Stephen Ngalya Chelu
JF-Expert Member
- Oct 31, 2017
- 8,288
- 18,571
kiranga mbona unarukaruka sana? Ni nimeomba unijibu ndiyo au hapana umekimbilia kwenye kitu kipya, muda. Unasema kuwa kitu kimoja ili kiongoze kingine kunahitajika uwepo wa muda ambao kiuhalisia haupo kwa hiyo hatuwezi kusema Luna kitu kinachoongoza kingine. Uliposema kuwa The Second Law of Thermodynamics inaiongoza dunia na unaniforce nikubali kuwa kama The Second Law of Thermodynamics ni Mungu. Hiyo The Second Law of Thermodynamics inaiiongoza dunia na vilivyomo kwa kupitia kanuni zipi? Na umesema kuwa kimoja kuongoza kingine ni kitu ambacho hakipo.Umetoa jibu kabla ya kuelewa unachojibu ni nini.
Nikikwambia habari nzima ya "kuongoza furaha, hekima na mambo mengine ya kibinadamu" inatokana na umasikini wa mawazo yetu tu, na kwamba at the quantum level, hata muda (time) haupo, utanielewa?
Na hapo ndipo umuhimu wa kujua The Second Law of Thermodynamics ni nini.
Muda haupo, kwa hiyo hakuna habari ya kimoja kuongoza kingine. Hii ni habari unayoiona wewe kwa sababu ya level yako ya mwili na akili katika ulimwengu.
Lakini ukienda katika level ya subatomic particles, kitu kama photon, traveling at the speed of light, kwa photon hiyo hakuna muda. Hakuna past, hakuna present, hakuna future.
Sasa kabla hujaelewa kwamba muda haupo, unatokana na position yetu tu katika ulimwengu (Einstein's Relativity) na habari za kimoja kusababisha kingine zinaendana na muda, kitu ambacho ukiuchunguza ulimwengu ndani kabisa, hakipo, utasemaje kwamba kinachoongoza maisha ni Mungu, wakati habari nzima ya "kuongoza" ni njozi iliyogubikwa upofu wa macho yetu ya kibinadamu na katika quantum level, hakuna muda wa kufanya kimoja kiongoze na kingine kiongozwe?
kiranga mbona unarukaruka sana? Ni nimeomba unijibu ndiyo au hapana umekimbilia kwenye kitu kipya, muda. Unasema kuwa kitu kimoja ili kiongoze kingine kunahitajika uwepo wa muda ambao kiuhalisia haupo kwa hiyo hatuwezi kusema Luna kitu kinachoongoza kingine. Uliposema kuwa The Second Law of Thermodynamics inaiongoza dunia na unaniforce nikubali kuwa kama The Second Law of Thermodynamics ni Mungu. Hiyo The Second Law of Thermodynamics inaiiongoza dunia na vilivyomo kwa kupitia kanuni zipi? Na umesema kuwa kimoja kuongoza kingine ni kitu ambacho hakipo.
Mzee baba Kiranga unaenda speed sana.Muda haupo.
The Second Law of Thermodynamics ndiho kitu kinachofanya muda uonekane upo, hivyo, kila kitu kinachokuwa ndani ya muda ya kuweza kuwa na muda, kinaendeshwa na The Second Law of Thermodynamics (entropy).
Soma kitabu cha Dr. Stephen Hawking "A Brief History of Time: From The Big Bang To Black Holes". kuna sura moja inaitwa "The Aarrow of Time" inaelezea kwa lugha nyepesi sana kwa nini muda unaonekana upo na kwa nini muda unaenda mbele tu na haurudi nyuma.
Tusome tuelewe sababu za mambo, sio kuyapa jina tu "Mungu" kabla hata hatujayaelewa.
Kwa sababu ukianza kurahisisha tu kwamba "kinachoongoza maisha ndiyo Mungu" utakuja kuambiwa kwamba hiyo dhana nzima ya kitu kimoja kusababisha kingine, tunayo kwa upofu wetu tu wa large scale universe.
Aat the quantum level, causality as we know it breaks down. Cause and effect is violated.
Sasa hapo utaona kwamba msingi wako mzima wa kufikiri kwamba kuna Mungu, dhana ya kwamba kuna kilichosababisha, unavunjwa.
Kwa sababu causality and cause and effect is no longer necessary or central to existence.
Ndiyo maana ukifikiria haya mambo bila kujua na kuchunguza mambo kwa kina, unatoa jibu la kuchekesha kwamba chochote kitakachokuwa chanzo ni Mungu, katika ulimwengu ambao hauhitaji na wala hautambui habari nzima ya chanzo na matokeo ya chanzo.
