Uongozi wa simba umekubali kuwa driven na presha na papara ya mashabiki ili kushindana na Yanga..
Kwa maana nyingine Tatizo la Simba ni kuimarika kwa Yanga......
Simba wana-force kujiringanisha na Yanga ili kuwaridhisha mashabiki wake kwa njia za mkato..
Viongozi wamejikuta wanafanya maamuzi bila utulivu, fukuza huyu lete yule, ondoa hawa, ingiza wapya.....nk
Wamejikuta wanaanza upya kila msimu....ili ku-cope na mizaha, vicheko, tambo za watani wao dhidi ya mashabiki wao....
Kiuhalisia, Simba inafanya vizuri...
Simba hii imetoka kucheza fainali kombe la shirikisho.... ....Simba ilikuwa haijafikia hatua hii tangu miaka 23 iliyopita? Leo utasema Simba ni mbovu?
Hayo yalikuwa ni mafanikio, lakini inawezekana wasiyanekane simply kwasab Wamefungwa na yanga kila mara nyingine...
Viongozi wa Simba wanatakiwa watengeneze timu kwa utulivu, bila kubabaishwa na kelele za mashabiki wachache wanaolalama mitandaoni..
Hawa ni wachache sana achaneni nao...hawafiki hata mia.