Je, wewe ni malkia wa nguvu?

Innocent Kirumbuyo

JF-Expert Member
Jan 1, 2014
4,640
4,426
Uzuri huvutia wanaume, ila busara pekee ndio itakufanya udumu katika mahusiano. Ushawishi unaweza ukadaka utulivu wa mwanaume ila akili yako kubwa inaweza ikafanikiwa kumshawishi.

Malalamiko, ubishi na kelele vinamuudhi kila mwanaume, ila utulivu na unyenyekevu unamfanya mwanaume awe mpole kwako.

Ubaya wowote wa mwanaume hutokea kwa sababu fulani na uwezo wa kukabiliana na huo ubaya upo katika busara za mwanamke wake.

Kutambua maumivu ya mwanamke ni rahisi, kwa sababu hawezi kukaa nayo moyoni ni wazi atamueleza yule anaemuamini. Ila wanaume maumivu yao ni ya ndani kwa ndani na kuweza kuyang'amua inahitaji mwanamke aliye na busara ya kiungu.

Mwisho wa siku maneno yatokayo kinywani mwako ndio ya msingi zaidi kuliko uzuri wako. Hivyo basi wekeza katika maneno yaliyo jaa busara na hekima.

Mtii mwanaume na mpe heshima yake nae atakufanya uwe msaidizi wa kila kitu anachokifanya. Jifunze kutengeneza 'mood' ya mwanaume wako na utafanikiwa kuushinda moyo wake.

Mwanaume yupo tayari akushirikishe mambo yake yote kama ataona 'maturity' kubwa uliyonayo. Ni vema kama mawazo yako ni ya kawaida (mediocrity) ukajiongeza na kuleta mawazo yenye tija ili aweze kukuamini.

Wanawake wapo kila mahala tena ni wengi kuliko wanaume ila Malikia wa nguvu ni wachache mno. Jitengeneze kuwa malikia wa nguvu, ili mfalme wa nguvu aje katika maisha yako.

Mwanamke atajenga nyumba yake kwa kinywa chake kilichojaa maneno ya busara.

Busara yangu: For a man wins nothing better than a good wife, and then again nothing deadlier than a bad one!!
 
Back
Top Bottom