GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,426
- 120,784
Katika hali isiyokuwa ya kawaida na pia ni ya kusikitisha Shirikisho la Soka barani Africa ( CAF ) jana limesikitishwa na kitendo cha Idara ya Mawasiliano na Habari ya Klabu ya Yanga ( ambayo inaongozwa na Jerry Muro ) kwa kutokujua tararibu nzima za utoaji na upokeaji wa taarifa za Shirikisho hilo.
Kitendo ambacho CAF wamesikitika nacho ni baada ya kuona Klabu ya Yanga kupitia Idara yake hiyo ya Mawasiliano na Habari kuamua kujipangia wao siku, tarehe na muda wa mchezo wao dhidi ya TP Mazembe kinyume na taratibu za CAF ambazo hata hivyo zipo wazi na Mtu yoyote anaweza akazitafuta na kuziona.
Moja ya taratibu za CAF zinasema kuwa timu yoyote mwenyeji wa mchezo inatakiwa kutoa taarifa yake ya mechi siku tatu ( 3 ) baada ya kumaliza tu kucheza mchezo wake wa ugenini na si Siku ya nne ( 4 ) kama walivyofanya Yanga kupitia Msemaji wao Jerry Muro.
Kutokana na " upuuzi " huu wa Idara au Kurugenzi ya Mawasiliano na Habari Ya Klabu ya Yanga ambayo kwa 101% inaongozwa, kusimamiwa na kuratibiwa na Jerry Muro Shirikisho la Soka barani Afrika CAF limekataa ombi la Yanga la kucheza mchezo wao huo tarehe 29 Siku ya Jumatano ijayo na Saa 1 usiku na badala yake CAF imesema mchezo huo utachezwa tarehe ile ile ( ambayo hata hivyo nasikia Mganga wa Yanga aliikataa kwani Kinyota inaonyesha Watafungwa magoli mengi ) ya 28 ambayo itakuwa ni Siku ya Jumanne na muda ni Saa 10 jioni.
Kwa haya yaliyoitokea Klabu ya Yanga ukiwa kama mtu mweledi na unayejua nini unafanya utagundua kuwa Msemaji wao Jerry Muro ametuaibisha sana Watanzania mbele ya CAF kwani kwa " upuuzi " wake hatoonekana ni yeye tu ndiye mwenye matatizo bali sasa tutaonekana Watanzania wote ni " mbayuwayu ". Vile vile kwa hicho kitendo Jerry Muro ameiabisha sana Klabu yetu / yangu ya Yanga na nashangaa kwanini mpaka sasa Viongozi wa Yanga bado wanamkodolea tu macho huyu Msemaji kwani amefanya Kosa kubwa sana tena la KIULEDI na KITAALUMA na hakupashwa hadi sasa hivi naandika hii taarifa kuendelea kuwepo Yanga.
Lakini kama haitoshi Jerry Muro amewakosea sana wenye TAALUMA yao ya Mawasiliano na Habari kwa hicho kitendo alichofanya kwani moja ya SIFA kubwa ya Mtu yoyote wa Mawasiliano na Habari ni muda wote kuwa na UFAHAMU mkubwa wa mambo, kufuatilia mambo kwa UMAKINI mkubwa na kuwa ni mtu mwenye MAARIFA huku muda mwingi akitakiwa KUJIONGEZA.
Nilichokigundua ni kwamba Msemaji wa Yanga Jerry Muro anatumia 99% ya Kazi zake katika KUJISIFU, kuisema SIMBA SPORTS CLUB, kujiita wa KIMATAIFA, kuzungumza tu kwa MIKOGO jinsi anavyopanda NDEGE na safari ya Ndege itakuwaje utadhani labda yeye ndiyo Rubani ( PILOT ) wa hiyo Ndege na kusema kuwa anaishi Mbezi Beach na ameoa Mke Mzungu na hiyo 1% tu iliyobaki ndiyo huitumia pekee katika kufanya Kazi muafaka za Yanga.
Nikiwa kama Mdau wa Michezo na Mwana Yanga tena wa KUFA KUFA kabisa naomba UONGOZI wa Yanga umwangalie huyu Msemaji wetu Jerry Muro kwa jicho la Tai ( Eagle ) kwani kwa makosa haya ya KIZEMBE kuna siku hakika atakuja kutugharimu sisi Wana Yanga na tutajuta mno. Uongozi wetu wa Yanga tafadhalini hebu tusaidieni kwani huu mchezo wetu na TP Mazembe isingekuwa UZEMBE wa huyu Msemaji wetu basi tungeucheza siku ile ile ambayo Mganga wetu wa PEMBA alitaka tuucheze ambapo tungeshinda goli 7 na sasa kwa kitendo cha Msemaji wetu kutokuwa na TAARIFA na UFAHAMU mkubwa wa KIMAWASILIANO na Watu wa CAF nina uhakika sasa kuwa hizo goli saba ( 7 ) sasa tutafungwa sisi hiyo Jumanne ijayo ya tarehe 28 huo muda wa Saa 10 jioni.
