Jee Kunaukweli Wowote Kuwa, Ukiweka Nadhiri Mbele Ya Mungu, Usipoitekeleza, Unaparaganyikiwa?!

Jee Kunaukweli Wowote Kuwa, Ukiweka Nadhiri Mbele Ya Mungu, Usipoitekeleza, Unaparaganyikiwa?!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,103
Reaction score
128,722
Wanabodi,
Hakuna ubishi kuwa kitu chenye nguvu kuliko kitu chochote kwenye mwili wa binaadamu, ni "will power!" yaani nguvu ya nia!.
Ukiweka nia kimoyo moyo kuwa utafanya jambo fulani bila kutamka kwa kauli, hapo itaitwa umenuizia, ila Ukiweka nia kimoyo moyo kisha ukaitamka, tamko hilo linaitwa nadhiri!. Ni lazima ulitekeleze vinginevyo!, you'll have to pay tena hapa hapa duniani!.

Nimesema hivyo kufuatia ukweli kuwa kauli huumba!. Mungu, ameuumba ulimwengu na vyote vilivyomo kwa kauli tuu, alipotamka, na liwe giza, na uwe mwanga, na uwe nchi na yawe mali, etc, na vyote vikawa!. Baada Mungu kuumba kila kitu, akasema na tumuumbe mtu kwa mfano wetu, akafinyanga udongo akamuumba binaadamu na kumpulizia pumzi ya uzima yenye uwezo wa Mungu na kumpa jina la Adam. Hivyo sisi binaadamu tuna uwezo wa Mungu wa uumbaji kupitia kauli, hivyo nasema pasi shaka, maneno au kauli huumba!, hivyo natoa wito tuwe makini sana na kauli zetu tunazotoa na kuwa makini zaidi na nadhiri!.

Miongoni mwa nadhiri za hatari kabisa ni zile nadhiri zinazotolewa mbele ya Mungu , kikiwepo kiapo cha ndoa, au zile nadhiri zinazotolewa mbele ya Mungu kwa mtu kwa kutoa nadhiri kuwa atamtumikia Mungu katika useja, lakini kwa sababu zozote zile akaenda kinyume cha nadhiri yake, inasemekana, kile kiapo na nadhiri ile itamuwinda siku zote za maisha yake, kwa maisha yake kuparaganyika na kwamba s/he will never settle!.

Swali ni Jee kuna ukweli wowote katika hoja hii?. Naomba hebu fuatilia maisha ya watu waliokiuka viapo vya ndoa zao, reflect maisha yao, hali kadhalika fanya reflection ya maisha ya wengine wowote waliokiuka nadhiri zao mbele ya Mungu, maisha yao yakoje ?!. Jee ni kweli yameparaganyika?!. Jee ni kweli maneno huumba?!.

Nawatakieni Jumamosi Njema!.
Wasalaam
Pasco.
 
Wanabodi,
Hakuna ubishi kuwa kitu chenye nguvu kuliko kitu chochote kwenye mwili wa binaadamu, ni "will power!" yaani nguvu ya nia!.
Ukiweka nia kimoyo moyo kuwa utafanya jambo fulani bila kutamka kwa kauli, hapo itaitwa umenuizia, ila Ukiweka nia kimoyo moyo kisha ukaitamka, tamko hilo linaitwa nadhiri!. Ni lazima ulitekeleze vinginevyo!, you'll have to pay tena hapa hapa duniani!.

Nimesema hivyo kufuatia ukweli kuwa kauli huumba!. Mungu, ameuumba ulimwengu na vyote vilivyomo kwa kauli tuu, alipotamka, na like Gaza, na uwe mwanga, na uwe nchi na yawe Mali, etc, na vyote vikawa!. Baada Mungu kuumba kila kitu, akasema na tumuumbe mtu kwa mfano wetu, akafinyanga udongo akamuumba binaadamu na kumpulizia pumzi ya uzima yenye uwezo wa Mungu na kumpa jina la Adam. Hivyo sisi binaadamu tuna uwezo wa Mungu wa uumbaji kupitia kauli, hivyo nasema pasi shaka, maneno au kauli huumba!, hivyo natoa wito tuwe makini sana na kauli zetu tunazotoa na kuwa makini zaidi na nadhiri!.

