Je, maandamano ni haki ya kikatiba?

Je, maandamano ni haki ya kikatiba?

Lucious

Member
Joined
Mar 25, 2011
Posts
47
Reaction score
22
Sifungamani na upande wowote, naogopa kutekwa. Napenda maisha na familia yangu, naipenda Tanzania ya zamani sio ya sasa.

Je, maandamano ni haki ya kikatiba? Ndio swali najiuliza. Je dikteta ni mtu wa namna gani? Je, viongozi wa dini wana haki ya kufanya au kuongelea siasa?

Naanza kuwaza kwa sauti kwa swali langu la 3. Yesu kristo kipindi kile anasaka wanafunzi wake alipita sehemu mbalimbali; kwa wakusanya kodi, mahekaluni na hata akaoshwa miguu yake na malaya.

Kwenye maandamano/mikutano yake alifanya siasa pia. Aliulizwa je, ni haki kulipa kodi? Akawaomba sarafu na kusema mpeni Kaisari vilivyo vyake na Mungu vilivyo vyake. Alijua fika kwenye makutano wanakuja watu wengi, leo misikitini na makanisani sio kosa kukumbusha viongozi wetu kuhusu mienendo au kujisahau sana kwa kulewa madaraka. Wakiomba kura wanaenda makanisani au misikitini au kwa waganga. Imani bila matendo imekufa.

Daudi alianguka kwa kulewa madaraka. Nebukadreza na Wafarao pia. Hekima za Suleiman zinatakiwa. Ukiona dini inaingilia hayo acha kutaka kuombewa au kama neno katubu ni kosa au wakisema ni kosa kisheria rudi kwenye Katiba. Kuombewa sio haki ya kiongozi ni utashi wa mtu. Makanisani au misikitini wanakutana watu so lazima vyote visemwe na kukumbushana.

Swali langu lingine ni je, maandamano ni haki? Katiba yetu inasemaje?

Ibara ya 20(1): Kila mtu anastahili kuwa huru bila kuathiri sheria za nchi, kukutana kwa hiari yake na kwa amani, kuchanganyika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani. Ni haki kiķatiba kuandamana ukisoma sana hakuna sheria inayosema polisi anatoa kibali au anapaswa kuzuia, hakuna mtu aliyeko juu ya sheria hata rais. Ni haki na wajibu wa watu wote kuheshimu utawala wa sheria.

Tatu ninawaza dikteta ni nani? Mwalimu Nyerere alisema, "Katiba yetu inampa rais mamlaka sana na akiyatumia vibaya anaweza kuwa dikteta. Mwaka 1995 Mwalimu alisema "Kuogopwa ni sifa na ada ya madikteta, viongozi halisi hawapendi kuishiriki sifa hii. Kujenga mazoea ya kutii viongozi hata kwenye mambo haramu ni dalili ya woga, ni kukaribisha udikteta"

Leo nimewaza hayo tu, naogopa kutekwa.
 
Maandamano ni haki ya kikatiba lakini madhumuni yake yanaweza yasiwe na haki kikatiba!
 
1: Ndio ukipewa kibali na polisi unayo haki KIKATIBA KUANDAMANA.
 
Maandamano ni haki ya kikatiba lakini madhumuni yake yanaweza yasiwe na haki kikatiba!
Fafanua kwa kina ...kwani yangekuwa na nia ..unayosema wewe
Katiba zingefafanua.. Sio yetu tu ata mfano za nchii zingine zingekuwa nayo...
 
Kama unajue story ya MTEGO WA PANYA

Basi kilicho andikwa hapo juu haina budi kila mmoja kukiunga mkono

Kuna watu au tabaka la watu flani wanajiona haya yanaoendelea wao hayawahusu,

ila nawaambia one day yes,,,,
 
Maandamano katika Nchi nyingi Afrika kwa Mtazamo wa walio Madarakani ni 'Uhaini' ,japo Katiba walizo Apa kuzilinda na kuzisimamia kwa Heshima hazi semi/au kuelekeza hivyo..
 
Maandamo lazima yasimamiwe na kuratibiwa vizuri yakioñekana yanaashiria kuvuruga amani yasiruhusiwe kabisa
 
Maandamano ni haki ya kikatiba lakini madhumuni yake yanaweza yasiwe na haki kikatiba!
Katiba ya tanzania hairuhusu maandamano leta kipengele chochote kinachoongelea maandamano kwenye katiba
 
Katiba ya tanzania hairuhusu maandamano leta kipengele chochote kinachoongelea maandamano kwenye katiba
mkuu tusaidie hicho kifungu cha katiba
au tuwekee hapa tusiojua tufahamu kwamba tunavunja katiba
 
Maandamo lazima yasimamiwe na kuratibiwa vizuri yakioñekana yanaashiria kuvuruga amani yasiruhusiwe kabisa
Je nani anasimami na kwa nn?je amani ipi maandamamo yanavuruga...je ethics zake ni zipi...je hao wanaotisha kuua au kukamata nani anavuruga amani...as ulinitisha lazima.nijiandae....bt wanaovuruga ni polisi na viongozi
 
Back
Top Bottom