Jerry Muro muda ndiyo huu JIUZURU kwani bado hujachelewa!
Nawasilisha.
Kitendo ambacho CAF wamesikitika nacho ni baada ya kuona Klabu ya Yanga kupitia Idara yake hiyo ya Mawasiliano na Habari kuamua kujipangia wao siku, tarehe na muda wa mchezo wao dhidi ya TP Mazembe kinyume na taratibu za CAF ambazo hata hivyo zipo wazi na Mtu yoyote anaweza akazitafuta na kuziona.
Moja ya taratibu za CAF zinasema kuwa timu yoyote mwenyeji wa mchezo inatakiwa kutoa taarifa yake ya mechi siku tatu ( 3 ) baada ya kumaliza tu kucheza mchezo wake wa ugenini na si Siku ya nne ( 4 ) kama walivyofanya Yanga kupitia Msemaji wao Jerry Muro.
Kutokana na " upuuzi " huu wa Idara au Kurugenzi ya Mawasiliano na Habari Ya Klabu ya Yanga ambayo kwa 101% inaongozwa, kusimamiwa na kuratibiwa na Jerry Muro Shirikisho la Soka barani Afrika CAF limekataa ombi la Yanga la kucheza mchezo wao huo tarehe 29 Siku ya Jumatano ijayo na Saa 1 usiku na badala yake CAF imesema mchezo huo utachezwa tarehe ile ile ( ambayo hata hivyo nasikia Mganga wa Yanga aliikataa kwani Kinyota inaonyesha Watafungwa magoli mengi ) ya 28 ambayo itakuwa ni Siku ya Jumanne na muda ni Saa 10 jioni.
Kwa haya yaliyoitokea Klabu ya Yanga ukiwa kama mtu mweledi na unayejua nini unafanya utagundua kuwa Msemaji wao Jerry Muro ametuaibisha sana Watanzania mbele ya CAF kwani kwa " upuuzi " wake hatoonekana ni yeye tu ndiye mwenye matatizo bali sasa tutaonekana Watanzania wote ni " mbayuwayu ". Vile vile kwa hicho kitendo Jerry Muro ameiabisha sana Klabu yetu / yangu ya Yanga na nashangaa kwanini mpaka sasa Viongozi wa Yanga bado wanamkodolea tu macho huyu Msemaji kwani amefanya Kosa kubwa sana tena la KIULEDI na KITAALUMA na hakupashwa hadi sasa hivi naandika hii taarifa kuendelea kuwepo Yanga.
Lakini kama haitoshi Jerry Muro amewakosea sana wenye TAALUMA yao ya Mawasiliano na Habari kwa hicho kitendo alichofanya kwani moja ya SIFA kubwa ya Mtu yoyote wa Mawasiliano na Habari ni muda wote kuwa na UFAHAMU mkubwa wa mambo, kufuatilia mambo kwa UMAKINI mkubwa na kuwa ni mtu mwenye MAARIFA huku muda mwingi akitakiwa KUJIONGEZA.
Nilichokigundua ni kwamba Msemaji wa Yanga Jerry Muro anatumia 99% ya Kazi zake katika KUJISIFU, kuisema SIMBA SPORTS CLUB, kujiita wa KIMATAIFA, kuzungumza tu kwa MIKOGO jinsi anavyopanda NDEGE na safari ya Ndege itakuwaje utadhani labda yeye ndiyo Rubani ( PILOT ) wa hiyo Ndege na kusema kuwa anaishi Mbezi Beach na ameoa Mke Mzungu na hiyo 1% tu iliyobaki ndiyo huitumia pekee katika kufanya Kazi muafaka za Yanga.
Nikiwa kama Mdau wa Michezo na Mwana Yanga tena wa KUFA KUFA kabisa naomba UONGOZI wa Yanga umwangalie huyu Msemaji wetu Jerry Muro kwa jicho la Tai ( Eagle ) kwani kwa makosa haya ya KIZEMBE kuna siku hakika atakuja kutugharimu sisi Wana Yanga na tutajuta mno. Uongozi wetu wa Yanga tafadhalini hebu tusaidieni kwani huu mchezo wetu na TP Mazembe isingekuwa UZEMBE wa huyu Msemaji wetu basi tungeucheza siku ile ile ambayo Mganga wetu wa PEMBA alitaka tuucheze ambapo tungeshinda goli 7 na sasa kwa kitendo cha Msemaji wetu kutokuwa na TAARIFA na UFAHAMU mkubwa wa KIMAWASILIANO na Watu wa CAF nina uhakika sasa kuwa hizo goli saba ( 7 ) sasa tutafungwa sisi hiyo Jumanne ijayo ya tarehe 28 huo muda wa Saa 10 jioni.
Jerry Muro muda ndiyo huu JIUZURU kwani bado hujachelewa!
Nawasilisha.