Jen. Ulimwengu: Ni vyema Rais Magufuli asishiriki utawala wa mikusanyiko ya halaiki

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
53,679
120,361
Majuzi tu, katika mkutano wa hadhara, Rais John Magufuli alikuwa akiwauliza watu “Nitumbue, nisitumbue?” na watu wakamjibu kwa sauti moja “Tumbua!”

Mikutano ya aina hii, na majibizano ya aina hii baina ya mkuu wa nchi na wananchi wake yanaweza kutoa taswira ya mkuu ambaye amefungamana na watu wake kiasi kwamba anafanya yale tu ambayo wananchi wake wanataka ayafanye, na hili litaonekana kama jambo jema.

Lakini pia ni jambo la hatari, nami nitaeleza. Mimi sina tatizo kubwa na watendaji wa umma “kutumbuliwa” ingawa silipendi sana neno hilo. Silipendi kwa sababu ile ile niliyokwisha kuisema, kwamba tatizo linaloikabili nchi hii si majipu, bali ni saratani, na hakuna utaalamu wa kuitumbua saratani.

Tunaweza kuendelea na kelele za “utumbuaji” hadi miaka mitano ikakatika bila kuona matokeo ya kweli kwa sababu tu tulikuwa hatujabaini tatizo ni nini. Sisi tumefanywa tuamini ni majipu kumbe ni tatizo la msingi zaidi.

Mantiki ya kawaida inaniambia kwamba huyo mtuhumiwa atakuwa tayari amekwisha kupachikwa nembo ya “ufisadi’ kutokana na jinsi alivyotangazwa na mkuu kwenye ule mkutano wa hadhara na wananchi wakamwitikia mkuu kwa kusema kwa sauti moja, “Tumbua!”

Hali hii haina tofauti kubwa sana na utawala wa imla wa mkusanyiko wa halaiki. Pamoja na nia njema kabisa, mkuu anaweza kutumia nguvu ya magenge. Daima wanasiasa watakuwa ni wanasiasa, na si watoa haki. Wanachotaka wanasiasa ni kuona kwamba wanakubalika mbele ya halaiki ya watu na kila wafanyacho kinashangiliwa.

Katika hali tuliyo nayo leo hii, na najua kwamba hali hii imegubikwa na uozo tulioachiwa na watawala wetu waliopita, kuna umuhimu mkubwa wa kupambana na uozo huo. Lakini mapambano hayo hayana budi kuwa na utaratibu unaojulikana, utaratibu unaotabirika. Hili ni muhimu sana kiasi kwamba sijui kama linaweza kuwa na maelezo ya kutosha.

Hatuna budi kujenga utamaduni wa kufuata kanuni, taratibu, sheria na katiba, hata kama tunawashughulikia wale tunaodhani ni waovu. Hatuna haki ya kutenda maovu kwa sababu tu eti tunapambana na watu waovu. Kama tuna uhakika kwamba ni waovu, basi itakuwa rahisi kudhihirisha uovu wao.

Kama tumeshindwa kudhihirisha uovu huo, basi hatuna budi kukiri kwamba kesi yetu ni dhaifu kwa sababu ama wapelelezi wetu hawafai ama kesi yenyewe ilijengwa juu ya misingi ya hisia na siyo hali halisi


Tamko la Rais Magufuli kwamba hata hao wanaotetea majipu nao ni majipu pia linatia hofu ya kweli kwamba tumeanza kuserereka.

Namuomba Rais Magufuli aiangalie tena kauli hii tusije tukajikuta katika mashaka makubwa.


Mashaka hayo nayaona kwa njia mbalimbali, lakini mojawapo ni ile ya wateule wa Magufuli watakaopenda kuchukua hatua zitakazomfurahisha bosi wao, hata kama hatua hizo si sahihi.

Si kila mara tutaweza kupata taarifa za watu walioonewa huko wilayani au vijijini kwa sababu tu wameshukiwa kuwa “mafisadi” au watetezi wa “majipu” ambao nao wanageuka kuwa “majipu”.

Katika matatizo makubwa ambayo nchi hii haina budi kukabiliana nayo, mojawapo ni lile la watu kutotaka kutendeana haki bila mizozo isiyokuwa na tija.
 
Majuzi tu, katika mkutano wa hadhara, Rais John Magufuli alikuwa akiwauliza watu “Nitumbue, nisitumbue?” na watu wakamjibu kwa sauti moja “Tumbua!”

