Je roho ya binadamu ni Mungu ndani ya akili yake Yenyewe?

Je roho ya binadamu ni Mungu ndani ya akili yake Yenyewe?

Nombo de classic

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2016
Posts
286
Reaction score
380
Wanabodi hii mada ni tata sana, kabla hujaisoma inabidi uweke hisia na mafundisho ya dogma pembeni.
Albert Pike kwenye kitabu chake cha "Moral and dogma of freemasonry and accepted Scottish right" analijadili kuhusu Daumonios
(δαιμονιος) Pike ananakili moja kwa moja kutoka kwenye dhana ya kale ya Kigiriki ya daimon (δαίμων) — si “pepo au shetani” kwa maana ya Kikristo ya baadaye, bali kiumbe wa kati kati ya binadamu na uungu, au roho ya kiungu inayomwongoza mtu.

Katika muktadha huu, daimonios (δαιμόνιος) ni kivumishi kinachomaanisha:
cha kiungu,
chenye msukumo wa kimungu,
chenye asili ya daimon,
kinachohusiana na nguvu ya juu ya kiroho.

Roho ya mwanadamu ni ya kiungu kwa asili, ni kipande cha Roho ya Ulimwengu Mzima (ambayo Pike anaifananisha na Dionysos).
Uungu huu wa ndani humwezesha mwanadamu kufikia hali ya kishujaa au ya kutokufa kupitia maadili, tafakari ya ukweli, na kuingizwa katika mafumbo ya kiroho.
Hii inaendana na wazo la Socrates kwamba kila mtu ana daimonion yake binafsi — sauti ya ndani ya dhamiri na mwongozo wa kiroho.
Pike anaunganisha hili na mitholojia ya Dionysos kama Mkombozi: kama Dionysos anavyoiweka huru roho kutoka kifungo cha mambo ya Dunia, ndivyo hali ya daimonios ya roho inavyoifanya iweze kukombolewa na kufanywa ya kimungu.
Hivyo basi, daimonios hapa si jina la mtu (kama kuhani wa Galatia aliyatajwa awali), bali ni sifa ya kiroho ya roho ya mwanadamu — cheche ya uungu iliyo ndani yake.

Hapo zamani za Wagiriki wa kale, neno Daumonios (δαιμόνιος) lilikuwa jina zuri kabisa. Lilimaanisha "cheche za kimungu," "cheche takatifu ndani ya mtu." Wanafalsafa kama Socrates walisema kila mtu ana daimonion ndani yake – sauti ya ndani ya hekima na uongofu inayotoa mwongozo wa maadili. Daumonios haikuwa kitu cha kuogopa; ilikuwa cheche ya Mungu ndani ya roho ya mwanadamu, ishara kwamba binadamu na Mungu wana uhusiano wa karibu.

Wakati Ukristo ulipoenea katika Dola la Warumi, walikutana na imani nyingi sana ambazo waliziona ni zakishetani na sanamu. Sasa Ili kuthibitisha kuwa "Mungu mmoja" wa Kikristo ndiye pekee, ilibidi dini hii mpyo "ilinde" waumini wake kwa kuyakataa mafundisho yote ya kale. Njia moja ilikuwa kupitia lugha. Maneno yaliyokuwa matakatifu kwa wenyeji yalibadilishwa maana.

Daumonios aliyekuwa roho mwema wa kigiriki, akawa shetani wa Kikristo. Yaani kwa lugha ya Sasa wanaita Demon
Miungu yote ya kale na roho zote za makabila ikapewa jina moja: mapepo.
Hili lilikuwa na lengo kubwa: kufanya mtu asitegemee mwongozo wa ndani (daimonion yake), bali ategemee mwanzo wa nje – yaani kanisa, maaskofu, na sakramenti. Ikiwa roho zote za kale ni shetani, basi hakuna mwongozo halali upatikanao nje ya mfumo mpya wa Kikristo.