Miongoni mwa nadhiri za hatari kabisa ni zile nadhiri zinazotolewa mbele ya Mungu , kikiwepo kiapo cha ndoa, au zile nadhiri zinazotolewa mbele ya Mungu kwa mtu kwa kutoa nadhiri kuwa atamtumikia Mungu katika useja, lakini kwa sababu zozote zile akaenda kinyume cha nadhiri yake, inasemekana, kile kiapo na nadhiri ile itamuwinda siku zote za maisha yake, kwa maisha yake kuparaganyika na kwamba s/he will never settle!.

Swali ni Jee kuna ukweli wowote katika hoja hii?. Naomba hebu fuatilia maisha ya watu waliokiuka viapo vya ndoa zao, reflect maisha yao, hali kadhalika fanya reflection ya maisha ya wengine wowote waliokiuka nadhiri zao mbele ya Mungu, maisha yao yakoje ?!. Jee ni kweli yameparaganyika?!. Jee ni kweli maneno huumba?!.

Nawatakieni Jumamosi Njema!.
Wasalaam
Pasco.

Mkuu PASCO jambo hili ni kweli kabisa , ukiweka nadhiri mbele ya mwenyezi mungu ni sharti uitimize, Mungu mwenyezi hadhiakiwi. Kwa yanayompata aliyewahi kuwa KATIBU MKUU WA BARAZALA MAASKOFU KATOLIKI ( TEC) na pia PADRI katika jimbo la Mbulu ni mfano hai wa jambo hili.

Huyu bwana pamoja kukiuka nadhiri yake pia ameikiuka mara mbili mfululizo kwa wanawake wawili tofauti. kwa mujibu wa sheria za roma na mitaguso ya kanisa , huyu bwana kwake yafutayo yanamuhusu;
"ROMA LOCUTA CAUSA FINITA"
wanaomfuata ni misukule tu.
 
Pasco, nakushauri rejea kwenye Jukwaa la Siasa; mada hii uliyoileta haijadiliki kwa mantiki bali kwa imani. Bila shaka unafahamu mauzauza yanayoandamana na masuala ya imani.
 
Mkuu PASCO jambo hili ni kweli kabisa , ukiweka nadhiri mbele ya mwenyezi mungu ni sharti uitimize, Mungu mwenyezi hadhiakiwi. Kwa yanayompata aliyewahi kuwa KATIBU MKUU WA BARAZALA MAASKOFU KATOLIKI ( TEC) na pia PADRI katika jimbo la Mbulu ni mfano hai wa jambo hili.

Huyu bwana pamoja kukiuka nadhiri yake pia ameikiuka mara mbili mfululizo kwa wanawake wawili tofauti. kwa mujibu wa sheria za roma na mitaguso ya kanisa , huyu bwana kwake yafutayo yanamuhusu;
"ROMA LOCUTA CAUSA FINITA"
wanaomfuata ni misukule tu.
Mkuu Ph.D, nakuomba ondoa hilo jina na naomba sana tuepuke kutaja taja majina ya watu na haswa kwa kuzingatia mwelekeo wa wengi ndani ya hii jf yetu!.
Pasco
 
Topic nzuri lakini as long as Dr Slaa atatajwa humu
naona uwezekano wa kuharibu thread upo mkubwa
Mkuu The Boss, kila unapohisi jambo ambalo sii jema, ukilitaja tuu, unakuwa umelizuia lisitoke!. Kitendo tuu cha kuweka angalizo lako kwenye mada hii, ndio imekuwa caveat, watu wasichangie kabisa!. Hiyo ni manifestation of powers kwenye kufanya priemptive strike hivyo jambo baya haliwezi kutokea tena, unakuwa umelizuia!.

