Je, ni kweli elimu imeboreshwa?

Je, ni kweli elimu imeboreshwa?

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,441
Reaction score
1,049
Tangu Rais Samia Suluhu aingie madarakani amefanikiwa kuboresha sekta ya elimu amejenga vyumba vya madarasa zaidi ya elfu 20 nchi nzima na kupelekea kufutwa kwa chaguo la pili kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza na leo wanafunzi wameanza masomo kwa pamoja bila kuhofia upungufu wa madarasa.

lakini pia ukiachana na ujenzi wa madarasa kuna watu wanahoji ya kuwa madarasa hayaendani na idadi ya walimu iliyopo lakini ukweli ni kwamba Rais Samia Suluhu ameajiri walimu zaidi ya 32000 nchi nzima lengo ikiwa kuboresha sekta ya elimu na kupunguza tatizo la ajira nchini.

Vilevile wazazi wanasema wamenufaika na ujenzi wa madarasa hayo maana hawajatoa mchango wowote ukilinganisha na miaka ya nyuma wazazi walilazimika kuchangia michango kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na wazazi wameongeza kuwa january hii sio ya stress ukilinganisha na kipindi kila cha kulipa ada.

Rais Samia Suluhu amefanikisha elimu bila ada kuanzia awali mpaka kidato cha sita sasa elimu ni lazima na sio hiyari mzazi ambaye hatampeleka mtoto wake shule anahatari ya kupelekwa polisi maana Rais Samia Suluhu amefabikisha elimu bure lengo ikiwa ni kuhakikisha watoto wote hata wanaotoka katika familia magumu wapate elimu.
 
inaezekana imeboreshwa, kama mitandao ya simu inavyosema inaboresha vifurushi.
 
Sio kweli usemacho. Njoo field. Uje na data sahihi
 
Tangu Rais Samia Suluhu aingie madarakani amefanikiwa kuboresha sekta ya elimu amejenga vyumba vya madarasa zaidi ya elfu ...
Kwani uboreshaji wa elimu huwezi kusema tu kwa kujenga madarasa na kuajiri walimu,

Madarasa haya mengi,hujengwa katika shule zilezile kila siku,Kuna maeneo huko hawajawah kupata darasa lililo ezekwa kwa bati.
 
Back
Top Bottom