ladyfurahia
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 14,758
- 9,592
Habarini wanajamvi wenzangu ya leo tena ni kali kwani nimeingia kiditali kabisa kuwaasa na kuwaonya wale WANANDOA NA WASIO WANANDOA humu jamvini na kwingineko kule.
Nina jambo nataka tulikumbuke au tulijue hususani kwa wanandoa waliotimiza ahadi zote za ndoa, . Nataka kusema leo lile swala letu la KIAPO CHA NDOA pale mlipofunga pingu za maisha hususani yale maneno yanayosemwa na viongozi wa dini au serikali katika boma. Je kwenu wanandoa mnayazingatia yale maneno ya kiapo au mnakuwa tu pale kama pambo tu na mnakumbuka maneno ambayo mliambiana siku hiyo ya fungate, iweje sasa NDOA nyingi zimekuwa na mgogoro ndani yao na iweje mnarushiana vijembe ndani ya ndoa na wakati mlisema maneno yenye mvuto na upendo kati yenu. Au mmesahau kuwa nyie ni kiungo kimoja ambacho siku hiyo Mungu aliwaunganisha mkawa mwili mmoja. Sasa je hayo maneno ya kashfa, dharau, majivuno na kutupiana lawama yametoka wapi tena? na wakati mlisema nyie kuwa mtakuwa pamoja katika raha na shida zote za maisha yenu. KUMBUKA yale maneno ya kiapo ambacho ulimwapia mwenzako kuwa utakuwa naye katika shida na raha, utampenda na kumtunza, kumjali, utakuwa mtiifu kwake, utamheshimu mpaka kifo kiwatenganishe, sasa je kwanini mmebadilika na kuwa watu wasiopendana kama awali?.
HEBU SOMA HAPA NA UJITAMBUE ULIKUWAJE KABLA YA NDOA YAKO:
MUME: Nilitamani sana muda huu ufike.
MKE: Vipi wataka niondoke?
MUME: Hapana hata kidogo,
MKE: Unanipenda?
MUME: Ndio maanake.
MKE: Utaniletea demu (mwanamke) mwingine ndani?
MUME: Siwezi huo upuuzi.
MKE: Utanibusu milele?
MUME: Kila mara!
MKE: Je utanipiga?
MUME: Aaaa! haiwezi tokea.
MKE; Naweza kukuamini?
MUME: Ndio.
MKE; Aaaah! Mpenzi!
Ukitaka kujua BAADA YA NDOA inakuwaje hebu soma kuanzia chini ya hayo maneno ukienda (kuelekea) juu ndipo utagundua kuwa NDOA nyingi za sasa zina dosari na migogoro haiishi kamwe pasipo mtanguliza Mungu ambaye ndiye mwanizilishi wa NDOA. Ni vyema wanandoa na wasiona ndoa mkajifunza hii na kufuata vile Mungu anavyotaka.
Nina jambo nataka tulikumbuke au tulijue hususani kwa wanandoa waliotimiza ahadi zote za ndoa, . Nataka kusema leo lile swala letu la KIAPO CHA NDOA pale mlipofunga pingu za maisha hususani yale maneno yanayosemwa na viongozi wa dini au serikali katika boma. Je kwenu wanandoa mnayazingatia yale maneno ya kiapo au mnakuwa tu pale kama pambo tu na mnakumbuka maneno ambayo mliambiana siku hiyo ya fungate, iweje sasa NDOA nyingi zimekuwa na mgogoro ndani yao na iweje mnarushiana vijembe ndani ya ndoa na wakati mlisema maneno yenye mvuto na upendo kati yenu. Au mmesahau kuwa nyie ni kiungo kimoja ambacho siku hiyo Mungu aliwaunganisha mkawa mwili mmoja. Sasa je hayo maneno ya kashfa, dharau, majivuno na kutupiana lawama yametoka wapi tena? na wakati mlisema nyie kuwa mtakuwa pamoja katika raha na shida zote za maisha yenu. KUMBUKA yale maneno ya kiapo ambacho ulimwapia mwenzako kuwa utakuwa naye katika shida na raha, utampenda na kumtunza, kumjali, utakuwa mtiifu kwake, utamheshimu mpaka kifo kiwatenganishe, sasa je kwanini mmebadilika na kuwa watu wasiopendana kama awali?.
HEBU SOMA HAPA NA UJITAMBUE ULIKUWAJE KABLA YA NDOA YAKO:
MUME: Nilitamani sana muda huu ufike.
MKE: Vipi wataka niondoke?
MUME: Hapana hata kidogo,
MKE: Unanipenda?
MUME: Ndio maanake.
MKE: Utaniletea demu (mwanamke) mwingine ndani?
MUME: Siwezi huo upuuzi.
MKE: Utanibusu milele?
MUME: Kila mara!
MKE: Je utanipiga?
MUME: Aaaa! haiwezi tokea.
MKE; Naweza kukuamini?
MUME: Ndio.
MKE; Aaaah! Mpenzi!
Ukitaka kujua BAADA YA NDOA inakuwaje hebu soma kuanzia chini ya hayo maneno ukienda (kuelekea) juu ndipo utagundua kuwa NDOA nyingi za sasa zina dosari na migogoro haiishi kamwe pasipo mtanguliza Mungu ambaye ndiye mwanizilishi wa NDOA. Ni vyema wanandoa na wasiona ndoa mkajifunza hii na kufuata vile Mungu anavyotaka.