Wakristo walianzisha fundisho la "Dhambi ya Asili" (Original Sin). Lilisema: Adamu alimwasi Mungu, na dhambi hiyo imerithiwa kwa binadamu wote. Kwa hiyo, kizazi chote kimezaliwa kwenye hali ya dhambi. Mwanadamu kwa asili yake ni mhitaji, mwombaji, mwenye dosari. Lengo la maisha yako ni kuomba msamaha na kukubali neema ya Mungu kupitia Yesu.
Lakini kuna hadithi nyengine, ya siri zaidi, ya "Uungu wa Kurithi" (Inherited Divinity). Hii ndiyo hadithi ya Daumonios asili. Inasema: Kama Mungu aliumba mwanadamu kwa mfano wake, basi kiini cha mwanadamu ni cha kimungu. Mwanadamu huzaliwa na cheche ya Mungu ndani yake. Lengo la maisha si kuomba msamaha kwa kuwa tumekosa, bali kukumbuka na kutimiza ule uungu ulio tayari ndani yatu kwa kufanya mema, kutafuta hekima, na kujitoa kwa upendo. Binadamu si mhitaji, bali ni mrithi.

Kwa Nini Dini Za Kisasa Ukristo, Uislamu n.k Zinapingana na Uungu wa Kurithi?
Kwa mtazamo wa kisasa, dini nyingi zimejenga utawala wake juu ya mawazo mawili:

1. Uhitaji wa Mwanadamu: Ikiwa wewe ni mwenye dhambi na unahitaji, utamtafuta Mungu kupitia watawala wake duniani (kanisa, padre, sheikh, vitabu).
2. Uhakika na Udhibiti: Dhana ya dhambi ya kurithi inatoa jibu moja wazi la shida kubwa ya binadamu (kwa nini tunaumia, kufanya maovu?). Ikidai kuwa na jibu hilo, inakuza utegemezi.
Dhana ya Uungu wa Kurithi inavunja mfumo huu. Ikiwa kila mtu ana mungu ndani yake, basi:

Huhitaji mpatanishi wa nje kwa kiasi kikubwa.
Mwongozo wako mkuu unatoka kwenye sauti yako ya ndani na uzoefu wako binafsi, si kwenye maagizo yaliyoandikwa pekee.
Uwezo wako na hatia yako ni yako mwenyewe zaidi.
Kwa dini zilizo na utaratibu na utawala hili linaweza kuonekana kama tishio? Linapunguza umuhimu wa taasisi na wakuu, na kuwaweka watu huru zaidi kijamii na kiroho.
 
Ndugu ukitaka kufa masikini na mnyonge, basi haya mambo yawe kipaombele katika maisha yako.
 
Nawakaribisha makafiri wote mje mtoe neno nyinyi ndo mnaelimu sana kuliko sisi kobaz

Naona kafir mkuu ELI COHEN kafika tayar bado shost zake
KAFIR NI BABA AKO ANAEGONOKEA WANAUME WENZAKE ILI AWALISHE WANAE, WEWE NAE UNAGONOKEA WANAUME WENZAKO ILI UISHI MJINI KAMA UONGO KWANINI UJIITE ANA NA KWANINI UFATE WANAUME INBOX😁

20260122_083543.jpg
 
Ndugu yangu unapozungumza kuhusu mambo yanayomuhusu Mwenyezi Mungu basi uwe makini. Usikurupuke tu. Chukua Quran soma au vitabu vengine vye Mwenyezi Mungu. Kamwe usianzishe mjadala wa Mwenyezi Mungu kwa mambo usiyo na ujuzi nayo au kwa mambo ya mzaha, unaweza ukajikuta unapata laana na majanga hivihivi

QURAN 22: 8-9
8. "Na katika watu wapo wanao bishana juu ya Mwenyezi Mungu bila ya elimu, wala uwongofu, wala Kitabu chenye nuru.
9. Anaye geuza shingo yake ili kupoteza watu waache Njia ya Mwenyezi Mungu. Duniani atapata hizaya, na Siku ya Kiyama tutamwonjesha adhabu ya kuungua. "
 
Ndugu yangu unapozungumza kuhusu mambo yanayomuhusu Mwenyezi Mungu basi uwe makini. Usikurupuke tu. Chukua Quran soma au vitabu vengine vye Mwenyezi Mungu. Kamwe usianzishe mjadala wa Mwenyezi Mungu kwa mambo usiyo na ujuzi nayo au kwa mambo ya mzaha, unaweza ukajikuta unapata laana na majanga hivihivi

