Je, ni kweli udhamini GSM ni wa kimkakati?

Ayenda M

Member
Jan 4, 2018
97
132
Soka la Kiafrika ni la aina yake kabisa. Soka la Kiafrika lina utamaduni wake na mambo yake tofauti na soka la mataifa ya Ulaya. Ukifuatilia sana masuala ya ndani kwenye soka la Kiafrika unaweza jikuta unauchukia mchezo wenyewe.

Kuna vitu vinatokea kwenye soka letu badala ya kukuhuzunisha inabidi ufurahie. Juzi kati kuna baraka ilitokea kwenye Ligi yetu baada ya Kampuni ya GSM kuingia mkataba wa kuidhamini Ligi. Ni jambo la baraka ila ni baraka ambayo inaacha maswali mengi?

1. Je, ni sahihi kwa boss anayetaka kuwa na umiliki wa timu kudhamini Ligi ambayo anamiliki timu? Tumwangalie Eng. Hersi, Haji Manara na Senzo Masingiza ambao ni mabosi pale yanga na Frontmen kwenye timu na kampuni ya GSM ambao ndio walikuwepo kwenye utiaji wa SAINI pale TFF. Kwanini wao? Kwa picha ndogo tunayoipata ni kuwa GSM na YANGA ni kitu kimoja na ndio maana viongozi wake wa juu wanafanya kazi pande zote mbili. Kuna dhana inafichwa na tunazidi kufichwa mashabiki.

Mashabiki walio wengi wanatumia mwamvuli wa AZAM TV kutaka kupitisha mawazo yao lakini wanasahau kuwa Popat pale Azam FC hajawahi kukaa mezani na Mzee Tido Mhando kusaini mkataba wa haki ya Udhamini wa matangazo kupitia Television.

Na watetezi wanasahau kuwa Mzee Bakheresa hajawahi kuingia kamati ya Usajili ya Azam FC au kuonekana akijadili masuala ya timu live tena akiwa na benchi la Ufundi. Kama anafaya kuna ethics anafuata tofauti na Mzee Ghalib. Maboss wa GSM ndo wanasajili, wanalipa mishahara na kutoa bonus kadhaa, tukumbuke kauli ya Khalid Aucho.

2. Dhana ya Umiliki na Udhamini! Hapa ni mtego mkubwa. Ukweli ni upi? Hivi Yanga anadhaminiwa au anamilikiwa na GSM? Kabla hatujajibu swali hili tukumbuke kuwa Club ya Yanga na GSM wapo kwenye transformation kama ilivyo kwa Simba ambayo tiyari ishaanza kumilikiwa kwa 49% ya hisa zake na MO.

Nini nakiona? Endapo mchakato utakamilika inamaana GSM atakuwa anamiliki hisa asilimia kadhaa pale Yanga na probably 49% ya hisa zote na hivyo kuwa mmiliki. Je, wale tunaotetea udhamini wa GSM kwenye ligi kuwa hauna athari kwenye mpira wetu itakuwaje kesho mchakato ukikamilika rasmi? Ina maana kampuni inayomiliki timu, inadhamini ligi kuu ambayo timu hiyo inacheza.

3. Kwanini nguvu kubwa inatumika kuhalalisha udhamini huu? Udhamini wa Azam Tv ulipita bila kelele kubwa za wadau. Udhamini wa NBC ukapita bila kelele. Swali kwanini wadau wanautilia shaka udhamini huu? Hadi FCC kuingilia kati.

Hapa ndipo wenye jukumu la kuongoza soka letu wanapaswa kupatazama. Macho ya wadau wengi yanaona mbali na ndo maana wanahoji. Msemaji wa Timu, Mjumbe wa kamati ya usajili na mshauri (mtendaji mkuu) wa timu wanawakilisha kampuni kwenye utiaji saini wa issue nyeti then watu wanyamaze wasihoji? Hapana. Sio sahihi.

Nitakuwa mtu wa mwisho kuamini kuwa GSM na Yanga si kitu kimoja na udhamini huu sio kimkakati. Na soka hili lina aina yake kabisa.

Pesa kwenye soka letu inahitajika tena sana lakini tuangalie namna nzuri ya kupata udhamini wenye sura nzuri. Itakuwa sahihi zaidi kama GSM ataweka pesa yake CHAMPIONSHIP au LEAGUE ONE maana huko ndo hatutahoji sana.

Ni wakati sasa kuacha mpira uchezwe bila kelele zisizo za lazima. FAIR COMPETITION. Atakayesukuma kete yake vibaya kwenye hili asilaumu mbeleni. Heko kwa wale wanaohoji.
 
