Je, Rais anaweza kuitoroka nchi yake (defection)?

Je, Rais anaweza kuitoroka nchi yake (defection)?

Beautiful Nkosazana

Senior Member
Joined
Oct 4, 2016
Posts
176
Reaction score
660
Defection is the desertion of one's country or cause in favor of an opposing one.

Edward Snowden mfanyakazi wa shirika la kijasusi la marekani alikimbia nchi yake na kwenda Russia ambapo Russians wanampa siri na kuanza kuzimwaga bila hiyana.

Kayumba Nyamwasa, mkuu wa zamani wa idara ya ujasusi wa rwanda alikimbia nchi yake akitokea ubalozi India na kwenda kuishi South Africa, bila kusahau kisa cha Partick Karegeya ambaye mwishoe akaja kuuawa.

Munir Redfa rubani wa ndege za jeshi la Iraq aliyetoroka na ndege aina ya MIG-21 kutoka Iraq mpaka Israel baada ya kushawishiwa na magaidi ya mossad. click here: Operation Diamond - Wikipedia, the free encyclopedia

Visa ni vingi sana na siwezi kuviandika vyote humu, ila swali langu la msingi ni hili hapa;-

Je, Rais wa nchi, kama vile Mahmoud Ahmadinejad wa Iran baada ya kustaafu hawezi kuitoroka nchi yake ya Iran na kuhamia kwa mahasimu wao Israel ama Marekani kama wanavyofanya majasusi? na endapo itatokea kipi kitaendelea.

Ninakaribisha maoni na uchambuzi
 
Hivi yule Fujimori wa Peru mwenye asili ya Japan si alitoroka nchi yake baada ya kuandamwa na kashfa za ufisadi!? Ngoja nichimbue hii habari.
 
Hivi yule Fujimori wa Peru mwenye asili ya Japan si alitoroka nchi yake baada ya kuandamwa na kashfa za ufisadi!? Ngoja nichimbue hii habari.

Alberto Fujimori yupo gerezani nchini Peru akitumikia kifungo cha miaka 25 alichopewa mwaka 2009 kwa makosa ya ukiukaji haki za binadamu.

Hii ni pamoja na kukimbiakimbia kwanza kwa babu zake Japan halafu akaenda Chile na pale akakamatwa na Peru walioomba msaada kwa Chile.

Kuna wakati huyu mzee aliidhinisha operesheni tatu zilizoitwa La Cantuta, Barrios Altos na Santa ambapo mwandishi wa habari na mfanyabiashara walikuwa ni miongozi mwa watu mbalimbali ambao walitekwa na kuuawa na kikosi cha mauaji alichounda kilichoitwa Grupo Colina.

Huyu mzee alikuwa ni katili sana na tabia zake zilishabihiana na zile za yule jamaa mwingine alieitwa Pol Pot wa Cambodia.

Hatari sana.
 
Defection is the desertion of one's country or cause in favor of an opposing one.

Edward Snowden mfanyakazi wa shirika la kijasusi la marekani alikimbia nchi yake na kwenda Russia ambapo Russians wanampa siri na kuanza kuzimwaga bila hiyana.

Kayumba Nyamwasa, mkuu wa zamani wa idara ya ujasusi wa rwanda alikimbia nchi yake akitokea ubalozi India na kwenda kuishi South Africa, bila kusahau kisa cha Partick Karegeya ambaye mwishoe akaja kuuawa.

Munir Redfa rubani wa ndege za jeshi la Iraq aliyetoroka na ndege aina ya MIG-21 kutoka Iraq mpaka Israel baada ya kushawishiwa na magaidi ya mossad. click here: Operation Diamond - Wikipedia, the free encyclopedia

Visa ni vingi sana na siwezi kuviandika vyote humu, ila swali langu la msingi ni hili hapa;-

Je, Rais wa nchi, kama vile Mahmoud Ahmadinejad wa Iran baada ya kustaafu hawezi kuitoroka nchi yake ya Iran na kuhamia kwa mahasimu wao Israel ama Marekani kama wanavyofanya majasusi? na endapo itatokea kipi kitaendelea.

Ninakaribisha maoni na uchambuzi

Raisi hawezi kuitoroka nchi yake akiwa pia ni Amiri jeshi mkuu.

Kama ulifuatilia suala la jaribio la mapinduzi nchini Uturuki utaelewa hili la raisi.

Pia Mohamed Ahmadinejad nae hana shida sasa hivi anafundisha chuoni na hana wasiwasi na maisha ingawa ana utaalam wa uhandisi wa majengo.

Kuhusu Edward Snowden yeye sio defector bali anaitwa "fugitive" ambae bado anatafutwa na serikali ya Marekani.

Kwa sasa yupo nchini Russia kwa ruhusa ya miaka 3 alopewa kwa hadhi ya ukimbizi na bado anaomba hifadhi ya ukimbizi katika nchi zingine.

Angekuwa "defector" kama wale wa Korea kaskazini ambao hukimbilia Korea Kusini na kuishi huko basi tungempa cheo hicho cha "defector", na hata Russia wangempa nafasi ya kuelezea mambo mbalimbali ya siri.

Ndiyo maana mpaka leo bado anashiriki makongamano mbalimbali duniani kwa njia ya "video conferencing" na anapata hadhira kubwa sana.

Hali hii ni sawasawa na hali ya Kayumba Nyamwasa ambae nae alikimbilia Afrika Kusini na akaomba hifadhi ya ukimbizi.

Lakini huyu Munir Redfa ndiye mfano wa mtu tunaeweza kumwita "Defector" kwamba anapokimbia nchi yake basi anakuwa na nyaraka, nyara au mali ya serikali na taarifa nyingine muhimu na za siri ambapo anakuwa anawapatia nchi maadui, na ukaona kwenye hiyo operesheni "diamond".

Israel na Marekani walitaka kufahamu ilikuwaje Iraq kwa wakti ule ikaweza kutengeza ndege kama ile ilhali wao ndio wataalam wa kila kitu?

Hivyo jaribu kutofautisha Defection (uasi) na Asylum seeking (kuomba hifadhi ya ukimbizi) kwamba ni vitu viwili tofauti.
 
Unatoroka tu hkn cha amiri jeshi
Ukijifanya amiri jeshi unakuwa km sadan husein
Amin dada alikimbis akawa salama.vilevile mobutu.mangistu haile pia.obote.sias baree.
 
Edward Snowden hakuenda Russia directly bali Hong Kong na kuhusu kuvujisha siri kwa Warusi hajavujisha maana lengo lake ilikuwa sio spying bali ku leak tu siri za jinsi NSA walikuwa wana spy mawasiliano ya watu.

Hata alipoondoka kutoka Hong Kong kwenda Russia aliharibu documents zote alizokuwa nazo hakuingia Russia na kitu chochote. KGB walimpa ofa ya kazi akiwa in holding akaikataa kwasababu yeye nia yake haikuwa hiyo.
 
Back
Top Bottom