Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,768
- 49,934
Kuna wakati inashindikana kumtambua Rsis wetu anasimamia kitu gani. Analinda haki au yupo kwaajili ya kulinda na kunawirisha uovu.
Kesi ya kubumba dhidi ya Mbowe iliweka wazi uovu wa baadhi ya maafisa wa Polisi. Ilidhihirika wazi maafisa hao wa Polisi ni maharamia dhidi ya raia, wanateka, wanatesa na hata kupoteza watu (komandoo wa JWTZ yuko wapi?)
Kwa kiongozi anayezingatia haki, ni lazima baada ya ushahidi ule wa wazi angeamuru mara moja uchunguzi dhidi ya Polisi wale, na kisha kuchukuliwa hatua.
Jambo la ajabu, Rais Samia aliwatunuku vyeo vikubwa zaidi, ishara ya kuonesha kuwa alikuwa akiwapongeza kwa kazi nzuri ya uovu ule.
Lakini ni Rais Samia huyu huyu aliyewatunuku vyeo maofisa Polisi kwa sababu ya kutenda uovu, kinywani mwake kila mara anatamka umuhimu wa Polisi na mawakili kulinda haki!
Tunamwomba Rais wetu, kauli zake zishibishwe na matendo. Wala asiwe popo, si ndege si mnyama. Asimame upande mmoja kwa uthabiti, asiwe vuguvugu, aamue kuwa moto au baridi.
Kesi ya kubumba dhidi ya Mbowe iliweka wazi uovu wa baadhi ya maafisa wa Polisi. Ilidhihirika wazi maafisa hao wa Polisi ni maharamia dhidi ya raia, wanateka, wanatesa na hata kupoteza watu (komandoo wa JWTZ yuko wapi?)
Kwa kiongozi anayezingatia haki, ni lazima baada ya ushahidi ule wa wazi angeamuru mara moja uchunguzi dhidi ya Polisi wale, na kisha kuchukuliwa hatua.
Jambo la ajabu, Rais Samia aliwatunuku vyeo vikubwa zaidi, ishara ya kuonesha kuwa alikuwa akiwapongeza kwa kazi nzuri ya uovu ule.
Lakini ni Rais Samia huyu huyu aliyewatunuku vyeo maofisa Polisi kwa sababu ya kutenda uovu, kinywani mwake kila mara anatamka umuhimu wa Polisi na mawakili kulinda haki!
Tunamwomba Rais wetu, kauli zake zishibishwe na matendo. Wala asiwe popo, si ndege si mnyama. Asimame upande mmoja kwa uthabiti, asiwe vuguvugu, aamue kuwa moto au baridi.