Mikutano ya aina hii, na majibizano ya aina hii baina ya mkuu wa nchi na wananchi wake yanaweza kutoa taswira ya mkuu ambaye amefungamana na watu wake kiasi kwamba anafanya yale tu ambayo wananchi wake wanataka ayafanye, na hili litaonekana kama jambo jema.

Lakini pia ni jambo la hatari, nami nitaeleza. Mimi sina tatizo kubwa na watendaji wa umma “kutumbuliwa” ingawa silipendi sana neno hilo. Silipendi kwa sababu ile ile niliyokwisha kuisema, kwamba tatizo linaloikabili nchi hii si majipu, bali ni saratani, na hakuna utaalamu wa kuitumbua saratani.

Tunaweza kuendelea na kelele za “utumbuaji” hadi miaka mitano ikakatika bila kuona matokeo ya kweli kwa sababu tu tulikuwa hatujabaini tatizo ni nini. Sisi tumefanywa tuamini ni majipu kumbe ni tatizo la msingi zaidi.

Mantiki ya kawaida inaniambia kwamba huyo mtuhumiwa atakuwa tayari amekwisha kupachikwa nembo ya “ufisadi’ kutokana na jinsi alivyotangazwa na mkuu kwenye ule mkutano wa hadhara na wananchi wakamwitikia mkuu kwa kusema kwa sauti moja, “Tumbua!”

Hali hii haina tofauti kubwa sana na utawala wa imla wa mkusanyiko wa halaiki. Pamoja na nia njema kabisa, mkuu anaweza kutumia nguvu ya magenge. Daima wanasiasa watakuwa ni wanasiasa, na si watoa haki. Wanachotaka wanasiasa ni kuona kwamba wanakubalika mbele ya halaiki ya watu na kila wafanyacho kinashangiliwa.

Katika hali tuliyo nayo leo hii, na najua kwamba hali hii imegubikwa na uozo tulioachiwa na watawala wetu waliopita, kuna umuhimu mkubwa wa kupambana na uozo huo. Lakini mapambano hayo hayana budi kuwa na utaratibu unaojulikana, utaratibu unaotabirika. Hili ni muhimu sana kiasi kwamba sijui kama linaweza kuwa na maelezo ya kutosha.

Hatuna budi kujenga utamaduni wa kufuata kanuni, taratibu, sheria na katiba, hata kama tunawashughulikia wale tunaodhani ni waovu. Hatuna haki ya kutenda maovu kwa sababu tu eti tunapambana na watu waovu. Kama tuna uhakika kwamba ni waovu, basi itakuwa rahisi kudhihirisha uovu wao.

Kama tumeshindwa kudhihirisha uovu huo, basi hatuna budi kukiri kwamba kesi yetu ni dhaifu kwa sababu ama wapelelezi wetu hawafai ama kesi yenyewe ilijengwa juu ya misingi ya hisia na siyo hali halisi


Tamko la Rais Magufuli kwamba hata hao wanaotetea majipu nao ni majipu pia linatia hofu ya kweli kwamba tumeanza kuserereka.

Namuomba Rais Magufuli aiangalie tena kauli hii tusije tukajikuta katika mashaka makubwa.


Mashaka hayo nayaona kwa njia mbalimbali, lakini mojawapo ni ile ya wateule wa Magufuli watakaopenda kuchukua hatua zitakazomfurahisha bosi wao, hata kama hatua hizo si sahihi.

Si kila mara tutaweza kupata taarifa za watu walioonewa huko wilayani au vijijini kwa sababu tu wameshukiwa kuwa “mafisadi” au watetezi wa “majipu” ambao nao wanageuka kuwa “majipu”.

Katika matatizo makubwa ambayo nchi hii haina budi kukabiliana nayo, mojawapo ni lile la watu kutotaka kutendeana haki bila mizozo isiyokuwa na tija.
Maneno kuntu kabisa.
 
