Je, Mradi wa KIGAMBONI ndio GESI yao?

Je, Mradi wa KIGAMBONI ndio GESI yao?

KAZIMOTO

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2010
Posts
1,073
Reaction score
325
Mji mpya wa wakazi wa Kigamboni ndio GESI yao hivyo wanatakiwa kuwa wa kwanza kunufaika na mradi huo kupitia Manispaa ya Temeke.

Kuwapa Wakala (KIGAMBONI DEVELOPMENT AGENCY- KDA) nguvu kubwa kwenye mradi huo BADALA ya Manispaa ya Temeke ni sawa na kujenga kiwanda cha kusafisha GESI Kinyerezi - Dar esalaam badala ya Mtwara.

Temeke ni Wilaya iliyo nyuma kuliko zote Dar es salaam imesahaulika kama watu wa mtwara. Ni wakati wao kupata faida kupitia mradi wa Kigamboni.

Dar es salaam inataka kufaidika kwanza na GESI ya Mtwara kabla ya WanaMtwara. Ndivyo hivyo Wizara ya Ardhi inataka kufaidika kwanza na mradi wa Kigamboni kabla ya wanakigamboni kupitia Manispaa yao ya Temeke (madiwani wao na mbunge wao).

Je, danadana za TIbaijuka kuhusu Kigamboni hazifanani na danadana za Muhongo kuhusu Gesi ya Mtwara???
Je, Mradi wa Kigamboni ni GESI nyingine??? Tutegemee nini?

KIGAMBONI KWANZA UHAI BAADAYE????
 
wananchi wa Kigamboni bado wanalalamika kwamba hawashirikishwi. Hayo yako mitaani na kupitia vyombo vya habari hasa vilivyoendeshwa na Chanel 10 kupitia mbunge wao FAUTINE NDUNGULILE na Kamati yao ya madai hayo. Je, ni Mtwara nyingine?

Je, kitendo cha waziri Tibaijuka kuwanyang'anya mamlaka Manispaa ya Temeke hakikuwa kinaashiria kuwanyang'anya wanakigamboni nguvu ya kulalamika kupitia madiwani wao?

Wizara ya Ardhi inaisemea serikali katika mradi wa Kigamboni na Manispaa ya Temeke (madiwani) wanawasemea wanakigamboni. Inakuwaje Wizara ya Ardhi ambayo ndio serikali ilitaka kubaki peke yake na KDA??? kuna nini kinafichwa?
 
Kazimoto uko sahihi. Kigamboni wanajifunza kitu Mtwara

busara inazidi kuwa bidhaa adimu kwenye tunu za taifa, kushirikisha wananchi ni muhimu sana.

Likianza la Kigamboni Vyama vya upinzani vitadandia kama la Mtwara, wanasubiri kwa hamu.

Huko Kigamboni kuna wanaJeshi wengi waliojenga nafikiri pana kazi ngumu maana wapo pia wanajeshi waliostaafu na kuweka makazi yao huko. Wako wengi wameweka makazi huko kutokana na kuwepo kwa kambi za Jeshi za Navy na Mzinga kwa miaka mingi.
 
WanaKigamboni wamelalamika sana kuwa mradi haujawashirikishwa kama ilivyo kwa wanamtwara lakini majibu ya Tibaijuka ni kwamba wameshirikishwa kama ilivyokuwa anajibu Muhongo kwamba wanamtwara wameshirikishwa.

Mbunge wa Kigamboni anasema wananchi hao hawajashirikishwa. nani mkweli.

Kamati inayotetea wananchi hao inasema wananchi hawajashrikishwa. nani mkweli.

Mbunge au kamati au tibaijuka.
 
serikali inatakiwa kuwalipa wakazi wa kigamboni kwanza kabla ya huu mradi wao, kwani walitoa stop order mwaka 2006 hadi kufikia 2008 hakuna chochote walichokifanya. mpaka leo hakuna tathimini ya kina katika eneo hilo.