Kabla ya kikao chao, nitapandisha uzi humu jf nikisema "Leo, ...lazima watamfuta uanachama ...kwa sababu ndivyo walivyokuwa wamepanga tangu zamani!", hivyo wale wafutaji wanaweza kuchange mind!.

Kama topic ni nzuri, toa tuu maoni yako bila kutaja majina ya watu.
Pasco
 
Pasco, nakushauri rejea kwenye Jukwaa la Siasa; mada hii uliyoileta haijadiliki kwa mantiki bali kwa imani. Bila shaka unafahamu mauzauza yanayoandamana na masuala ya imani.
Mkuu Drifter, nimeupokea ushauri wako, naufanyia kazi, na ikitokea miongoni mwao wakawa ni wanasiasa, huu uzi niupandishie kule Jukwaa la Siasa?!.
Pasco
 
phad uko sawa hata maswahibu anayoyapata doctor slaa kisiasa na kifamilia ni kwenda kinyume na nadhiri ya mungu na atapata tabu sana siku za usoni
 
Mi namuogopa sana MUNGU,ndo maana niliwatukana watu hapa waliokuwa wameanza discussion eti hakuna MUNGU,kwa kweli niliumia sana roho nikaona kutoa hasira ni bora kuwatukana tu,matokeo yake waka ni ban wiki nzima,nikawa sina access na JF,ndugu zangu MUNGU yupo,mambo aliyonitendea MUNGU ktk maisha yangu ni mazito na ya kusisimua,hivi sasa nalipwa 2.5 milioni kwa mwezi,ktk kampuni moja kubwa ya kimataifa,sina elimu,kifupi anayetaka kumjua MUNGU wangu anipe request,aone maajabu ya karne! nina mengi mazito ya kueleza.
 
yap ni kweli mkuu nadhiri na viapo mara nyingi huumba kitu katika mtiririko wa maisha thatwhy hata mtoto unapomuahidi kitu kipindi angali mdogo hujitokeza matatizo ukubwani inasemekana kuna malaika wanaoshinikiza kutekeleza lengo ulilolishirikisha katika roho
 
Mkuu Pascol, hili jambo linaukweli ndani yake! Mimi ninavyojua ukiwaza jambo fulani, ukaliruhusu kukaa katika roho/nafsi badaye ukawa unapendelea kulitamka aidha kwa kuwambia watu wako wa karibu i.e marafiki, familia n.k, basi jambo hilo hutokea kama lilivyo aidha liwe zuri au baya! Kwa mfano; umechoka kuishi maisha ya kimasiki na unataka kuishi maisha ya utajiri inawezekana! Just speak what you want to achieve into your life and the dream 'll come true. Ndiyo maana nikasema 'Nothing happens until you speak' angalia hapo chini!!

Mshua
 
Ukiweka nia kimoyo moyo kuwa utafanya jambo fulani bila kutamka kwa kauli, hapo itaitwa umenuizia, ila Ukiweka nia kimoyo moyo kisha ukaitamka, tamko hilo linaitwa nadhiri!. Ni lazima ulitekeleze vinginevyo!, you'll have to pay tena hapa hapa duniani!.
Hivi hata ile ya kumuahidi mtu nayo ni nadhiri?
 
Wanaotoa na kuweka nadhiri wengi hawana elimu au ufaham wa nadhiri unakuta umelala ndani unatizama sealing board unaanza kuongea na roho yako mwishowe unapiga magoti kuweka laana usiyoijua.

Wakati mwingine umasikini na ukosefu wa elimu ya ziada vinatufanya waafrika baadhi kuharibu mfumo wetu wa maisha yetu kwa kutoelewa.
 
Back
Top Bottom