Aliyetumbuliwa mbele ya watu, uchunguzi wake ulishafanywa kwa muda mrefu na kamati iliyoundwa na mkuu wa mkoa wa Dar Paul Makonda. Sio kwamba Rais aliamua pale pale jukwaani, ndio maana baada ya hotuba akamuita mkuu wa mkoa aje aeleze kwa mara nyingine tena taarifa kumhusu mkurugenzi.
Thread inajaribu kujenga taswira kwamba uamuzi wa kumtumbua mkurugenzi wa jiji ulifikiwa pale pale jukwaani. Rais hawezi kuwa na uelewa mdogo wa mipaka ya kazi yake kiasi cha kuongozwa na mawazo ya halaiki.
Tukijaribu kukumbuka muda ule alipomfukuza kazi mkurugenzi, kuna suala jingine liliibuka na Rais akamuambia mkuu wa mkoa kwamba hilo suala lipo chini ya mamlaka yako.
Tujaribu kuweka kila kitu kwenye mizani kabla hatujakurupuka kutoa hukumu.
 
Aliyetumbuliwa mbele ya watu, uchunguzi wake ulishafanywa kwa muda mrefu na kamati iliyoundwa na mkuu wa mkoa wa Dar Paul Makonda. Sio kwamba Rais aliamua pale pale jukwaani, ndio maana baada ya hotuba akamuita mkuu wa mkoa aje aeleze kwa mara nyingine tena taarifa kumhusu mkurugenzi.
Thread inajaribu kujenga taswira kwamba uamuzi wa kumtumbua mkurugenzi wa jiji ulifikiwa pale pale jukwaani. Rais hawezi kuwa na uelewa mdogo wa mipaka ya kazi yake kiasi cha kuongozwa na mawazo ya halaiki.
Tukijaribu kukumbuka muda ule alipomfukuza kazi mkurugenzi, kuna suala jingine liliibuka na Rais akamuambia mkuu wa mkoa kwamba hilo suala lipo chini ya mamlaka yako.
Tujaribu kuweka kila kitu kwenye mizani kabla hatujakurupuka kutoa hukumu.


Sawa kakutwa na hatia nini kimefuata baada ya huyo mkurugenzi kuachishwa kazi hadharani? Makonda na magufuli wameshalihukumu kuwa yule jamaa ana hatia je kuna haja ya kumpeleka mahakamani? Je hasara ya kulitia taifa inarud vp? Kwa nini kuna ukimya hadi leo katika hilo suala ikiwa maamuz yake yalikuwa hadharani?
 
Nami pia hili neno "Tumbua" na "Jipu" sipendi kulitumia maana linatumika kidhalilisha! Pia hayo ya Ulimwengu nilishayatoa humu mapema kabisa nikimtahadharisha rais kutokuhutubia kwenye hadhara za kitaifa au kimataifa kutokana na hisia kali anazozijenga kwenye akili yake hasa pale anapoongelea wabaya! Hapa anaweza kusema jambo lolote ambalo ni hatari sana kwa taifa na usalama wake!
 
Sawa kakutwa na hatia nini kimefuata baada ya huyo mkurugenzi kuachishwa kazi hadharani? Makonda na magufuli wameshalihukumu kuwa yule jamaa ana hatia je kuna haja ya kumpeleka mahakamani? Je hasara ya kulitia taifa inarud vp? Kwa nini kuna ukimya hadi leo katika hilo suala ikiwa maamuz yake yalikuwa hadharani?
Ulimsikiliza vizuri rais siku ile?, yeye alimsimamisha kazi akagiza vyombo vinavyohusika vifanye kazi yake, kama itagundulika kuwa mkurugenzi hana hatia basi serikali itakuwa imeshindwa kesi.
Mkuu wa mkoa aliunda tume iliyofanya kazi na kugundua madudu, unataka watu wa aina hii waendelee kuwaumiza wananchi wengi?.
Kumbuka kuwa kila wizi unaofanywa na mkurugenzi au mkuu fulani wa idara, inapunguza kitu fulani ambacho kingeweza kuisaidia nchi kwa ujumla wake. Isiwe tu ni kutaka kwenda kinyume na kile kinachofanywa na serikali, weka mizani sahihi kwenye utoaji wa maoni yako.
 
Amejua hiyo mikutano wanao hudhuria ni makabwela wenye hasira za maisha, wenye wivu na walio fanikwa ndio na yeye anawatumia hawa kuwaonesha wengine yeye ni masiha , kumzuia ni ngumu.
Wengi wamefanikiwa kwa kuiba ela za miradi ya maendeleo....hicho ndicho kinachowakera Watanzania waliowengi. Zisingeporwa ela hizo watanzania hawa wasingekuwa katika hali huyo. ..........!
 
Nakiri mimi namkubali JPM lakini anachosema Ulimwengu ni kweli na haki kabisa.

