Je, nina ugonjwa wa moyo au nini?

Je, nina ugonjwa wa moyo au nini?

curtis jr2

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2016
Posts
770
Reaction score
4,588
Nitangulize shukrani kwenu nyote wana JF, kwa kazi nzuri ya kuelimishana juu ya mambo mbalimbali katika jamii yetu, Shukrani sana ziwafikie.

Nimekuwa, na tatizo au maumivu makali sana kifuani upande wa kushoto wa moyo ambayo hayana kikomo, (naumia kila muda usiku mchana) bila hata kufanya kazi yoyote naumia.

Maumivu usambaa mpaka nyuma mgongoni chini ya scapular yanauma mithili ya mtu anayechomwa na kisu au kitu chenye ncha kali au mgandamizo kama kuna jiwe kubwa.

Nimefanya baadhi ya vipimo x-ray mala mbili ambapo mwanzo ilionekana nina pneumonia, na mala ya pili ikaonekana sina tena pneumonia, wala shida ya moyo kwa kipimo hicho cha x-ray.

Nimepima pia ugonjwa wa figo nikaambiwa nina vitu kama vidonda vidonda vidogo kwebye figo ambapo nilipewa dawa lakini tatizo ilo halikuisha, daktari mwingine akanambia labuda nitakuwa na ulcers, na niko na dalili za ulcers lakibi je ndo nipate maumivu makali kiasi icho, dr alienda mbali akahusisha maumivu hayo na kuziba kwa mishipa ya damu au Angina lakini yote hayo sijajua nini shida.

Naomba kwa mwenye Utaalamu kuhusiana na magonjwa ya moyo au mapafu anipe mwanga nifanye nini nipime kipimo gani, au niende wapi ili nisolve tatizo kwani nimekuwa nalo yapata miaka 5 sasa.

Natanguliza shukrani.

IMG_20210401_211633_787.jpg
 
Pole...

Una umri gani?

Je, unapata kiungulia?

Unapata maumivu ya chembe ya kifua(epigastric pain)?

Koo linauma?

Unapumua kwa shida?

Maumivu yanatoka upande wa kushoto hadi mgongoni yanapanda kwenye mabega?

Kama yote ndio au nusu ya maswali ndio cheki H pylori kwanza au utakua na GERD.
 
Nitangulize shukrani kwenu nyote wana JF, kwa kazi nzuri ya kuelimishana juu ya mambo mbalimbali katika jamii yetu, Shukrani sana ziwafikie.

Nimekuwa, na tatizo au maumivu makali sana kifuani upande wa kushoto wa moyo ambayo hayana kikomo, (naumia kila muda usiku mchana) bila hata kufanya kazi yoyote naumia...
utakuwa na tatizo la mfumo wa umeme kwenye moyo ili kui-stabilize pendelea kula ndizi mbivu angalau kila siku ndizi mbili,wakati unajiandaa kwenda pale Jakaya cardiac hospital
 
Nenda kapime kipimo cha moyo lakini anza na kipimo cha vidonda vya tumbo, peptic ulcers usiidharau ivoo, kama hujaigundua itakuendesha uhisi ni moyo kumbe gesi zimejaa.
 
Nenda kapime kipimo cha moyo lakini anza na kipimo cha vidonda vya tumbo, peptic ulcers usiidharau ivoo, kama hujaigundua itakuendesha uhisi ni moyo kumbe gesi zimejaa.
Shukrani sana je nikipima naweza kuondokana na ilo tatizo kuna matibabu
 
Shukrani sana je nikipima naweza kuondokana na ilo tatizo kuna matibabu
Naam matibabu yapo hakuna ugonjwa usio na matibabu lakini pia pendelea sana kula bamia, unazikata kata unaweka chumvi kidogo unachemsha na maji kiasi, ikipoa kunywa, bamia ni tiba nzuri sana kwa vidonda vya tumbo
 
Kama ni Moyo chukua kipande cha wastan cha muhogo mbichi, saga kwenye blender kwa maji kiasi hadi ilainike vizuri,

Chukua yai moja la kienyeji bichi changanya na asali mbichi kijiko kimoja, piga piga hadi vyote vilainike pamoja,

Chukua ule mchanganyiko wa muhogo changanya na mchanganyiko wa asali na yai, weka kwenye glass kunywa, hakikisha unakunywa asubuhi kabla hujala kitu na usiku wakati wa kulala,

Endelea kutumia kwa siku 40, lakini matokeo utayapata ndani ya siku 7 tu,

MUHIMU: Mchanganyiko huo unaweza ukakukera wakati wa kunywa unaweza hata kutaka kutapika, jikaze ni dawa lakini pia unashibisha sana, usiogope ukiona tumbo limejaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom