutopatikana) kwa Mtandao wa JamiiForums ambayo imepangwa kwa ajili ya kuimarisha zaidi miundombinu yetu na kuboresha mambo kadhaa katika miundombinu.
Mabadiliko hayataonekana kwa macho bali experience ya JF upande wa ufungukaji (kasi) ndo itaongezeka.
Tusingeweza kufanya mabadiliko haya makubwa bila kwenda offline kutokana na sababu zisizoepukika. Mabadiliko mengine ya kimwonekano na upande wa app yatafanyika bila ya kwenda offline kabisa.
Kuna mada nyingi sisi hatutaki ziona japo wengine wanataka ziona kwanini usituwezeshe tuweze kuzuia kuona hizo mada.
Mfano mtu kaweka mada kuhusu ushoga na mimi sitaki ionekane kwangu
Au
Mtu anaandika utoto na mimi sitaki kuuona baada ya kusoma mara ya kwanza