Kila mkazi wa kigamboni anatakiwa kulipwa fidia zuio hilo la kisheria la miaka 2. Baada ya hapo sasa ndiyo waanze mazungumzo na jinsi ya kuwashirikisha wananchi kwenye huo mradi, kama ni kuwahamisha (mimi siafiki) au kuwa part of that project as land owners, nafikiri hili ni bora zaidi.

Kwa project hiii serikali ijiepushe kuwa DALALI wa ardhi ni dhambi kubwa, Kupokonya ardhi wa wananchi maskini kwa bei chee na kuwapa wawekezaji, hapana kinachotakiwa ni wananchi wakubaliane na wawekezaji na kama ni ununuzi basi iwe kwa bei ya soko.

Nasema hivyo sababu juzi juzi tu yametokea Gezaulole, fuatilia uone ni kina nani hatimaye wamepata viwanja hivyo. leo hii Dar es salaam ukiwa na mil 8 mpaka 10 bado huna uhakika wa kiwanja, maskini anabakia maskini na tajiri anaendelea kujilimbikizia ardhi hata kwa njia ya dhuruma. hili ndiyo linafanya watu wawe na hasira na serikali yao.

Nawashauri serikali acheni UDALALI, kwa nini hamtaki wananchi wauze ardhi kwa bei ya soko? au kuingia ubia moja kwa moja na wawekezaji as owners of that land badala ya nyie kusogelea sogelea mradi?

Katika nchi zote za kiafrica nafikiri ya Tanzania inaongoza kwa kuwagalaziza wananchi wake, sasa haya ya mtwara ndiyo matokeo ya udalali.
 
Waziri anasema serikali itajenga nyumba na kuwahamisha wakazi wa Kigamboni lakini kuna wakazi wana nyumba za matope za thamani ya laki 2 na wengine wana nyumba za thamani ya hadi milioni 50, 100, 2000 nk. Je huyu wa laki mbili itakadiriwa vipi kupewa makazi. Kimsingi Naamini huwezi kulipa fidia ya makazi ya sh. milioni 50 kwa makazi ya laki 2.

Kama wa laki 2 atalipwa cha juu huwezi kukwepa kumlipa wa makazi ya milioni 50 cha juu. Utaratibu bora ni ambao haubagui na kuleta malalamiko
 
Kweli kigamboni mnatakiwa kufanya kama wenzenu wa Mtwara! wameonesha wanaweza kutetea haki zao
Baada ya utawala wa ubaguzi kwa mda mrefu,
je nyie kigamboni mnangoja nini?
Amkeni mdai Ardhi yenu iliyoporwa.
 
Kigamboni haiwezi kuuzwa na kama ikiuzwa basi watu watakula mipunga ya kutosha maana kuna wanajeshi wengi wamejenga kule kuanzia ferry hadi kisiwani, mjimwema na pia kuna wakubwa wana maeneo akieepomtoto wa nyerere pale mjimwema .
 
Wanakigamboni msiposikilizwa anzeni kuchoma nyumba ya abdul jumbe pale maweni, then mchome nyumba ya mwinchumu pale mjimwema (mb wa kg 2005-2010)
wananchi wa Kigamboni bado wanalalamika kwamba hawashirikishwi. Hayo yako mitaani na kupitia vyombo vya habari hasa vilivyoendeshwa na Chanel 10 kupitia mbunge wao FAUTINE NDUNGULILE na Kamati yao ya madai hayo. Je, ni Mtwara nyingine?

Je, kitendo cha waziri Tibaijuka kuwanyang'anya mamlaka Manispaa ya Temeke hakikuwa kinaashiria kuwanyang'anya wanakigamboni nguvu ya kulalamika kupitia madiwani wao?

Wizara ya Ardhi inaisemea serikali katika mradi wa Kigamboni na Manispaa ya Temeke (madiwani) wanawasemea wanakigamboni. Inakuwaje Wizara ya Ardhi ambayo ndio serikali ilitaka kubaki peke yake na KDA??? kuna nini kinafichwa?
 
Back
Top Bottom