Je, ni kweli wababa hawana mchango?

Je, ni kweli wababa hawana mchango?

Playboy

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2011
Posts
1,170
Reaction score
945
Huwa najiuliza maswali mengi sana ambayo labda leo naweza kupata majibu yake hapa..

Nimekuwa nikiwasikia watu maarufu kama wasanii au watu waliofanikiwa kimaisha au kama ni msanii amefanikiwa na kufikia kiwango fulani cha kuweza kujimudu kimaisha, wakiwa wana hojiwa "kufanyiwa interview "mara nyingi na wengi wao huwashukuru sana mama zao kuwa ndio mchango mkubwa mpaka kufikia hapo walipo,

Swali, Je ni kwanini huwa hawa'washukuru baba zao na unakuta ana baba na mama ni kwamba wababa hawapendi maendeleo ya watoto wao au sababu huwa ni nini hasa ni mara chache sana utasikia mtu aliyefanikiwa akitoa credit kwa baba yake..

Naombeni mawazo yenu..
 
Hebu anza kujibu wewe kwa mtizamo wako kwanza kisha na mimi nichangie
 
Katika maisha ya kibongo mtoto kabla hajaanza kujitegemea nguzo kubwa huwa ni mama, namaanisha tangu unavyozaliwa mpaka unapata akili ya kujitegemea mtu amboyo anakuwa karibu na wewe na anautumia muda wake mwingi kwa ajili yako ni mama,

Na ndio maana neno lako la kwanza kulitamka lilikuwa ni mama na ndio maana kwenye interviews jina rahisi kulitamka ni mamaBaba ni second isue, kwa maana nyingine sisi wababa ni wasindikizaji tu. (Over)
 
Kiukweli mama ndio aliye na uchungu sana na mwanae,atajaribu kila kitu ili maisha yawe mazuri kwa mtoto wake..ni wababa wachache wenye uchungu wa kweli kwa watoto wao, wangekuwa na uchungu sana usingeona watoto mitaani, wengi wao wanasahau jukumu lao la malezi kwa mtoto, hta kama yupo nyumbani lkn anayeshughulika sana na mtoto ni mama,..ila hawatakiwi kusaulika cz wanamchango pia
 
Katika maisha ya kibongo mtoto kabla hajaanza kujitegemea nguzo kubwa huwa ni mama, namaanisha tangu unavyozaliwa mpaka unapata akili ya kujitegemea mtu amboyo anakuwa karibu na wewe na anautumia muda wake mwingi kwa ajili yako ni mama,
Na ndio maana neno lako la kwanza kulitamka lilikuwa ni mama na ndio maana kwenye interviews jina rahisi kulitamka ni mama
Baba ni second isue, kwa maana nyingine sisi wababa ni wasindikizaji tu. (Over)

Neno la kwanza kulitamka ni mama. Ya kweli hayo?
 
Kuna saikologia kuwa patano lolote lenye sadaka ya damu lina nguvu kuliko patano lolote.Ndiyo maana watu wa kale walilijua dhahiri hivyo hata urafiki wao walichanjia damu ili agano lidumu na kuwa na nguvu.

Mama ni MTU pekee anayefanya agano la damu na mtoto na siyo baba.Hivi pia ndiyo maana ndoa za Leo hazidumu kwa kuwa wanandoa huwa hawana agano LA damu , pindi binti anapokuwa bikira akaolewa na bikira yake wanafunga patano la damu (agano) hili ndilo hudumu sana vinginevyo kudumu ni ngumu sana.
 
Huwa najiuliza maswali mengi sana ambayo labda leo naweza kupata majibu yake hapa..

Nimekuwa nikiwasikia watu maarufu kama wasanii au watu waliofanikiwa kimaisha au kama ni msanii amefanikiwa na kufikia kiwango fulani cha kuweza kujimudu kimaisha, wakiwa wana hojiwa "kufanyiwa interview "mara nyingi na wengi wao huwashukuru sana mama zao kuwa ndio mchango mkubwa mpaka kufikia hapo walipo,

Swali, Je ni kwanini huwa hawa'washukuru baba zao na unakuta ana baba na mama ni kwamba wababa hawapendi maendeleo ya watoto wao au sababu huwa ni nini hasa ni mara chache sana utasikia mtu aliyefanikiwa akitoa credit kwa baba yake..

Naombeni mawazo yenu..

ukweli ni kwamba kila binadam kama hawakumbadilisha hospital ana uakika kuwa huyo ndo mama yake 100% coz ndie aliye beba mimba. ila uwez kuwa na asilimia zote kuwa huyo ni baba yako.

Pili kwenye shida, misukosuko dhiki always mama will be there for u. Soooo ndo sababu kuu.
 
Kwa kweli mchango wa baba umedunishwa sana............

1.Mlitaka baba abebe mimba kivipi?
2.Bila baba kumshughulikia mama haungetungwa(tumboni)
3.Baba zetu hufanya kazi pia......tena zile hatarishi(outdoors) kuilisha familia
4.Ulinzi kwa familia/security.

Mie nafikiri ni mwanaume ndiye anaamua kuanza familia ndipo anapotafuta mke....hauwezi kulazimisha mwanaume kuanz familia.....so we are brought to this world first by the resolution of a man(father)...later we are carried and catered/cared for by mother.
 
Back
Top Bottom