Mchokoo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2015
- 1,188
- 1,604
Hivi yawezekana hii ikawa ni hulka ya ya watu wa taifa hili?
Kwamba, watanzania hawakuchukua silaha kukabiliana na watawala wa kikoloni katika kudai uhuru wao, bali waliipigania haki yao kimyakimya bila sauti ya mtutu kusikika.
Hata Mzee Mandela alipomjulisha Mwalimu juu ya azma ya ANC kuchukua silaha dhidi makaburu, bado mzee wetu hakuukubali mpango huo!
Sasa ninapouona uchache wa kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura; najiuliza, je, huku ndiko kudai haki hii nayo kimyakimya?
Haki ya uhuru wa kujiamulia mambo. Uhuru wa kuchaguana, kuchagua, na kuchaguliwa.
Eti labda ndiyo imesababisha watu wengi wameacha kwenda kujiandikisha kama wanavyosema baadhi ya wadau.
Kama si sababu nyingine iliyopelekea; sasa yawezekana wabongo wakayafundisha mataifa mengine kwamba; kudai chako sio lazima ufanye magomvi?
Wadau hili mnalionaje?
Kwamba, watanzania hawakuchukua silaha kukabiliana na watawala wa kikoloni katika kudai uhuru wao, bali waliipigania haki yao kimyakimya bila sauti ya mtutu kusikika.
Hata Mzee Mandela alipomjulisha Mwalimu juu ya azma ya ANC kuchukua silaha dhidi makaburu, bado mzee wetu hakuukubali mpango huo!
Sasa ninapouona uchache wa kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura; najiuliza, je, huku ndiko kudai haki hii nayo kimyakimya?
Haki ya uhuru wa kujiamulia mambo. Uhuru wa kuchaguana, kuchagua, na kuchaguliwa.
Eti labda ndiyo imesababisha watu wengi wameacha kwenda kujiandikisha kama wanavyosema baadhi ya wadau.
Kama si sababu nyingine iliyopelekea; sasa yawezekana wabongo wakayafundisha mataifa mengine kwamba; kudai chako sio lazima ufanye magomvi?
Wadau hili mnalionaje?