QURAN 22: 8-9
8. "Na katika watu wapo wanao bishana juu ya Mwenyezi Mungu bila ya elimu, wala uwongofu, wala Kitabu chenye nuru.
9. Anaye geuza shingo yake ili kupoteza watu waache Njia ya Mwenyezi Mungu. Duniani atapata hizaya, na Siku ya Kiyama tutamwonjesha adhabu ya kuungua. "
Acha kuhubiri hofu hiyo ni mitetemo ya chini (low vibration) sisi binadamu kiasili ni sehemu ya Uungu.
 
Haya Mawazo yako yote ni kweli kabisa asilimia 100 kua tuna asili ya Mungu. Ila huu uwezo tuliupoteza baada ya kuingia dhambi ya asili kupitia Adamu. Kwaio wote tunazaliwa tukiwa tumeshaupoteza utukufu wetu wa Mwanzo, kwaio tunazaliwa sio kama warithi Bali watumwa wa dhambi, ndio maana tunaumwa, tunapata shida nyingi na tunakufa.

Kwaio kupitua Yesu Kristo, Mungu anataka kuturejesha kwenye nafasi yetu ya Mwanzo tulioipoteza ya kutoka kuwa watumwa na kua warithi. NDIO MAANA KUNA AHADI YA UZIMA WA MILELE. ambayo ndio asili yetu
 
Wanabodi hii mada ni tata sana, kabla hujaisoma inabidi uweke hisia na mafundisho ya dogma pembeni.
Albert Pike kwenye kitabu chake cha "Moral and dogma of freemasonry and accepted Scottish right" analijadili kuhusu Daumonios
(δαιμονιος) Pike ananakili moja kwa moja kutoka kwenye dhana ya kale ya Kigiriki ya daimon (δαίμων) — si “pepo au shetani” kwa maana ya Kikristo ya baadaye, bali kiumbe wa kati kati ya binadamu na uungu, au roho ya kiungu inayomwongoza mtu.

Katika muktadha huu, daimonios (δαιμόνιος) ni kivumishi kinachomaanisha:
cha kiungu,
chenye msukumo wa kimungu,
chenye asili ya daimon,
kinachohusiana na nguvu ya juu ya kiroho.

Roho ya mwanadamu ni ya kiungu kwa asili, ni kipande cha Roho ya Ulimwengu Mzima (ambayo Pike anaifananisha na Dionysos).
Uungu huu wa ndani humwezesha mwanadamu kufikia hali ya kishujaa au ya kutokufa kupitia maadili, tafakari ya ukweli, na kuingizwa katika mafumbo ya kiroho.
Hii inaendana na wazo la Socrates kwamba kila mtu ana daimonion yake binafsi — sauti ya ndani ya dhamiri na mwongozo wa kiroho.
Pike anaunganisha hili na mitholojia ya Dionysos kama Mkombozi: kama Dionysos anavyoiweka huru roho kutoka kifungo cha mambo ya Dunia, ndivyo hali ya daimonios ya roho inavyoifanya iweze kukombolewa na kufanywa ya kimungu.
Hivyo basi, daimonios hapa si jina la mtu (kama kuhani wa Galatia aliyatajwa awali), bali ni sifa ya kiroho ya roho ya mwanadamu — cheche ya uungu iliyo ndani yake.

Hapo zamani za Wagiriki wa kale, neno Daumonios (δαιμόνιος) lilikuwa jina zuri kabisa. Lilimaanisha "cheche za kimungu," "cheche takatifu ndani ya mtu." Wanafalsafa kama Socrates walisema kila mtu ana daimonion ndani yake – sauti ya ndani ya hekima na uongofu inayotoa mwongozo wa maadili. Daumonios haikuwa kitu cha kuogopa; ilikuwa cheche ya Mungu ndani ya roho ya mwanadamu, ishara kwamba binadamu na Mungu wana uhusiano wa karibu.

