Jeshi la polisi, bajeti na funding

Jeshi la polisi, bajeti na funding

Ked zee

Member
Joined
Aug 20, 2022
Posts
14
Reaction score
17
Serikali iangalie hili swala,kwa jicho la tatu.Jeshi la polisi ni nguzo muhimu katika usalama,amani na ulinzi kwa wananchi.

Matatizo mengi ya kiusalama kwa wananchi yanaweza kuepukika.Jeshi la polisi likiwa kinafanyi kazi kwa ufanisi.

Kwa nini nasema liongezewe bajeti na funding

Kwanza jeshi la polisi lina gari chache za kupiga doria na zinazo kaa standpoint. Gari za kufanya doria zinabeba askari zaidi ya 7,kitu ambacho kinafinya ukubwa wa doria.

Kwa sababu wanazunguka wengi kwa pamoja,serikali iongeze magari hasa madogo yanayoweza kutembea na askari wawili,ili zipata nafasi ya kuwa karibu na mitaa mingi.Na zipewe zone za kuzugukia.

Matukio kama ya panya road yanatokea kirahisi kwa sababu polisi wako mbali.Hata ikipigiwa simu mapema wanachelewa kwa sababu ya umbali.

Liongezewe ufanisi wa anga,kwa kuongeza helikopta. Ikitokea tukio kubwa kuwe na support ya anga.

Ubora wa vifaa vya mawasiliano,iwe rahisi walio kwenye doria kuwasiliana kwa kupeana taarifa za matukio. Pia iwepo bajeti ya jeshi la polisi kwenda kutoa semina kwa wananchi jinsi ya kuwasiliana na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi. Haraka pindi uhalifu unapotekea.Wanachi wengi bado hawajui namba ya simu ya kupiga polisi.

Jeshi la polisi ni nguzo muhimu.Serikali ifanye maboresho.
 
Ningeandika mengi ila kwa vile Niko busy kidogo.

Lakini jeshi la polisi ni kinyaa haswa. Unakuta hata gari lao Halina mafuta. Ukiwaita kuja kwenye tukio hadi uwawekee mafuta la sivyo watakuja wakipata mafuta hata kama ni kesho yake.
 
Ningeandika mengi ila kwa vile Niko busy kidogo.

Lakini jeshi la polisi ni kinyaa haswa. Unakuta hata gari lao Halina mafuta. Ukiwaita kuja kwenye tukio hadi uwawekee mafuta la sivyo watakuja wakipata mafuta hata kama ni kesho yake.
Hapo jamaa washafanya ualifu na kusepa.
 
Back
Top Bottom