Kwamba hapo mwanzo, binadamu waliamua kujenga jengo kubwa na refu katika mji ule na kilele chake ni kifike mbinguni uko anakopatikana Mungu.
Kwamba Mpango huu haukumpendeza Mungu aliyewachanganyia lugha watu hao, wakashindwa kuelewana na baadae walilazimika kuachana na mradi huo.
Nawasilisha🙏
Ona mwamba: hadithi hii sio ya kuichukulia literally bali figuratively.
Hadithi hii katika uhalisia huu hapa: Kwamba wakati ambapo watu (a group of people) wanaongea lugha moja kwa maana ya wakisema ndiyo, wanakuwa wamemaanisha ndiyo na wanaeleweka kwa watu wamesema hiyohiyo ndiyo. Basi hakuna cha kuwazuia kufikia nia yao iwe njema au ovu
...... ntaendelea nna majukumu kidogo
haiya, sasa nnaendelea....;
So tuanze na ngazi mtu binafsi ikiwa nafsi yake mwili wake na roho yake vikiishi kwa kukubaliana (lugha moja) basi hakuna cha kuwazuia kufikia lengo na watasimama kama mmoja. Wakianza ile nafsi inataka smoothie mwili unapokea unasema 'anataka sodaa' hapohapo na roho inatamani kufunga huyu mtu hatasimama.
Tukija ngazi ya mahusiano, mme anataka nazungumzo, halafu mke anatafsiri 'mme anataka mabishano' na kama kuna watoto wakasoma 'wazazi wanagombana!!!' Basi jua hapo hiyo family ni majanga. Inatakiwa baba akisema leo tuna kikao basi kila mwanafamilia asikie na aelewe kinakuja kikao cha familia kujadili mustakabali wa maisha yetu memaa.
Hii unaweza kuendelea hata kitaifa, Inatakiwa CCM akisema 'tunajenga muundombinu huu x' kila mtu asikie na aelewe na atende kwa ukweli huo. Sio mwingine CHADEMA labda aanze kutafsiri wamesema 'tunaandaa mfumo wa upigaji kupitia geresha ya mradi x'. Watu wa usalama wa taifa mtanisaidia kazi ya propaganda katika kuliinua Taifa. Ni lazima watu wasikie na waelewe kitu tulichonia mamoja (mfano VIWONDER ovaa)
Kataeni msikatae hata enzi ya JPM suala lililotuweka pamoja sana lilikuwa pia ni suala la 'lugha moja' aliyoiwezesha Jpm mwenyewe, mwambaa💪🏿.
Na mwisho kidunia...... Inatakiwa marekani akisema 'tunachanja na kusambaza chanjo ili kuzuia korona' basi kila mtu asikie na elewe hivyo sio nchi nyingine isikie ujumbe kwa herufi kubwa kwamba marekani anasema 'TUNAWADUNGA SINDANO ZA KUWAFANYA MAZOMBI😁🙄' I mean how did everything get so twisted🤔.
Ndio sababu hatuendelei kufikia 'full potential yetu' - hatujafanikiwa kuzungumza 'lugha moja' kuwa katika ukurasa mmoja kunia mamoja, kusema mamoja, na kutenda mamoja. Sio kitu kimoja, a aah. MAMOJA.