Je, ulizini au ulilala na mkeo?

Je, ulizini au ulilala na mkeo?

MKETO THE DON

New Member
Joined
Jan 22, 2015
Posts
3
Reaction score
1
Nisaidie hili,

Mfano Wewe ni mkazi wa Tabora ila unafanya kazi Mwanza ukawambia nyumbani wakuolee Mke wakakuolea wakati unakuja kukutana na Mke wako

Ulipofika stend Tabora kabla hujafika nyumbani ukakutana na msichana mzuri ukashawishika. Ukamtongoza mkaenda guest na mkafanya mapenzi, ulipoenda nyumbani ili ukutane na mkeo ukaambiwa amefata nyanya sokoni aliporudi yule msichana kumbe ndio Mke mwenyewe! Uliyekuwa naye gest.

Je, ulizini au ulilala na Mkeo? Na wewe utamchukuliaje mke Huyo? Na yeye atakuonaje mume? Nani malaya? Kati yenu?

Maoni tiririka kwa SMS au mstue mdau mwingine tuone majibu.
 
Kuna mwingine kule kasema kaona miezi miwili,mwingine tena kasema anamkeshea TL.Wewe nae eti umefungiwa ndoa!
Siku ya leo ndefu!
 
Hii riwaya tuipe jina gani?










Let's meet at the top, cheers 🥂
 
Maskani ukileta story kama hii kamwe hutopata hata nafasi ya kukaa hata kwenye benchi.

Mambo haya ya Paukwa Pakawa waachie watoto wa chekechea au Cage 1.
 
Back
Top Bottom