Wakati Ukristo ulipoenea katika Dola la Warumi, walikutana na imani nyingi sana ambazo waliziona ni zakishetani na sanamu. Sasa Ili kuthibitisha kuwa "Mungu mmoja" wa Kikristo ndiye pekee, ilibidi dini hii mpyo "ilinde" waumini wake kwa kuyakataa mafundisho yote ya kale. Njia moja ilikuwa kupitia lugha. Maneno yaliyokuwa matakatifu kwa wenyeji yalibadilishwa maana.

Daumonios aliyekuwa roho mwema wa kigiriki, akawa shetani wa Kikristo. Yaani kwa lugha ya Sasa wanaita Demon
Miungu yote ya kale na roho zote za makabila ikapewa jina moja: mapepo.
Hili lilikuwa na lengo kubwa: kufanya mtu asitegemee mwongozo wa ndani (daimonion yake), bali ategemee mwanzo wa nje – yaani kanisa, maaskofu, na sakramenti. Ikiwa roho zote za kale ni shetani, basi hakuna mwongozo halali upatikanao nje ya mfumo mpya wa Kikristo.

Wakristo walianzisha fundisho la "Dhambi ya Asili" (Original Sin). Lilisema: Adamu alimwasi Mungu, na dhambi hiyo imerithiwa kwa binadamu wote. Kwa hiyo, kizazi chote kimezaliwa kwenye hali ya dhambi. Mwanadamu kwa asili yake ni mhitaji, mwombaji, mwenye dosari. Lengo la maisha yako ni kuomba msamaha na kukubali neema ya Mungu kupitia Yesu.
Lakini kuna hadithi nyengine, ya siri zaidi, ya "Uungu wa Kurithi" (Inherited Divinity). Hii ndiyo hadithi ya Daumonios asili. Inasema: Kama Mungu aliumba mwanadamu kwa mfano wake, basi kiini cha mwanadamu ni cha kimungu. Mwanadamu huzaliwa na cheche ya Mungu ndani yake. Lengo la maisha si kuomba msamaha kwa kuwa tumekosa, bali kukumbuka na kutimiza ule uungu ulio tayari ndani yatu kwa kufanya mema, kutafuta hekima, na kujitoa kwa upendo. Binadamu si mhitaji, bali ni mrithi.

Kwa Nini Dini Za Kisasa Ukristo, Uislamu n.k Zinapingana na Uungu wa Kurithi?
Kwa mtazamo wa kisasa, dini nyingi zimejenga utawala wake juu ya mawazo mawili:

1. Uhitaji wa Mwanadamu: Ikiwa wewe ni mwenye dhambi na unahitaji, utamtafuta Mungu kupitia watawala wake duniani (kanisa, padre, sheikh, vitabu).
2. Uhakika na Udhibiti: Dhana ya dhambi ya kurithi inatoa jibu moja wazi la shida kubwa ya binadamu (kwa nini tunaumia, kufanya maovu?). Ikidai kuwa na jibu hilo, inakuza utegemezi.
Dhana ya Uungu wa Kurithi inavunja mfumo huu. Ikiwa kila mtu ana mungu ndani yake, basi:

Huhitaji mpatanishi wa nje kwa kiasi kikubwa.
Mwongozo wako mkuu unatoka kwenye sauti yako ya ndani na uzoefu wako binafsi, si kwenye maagizo yaliyoandikwa pekee.
Uwezo wako na hatia yako ni yako mwenyewe zaidi.
Kwa dini zilizo na utaratibu na utawala hili linaweza kuonekana kama tishio? Linapunguza umuhimu wa taasisi na wakuu, na kuwaweka watu huru zaidi kijamii na kiroho.
Sehemu ya neno ROHO weka neno NAFSI ...japo nafsi nayo ni ROHO NA KILA KITU NI ROHO
 
Watu kama wewe wenye fikra huru, wamebaki wachache sana....

Dunia imefungwa ndani ya mnyororo ya dini, kuigawanya kidini ili itawalike vyema na kiurahisi...huu ndio ukweli mchungu!

Mungu ni wewe mwenyewe, na huyo mungu yu ndani ya mtu mwenyewe!.
 
Back
Top Bottom