Kungelea "chochote kilichoanzisha na kinachoongoza ni Mungu" kwa muktadha huu, ni sawa na kusema "rangi ya wimbo wa taifa ni bluu".
Ni sentensi ambayo inaumbika, lakini haina maana.
Unaelewa kwamba hizi habari zinaweza kuwa tofauti, tofauti, tofauti, tofauti kabisa na namna nzima ya kufikiria tuliyozoea?
Sasa kama unakubali kwamba kuna vitu vipo juu ya upeo wa watu kuvijua, kwa nini unajiridhisha kirahisi kwamba Mungu ni chochote kinachoongoza maisha wakati hata hujui kwamba hiyo dhana nzima ya kimoja kuongoza kingine ni mauzauza na mazingaombwe tu ya ulimwengu ambayo wewe unayaona kutokana na size, speed na sehemu yako katika ulimwengu huu?Mzee baba Kiranga unaenda speed sana.
Anyway, kuhusu habari ya muda sitoweza kulizungumzia sana kwa sababu concept niliyonayo kuhusu muda ni tofauti na uliyonayo were. Kwa hiyo sitaki kuizungumzia kwa kuwa sitaki tujadili vitu viwili kwa wakati mmoja.
Mzee baba, ukitaka kujua ukweli kuhusu mungu si lazima ujikite zaidi kwenye mifumo mikubwa mikubwa inayoendesha dunia ambapo kimsingi hata mifumo hiyo haikutokea kwa nasibu.
Inabidi ifike mahali tukubali kuna vitu vipo juu ya upeo wa fikra za mwanadamu. Kwa mfano sasa hivi nikikwambia uangalie mbele na kisha uniambie ni mpaka gani unaotenganisha upande unaouona na ule usiouona? Na huo upande usiouona unaona mini? Na kama hauuoni je, tunaweza kusema huo upande haupo? Siyo vitu vyote vinaweza kuwa katika life experience ili tupate sababu ya kuvikubali.
Haijalishi kuchomoza jua lini, kitendo cha kusema unaamini jua litachomoza iwe kesho au kesho kutwa hiyo ni imani. Na wewe mwenyewe ulisema kuwa hiyo imani ina ushahidi tofauti na imani ya uwepo wa mungu.Nani kakwambia kuchomoza kwa jua ni sawa na kupita Dodoma?
Umefananishaje mawili hayo?
Kwa mantiki gani?
Kwa muktadha gani?
Kuchomoza jua lini?
Kwa mujibu wa nini na lini?
Pamoja Mzee baba. Ila Mimi naamini Mungu yupo hapo kwa sasa hunitoi. Ngoja nikachimbe madude ila kuja kuniaminisha kuwa hakuna Mungu baadae sana, labda nikisha kufa.Sasa kama unakubali kwamba kuna vitu vipo juu ya upeo wa watu kuvijua, kwa nini unajiridhisha kirahisi kwamba Mungu ni chochote kunachoongoza maisha wakati hata hujui kwamba hiyo dhana nzima ya kimoja kuongoza kingine ni mauzauza na mazingaombwe tu ya ulimwengu ambayo wewe unayaona kutokana na size, speed na sehemu yako katika ulimwengu huu?
Kama watu wana upeo fulani wa kujua mambo, zaidi ya hapo ama hawajui na watajua kwa jitihada, ama hawawezi kujua kabisa, hiyo ni sababu ya kuongeza jitihada ya kuchunguza mambo ili tujue kikomo hiki kipo wapi na kipo namna gani.
Hii si sababu ya kuzembea na kuyapa maswali magumu majibu rahisi ambayo hayajajikita katika uchunguzi, majibu kama kusema Mungu ni chochote kinachoongoza maisha na ulimwengu wakati dhana nzima ya kuongoza ni potofu ukiiweka katika muktadha wa ulimwengu.
Unatakiwa kwenda kwa uchunguzi zaidi, si kwa kurahisisha mambo kwa kuvipa jina la Mungu vitu usivyovijua.
1. Unaruhusiwa kuamini chochote. Hiyo ni haki yako ya kikatiba. Provided huvunji sheria.Pamoja Mzee baba. Ila Mimi naamini Mungu yupo hapo kwa sasa hunitoi. Ngoja nikachimbe madude ila kuja kuniaminisha kuwa hakuna Mungu baadae sana, labda nikisha kufa.
Na ndio maana mm nimeacha kumjibu. Hajui lakini anakubishia. Sasa anabisha kitu ambacho yeye hakijui, unapata vipi guts za kubishia ambalo hulijui?. Na hata ukimwambia umekutana na Mungu bado atakubishia utadhani alikutana naye yeye. Anyways, ndio maana bible inasema wapumbavu husema moyoni mwao, hakuna Mungu.Hana hoja yoyote Sema tu anataka kuaminisha watu hakuna Mungu wakati nafsi yake mwenyewe inamsuta.