Baada ya kukosa ubingwa mara Nne mfululizo, Engineer ameona njia ya mkato ni Kuhonga TFF.

Halafu TFF wanapiga mkwara hakuna kuhoji mkataba wa TFF na GSM

Nakumbusha tu kuwa Mawakili wa Simba SC kwa Morrison kule CAS ndo watasimama katika hili NguvuMoja
 
Eti ni mkataba Kati ya TFF na GSM, usihojiwe na watu binafsi wala vilabu, mpitishe mkataba wenu huko na mmseme mjadala usiruhusiwe halafu uje kuwavalisha tu nembo wengine ambao hamkushirikishwa, TFF wao wavae nembo zilizoandikwa GSM kwasababu ndo mkataba baina yao na tusihoji,waitwe GSFf.
 
Tifufu walisema mktaba huo ni baina ya wao na gsm
Au kwa lugha nyingine mkataba huo ni baina yao na Yanga. Maana baada ya kutiwa saini mkataba wa udhamini na TFF aliibuka Haji Manara kuikejeli Simba kuwa sasa itakuwa mikononi mwa Yanga kupitia udhamini wa GSM na si Yanga wala GSM walikuja hadharani kumkana huyu kichaa.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Azam tv ndio wadhamini wa ligi sio Azam FC.

"Know the difference"
Azam Tv sio wadhamini wa ligi, isipokuwa wana haki za matangazo ya television ya ligi.

Kingine Azam haipo kwenye jezi ya timu, tofauti na timu anazozizamini.

Mkataba wa Gsm na TFF una makandokando mengi ya kikanuni. Kwanza kanuni hakuna sehemu zinaposema mdhamini mwenza anakaa kwenye jezi, isipokuwa mdhamini mkuu. Sasa kwa nini TFF walazimishe gsm akae kwenye jezi wakati ni mdhamini mwenza?

gsm ni kit supplier wa Yanga lakini baadhi ya timu zina kit supplier wengine ambao kiuhalisia ni washindani wa kibiashara wa gsm. Mfano Simba na polisi Tanzania wana vunjabei. Kuwaweka gsm na vunjabei kwenye jezi moja ambao ni washindani kibiashara hauoni ni mgongano wa kimaslahi?

Sikuwahi kudhania kama TFF na gsm ni mbumbumbu kiasi hiki.
 
Azam Tv sio wadhamini wa ligi, isipokuwa wana haki za matangazo ya television ya ligi.

Kingine Azam haipo kwenye jezi ya timu, tofauti na timu anazozizamini.

Mkataba wa Gsm na TFF una makandokando mengi ya kikanuni. Kwanza kanuni hakuna sehemu zinaposema mdhamini mwenza anakaa kwenye jezi, isipokuwa mdhamini mkuu. Sasa kwa nini TFF walazimishe gsm akae kwenye jezi wakati ni mdhamini mwenza?

gsm ni kit supplier wa Yanga lakini baadhi ya timu zina kit supplier wengine ambao kiuhalisia ni washindani wa kibiashara wa gsm. Mfano Simba na polisi Tanzania wana vunjabei. Kuwaweka gsm na vunjabei kwenye jezi moja ambao ni washindani kibiashara hauoni ni mgongano wa kimaslahi?

Sikuwahi kudhania kama TFF na gsm ni mbumbumbu kiasi hiki.
Uyo gharib mwenyewe elimu yake inatatanisha kapata pesa kiunyonyaji na uhujumu uchumi,amezungukwa na machawa na vishoia unafikili kuna kitu hapo
 
Azam Tv sio wadhamini wa ligi, isipokuwa wana haki za matangazo ya television ya ligi.

Kingine Azam haipo kwenye jezi ya timu, tofauti na timu anazozizamini.

Mkataba wa Gsm na TFF una makandokando mengi ya kikanuni. Kwanza kanuni hakuna sehemu zinaposema mdhamini mwenza anakaa kwenye jezi, isipokuwa mdhamini mkuu. Sasa kwa nini TFF walazimishe gsm akae kwenye jezi wakati ni mdhamini mwenza?

gsm ni kit supplier wa Yanga lakini baadhi ya timu zina kit supplier wengine ambao kiuhalisia ni washindani wa kibiashara wa gsm. Mfano Simba na polisi Tanzania wana vunjabei. Kuwaweka gsm na vunjabei kwenye jezi moja ambao ni washindani kibiashara hauoni ni mgongano wa kimaslahi?

Sikuwahi kudhania kama TFF na gsm ni mbumbumbu kiasi hiki.
TFF wana Uroho wa fedha na GSM wana Uroho wa Kombe la Ligi Kuu

Kwahivyo magumashi lazima hapa.
 
Back
Top Bottom