Rais afanye kazi zaidi kwenye background lakini matokeo yake tutayaona tu. Ilikuwa staili ya Kambarage. Alikuwa akiwaondoa watu kimya kimya lakini siku zote ujumbe kwa wengine ulifika. JPM can do the same. Watumbuliwe lakini utu wao ubaki na wahukumiwe kwa makosa mahakamani sio kwenye mikutano ya hadhara.
 
Ulimsikiliza vizuri rais siku ile?, yeye alimsimamisha kazi akagiza vyombo vinavyohusika vifanye kazi yake, kama itagundulika kuwa mkurugenzi hana hatia basi serikali itakuwa imeshindwa kesi.
Mkuu wa mkoa aliunda tume iliyofanya kazi na kugundua madudu, unataka watu wa aina hii waendelee kuwaumiza wananchi wengi?.
Kumbuka kuwa kila wizi unaofanywa na mkurugenzi au mkuu fulani wa idara, inapunguza kitu fulani ambacho kingeweza kuisaidia nchi kwa ujumla wake. Isiwe tu ni kutaka kwenda kinyume na kile kinachofanywa na serikali, weka mizani sahihi kwenye utoaji wa maoni yako.


Kwa maelezo haya lazima ukubali mkuu serikali ILIKURUPUKA kwa nini nasema serikali ilikurupuka rejea bandiko lako chombo kiliundwa kuchunguza hilo suala muda mrefu na wakajiridhisha yule jamaa kusimamishwa kazi hadharani. Rais kaagiza tena uchunguz ufanyike!!! Haya akikutwa hana hatia itakuwaje? Je hao waliopewa kuchunguza wakija na majibu tofaut itakuwaje? Kesi nyingi zinafelishwa na wanasiasa nakwambia ukweli huyu aliposimamishwa kazi ilifaa awe sehemu husika anajibu hiyo kesi sio uchunguz tena kama wapo makini na walichokifanya kumbe bado ngoma ipo kati kasimamishwa lakini hakuna mwenye uhakika kuwa huyu jamaa anahusika kazi ipo.
 
Pole ndugu, hujajua lilipo tatizo! ni kweli kuna tatizo hasa baina ya raia/wananchi kimtazamo na uwezo wa Magufuli! Endelea kufuatilia, Magufuli ni zaidi ya mwanasiasa, na mtazamo wa raia/wananchi wengi walizoea kuongozwa na wanasiasa na kubadilika kwa mind hizo itachukua muda.
Magumu anayokutana nayo Magufuli ni kwa kuwa hata watendaji wake bado wanasumbuliwa na minds wa wanasiasa uchwara wasiojali uhalisia wa wanayozungumza katika utendaji wake! Kazi kubwa iliyo mbele ya Magufuli ni kubadili minds za watendaji kwanza katika mwanzo huu wa uatawala wake!
 
Ulimsikiliza vizuri rais siku ile?, yeye alimsimamisha kazi akagiza vyombo vinavyohusika vifanye kazi yake, kama itagundulika kuwa mkurugenzi hana hatia basi serikali itakuwa imeshindwa kesi.
Mkuu wa mkoa aliunda tume iliyofanya kazi na kugundua madudu, unataka watu wa aina hii waendelee kuwaumiza wananchi wengi?.
Kumbuka kuwa kila wizi unaofanywa na mkurugenzi au mkuu fulani wa idara, inapunguza kitu fulani ambacho kingeweza kuisaidia nchi kwa ujumla wake. Isiwe tu ni kutaka kwenda kinyume na kile kinachofanywa na serikali, weka mizani sahihi kwenye utoaji wa maoni yako.
Sasa mkuu kama ndiyo hivyo, kulikua na umuhimu gani wa kuja Mh RC na kutoa mashitaka mbele ya Mh JPM tena mbele ya Halaiki? Pamoja na ukweli hana nia mbaya pale mtu anaposimamishwa kupisha uchunguz, ila Methodology haijatulia. Hata Mungu Muumba anajua sisi sote ni wakosaji, lakini anastahi wakosaji. Kwa makosa tuliyo nayo binadam, kama Mungu angeamua kuhumu instantly, wengi tungeunguzwa hapahapa duniani. Lakini kuna siku na mahali maalum pa hukumu!
 
Aangalie asitupeleke kule kwenye Cultural revolution ya enzi ya Mao tse Dong wa China miaka ile ya 1966.
 
Back
Top Bottom