Ambacho sikijui kipi na ambacho nakibishia kipi?Na ndio maana mm nimeacha kumjibu. Hajui lakini anakubishia. Sasa anabisha kitu ambacho yeye hakijui, unapata vipi guts za kubishia ambalo hulijui?. Na hata ukimwambia umekutana na Mungu bado atakubishia utadhani alikutana naye yeye. Anyways, ndio maana bible inasema wapumbavu husema moyoni mwao, hakuna Mungu.
Habari bwana kiranga.Ambacho sikijui kipi na ambacho nakibishia kipi?
Wewe unajua Mungu yupo?
Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?
Unaweza kuondoa contradiction katika dhana ya kuwepo Mungu huyo?
Unaweza kukubali kwamba square root ya 2 ni 10 kwa sababu hujui square root ya 2 ni nini?
Habari bwana kiranga.
Ningumu kuprove uwepo wa mungu kwa ile njia au mtindo uutakao...labda nkuulize swali pls.
KAMA JANA AU SIKU YOYOTE ULISHAWAHI KUOTA NJOZI UMEOKOTA ELA AU UNARUN.
tuthibitishie hili.
Dimentional reality.
Huyu Mungu unayedai Alisema hayo, ilikua wakati gani?Yaan inashangaza sana watu wanaodai mungu hayupo
huku wakisalimu amri kila kitu alichosema mwenyezi mungu maelfu ya miaka iliyopita
Mfano (1) mungu anasema ndani ya kur an binaadamu hajapewa elimu ya roho ndiyo maana tunashuhudia roho inatolewa mbele ya madakitar bingwa lkn wanashindwa kuzuwia
(2) mungu anasema kila nafsi lazima itaonja mauti
Pamoja na maendeleo makubwa ya kielimu iliyopo sasa
Mmeshindwa kukanusha haya
Inaonekana wazi aliye tamka haya ana elimu zaid yetu
Kwan amesema mambo ambayo mpaka leo hakuna aliye kanusha imebaki bra braa tu
Mungu ni Mungu wa maagano. Hivyo ukimtasama Mungu, mtazamw kupitia maagano yake.Nikisoma Vitabu Vya Dini Hasa Biblia... Mungu wa Kuanzia Kitabu Cha Mwanzo Au Vitabu Vya Kale Ni Tofauti Sana kitabia na Mungu wa Agano Jipya.
Tabia za KiMungu Alizokuwa nazo Katika agano la Kale Nikilinganisha Na Agano jipya naona Tofauti Kubwa Sana
Mfano AGANO LA KALE
Mungu Alikuwa ni Wa Hasira Sana na Anayependa Sana Waumini wake Wafuate Sheria ... Kulikuwa na Sheria Za Kitakatifu Mfano Kujiosha Mwili... mavazi.. Kuhudumia Sehemu ya Kuabudia kwa usafi wa hali ya juu... kuvukisha Ubani... kujitawaza... n.k n.k
Sasa Nitapokuja Kusoma Agano jipya Mungu anakuwa Amebadilika Sana Hasa Katika Kuabudiwa.. .. Yale Mambo ya kale aliyotaka hayapo tena.. Je Mungu amebadilika Hataki Tena Ubani... Zawadi za kuteketezwa Alizosema zinamvutia?
Je Kuna Ubaya Gani Kutoa Sadaka Za hivyo.. kuna Ubaya Gani Kurudia Kule kwa Kale.. Kujisafisha Uendapo Kuabudu..... Kuwa Msafi Au kujitawaza kama kale...
Ndoto zote ni activity katika ubongo, ukiweza ku rekodi activity katika ubongo utaweza kurekodi ndoto uliyoota jana kama unavyoweza kurekodi maneno uliyerokodi jana.
Kusema umeota kitu jana si ajabu kwa sababu almost kila mtu anaota, na dhana ya kuota haina contradiction.
Dhana ya kuwepo kwa Mungu ina contradiction.
Na hata ukishindwa kurekodi ndoto ulizoota jana, hilo halithibitishi Mungu yupo.
Unaweza kuthibitisha Mungu yupo? Hilo ndilo swali.
Hivi kuthibitisha jambo unaloliamini ndiyo inakuaje?
Na kwanini kuwepo na kuamini jambo ambalo una uthibitisho nalo?
Kuamini ni nini na kuthibitisha ni nini?
"Kuamini ni kukubali kitu ni kweli bila ya uthibitisho".Unathibitisha jambounaloliamini ililitoke katika seti ya imani liende kwenye seti ya ujuzi. Imaniunawezakuamini chochote, unawezakuaminikuna pembe tatu yenye pembe sita, lakini, uthibitisho unatenganisha vitu vinavyoaminiwa kwamba vipo wakati havi[po na vile vinavyoaminiwa kwamba vipi na kweli vipo.
Jambo ambalo una uthibitishonalo huliamini, hilo unalijua. Unaloliamini ni lile unalofikirikuwa ni la kweli, lakini huna uthibitisho, kama kusema kwamba Mungu yupo, hiyo ni imani, haijawahi kuthibitishwa.
Kuamini ni kukubali kitu ni kweli bila ya uthibitisho, kuthibitisha ni kuonesha kwamba imani fulani ina ukweli kwa ujuzi zaidi ya imani tu.
Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?
"Kuamini ni kukubali kitu ni kweli bila ya uthibitisho".Unathibitisha jambounaloliamini ililitoke katika seti ya imani liende kwenye seti ya ujuzi. Imaniunawezakuamini chochote, unawezakuaminikuna pembe tatu yenye pembe sita, lakini, uthibitisho unatenganisha vitu vinavyoaminiwa kwamba vipo wakati havi[po na vile vinavyoaminiwa kwamba vipi na kweli vipo.
Jambo ambalo una uthibitishonalo huliamini, hilo unalijua. Unaloliamini ni lile unalofikirikuwa ni la kweli, lakini huna uthibitisho, kama kusema kwamba Mungu yupo, hiyo ni imani, haijawahi kuthibitishwa.
Kuamini ni kukubali kitu ni kweli bila ya uthibitisho, kuthibitisha ni kuonesha kwamba imani fulani ina ukweli kwa ujuzi zaidi ya imani tu.
Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?
Kwa nini unasema kumwambia mtu athibitishe asichokuwa na uthibitishonacho ni kujichanganya?"Kuamini ni kukubali kitu ni kweli bila ya uthibitisho".
"Jambo ambalo una uthibitisho nalo huliamini,hilo unalijua".
" Unathibisha jambo unaloliamini ili litoke katika seti ya imani liende kwenye seti ya ujuzi".
Mkuu hebu twende taratibu.
Kwa ulivyoeleza ni kwamba kuamini ni kukubali jambo bila uthibitisho, na hivyo kama una uthibitisho wa jambo fulani hilo jambo haliwezi kuwa ni imani ni ujuzi kwahiyo hakuna kuamini kwenye lile ulilokuwa na ujuzi nalo.
Kwa maana hiyo mtu ambaye ana amini jambo fulani ni kwamba hana uthibitisho,angekuwa na uthibitisho basi hilo jambo lingetoka kwenye imani na kuwa ujuzi.
Sasa je hauoni kuwa ni sawa na kujichanganya mwenyewe kwa kumwambia mtu athibitishe asicho na uthibitisho nacho?
wote tuna imani tofauti,hatuna uthibitisho"Kwa nini unasema kumwambia mtu athibitishe asichokuwa na uthibitishonacho ni kujichanganya?
Kwa mfano,tumekaandani wawili, nyumba haina madirisha, tunasikia mlio nje.
Mimi nasema ni mvua hiyo, wewe unasemahayo ni magari tu yanapita barabarani, hiyoni sauti ya magari, si mvua.
Wote tunaimani tofauti. Hatuna uthibitisho.
Mimi nakwambia wewe, tutokenje tuthibitishe kama hii ni sauti ya mvua au magari.
Tunatoka nje, tunaona mvua inanyesha na ndiyo inayotoa hiyo sauti, barabara haina gari hata moja.
Tumethibitisha kwamba kilicholeta ile sauti ni mvua, si magari.
Sasa hapo kumwambia mtu athibitishe kitu ambacho hana uthibitisho nacho kunajichanganya vipi?
Huoni kwamba kutaka mtu athibitishe kile ambacho hana uthibitishonacho kumepelekea kuona kwamba kile alichokiamini si kweli,na kuutambua ukweli ni nini?
Kujichanganya kunakuja vipi hapo?
Unalazimisha kujichanganya sehemu ambayo haina kujichanganya?
Huna uthibitisho ukiwa ndani, kwa vile nyumba haina madirisha huwezi kuona nje.wote tuna imani tofauti,hatuna uthibitisho"
Halafu hapo hapo unasema
...tutoke nje tuthibitishe"
Huna uthibitisho unawezaje kusema umethibitisha tena?sijui kama tunaelewana? Unakubali kuwa huna uthibitisho halafu unasema utoke nje ukathibitishe!!!!!!!