Je itawezekana ?

Je itawezekana ?

Kidevu 1

Member
Joined
Jul 3, 2018
Posts
94
Reaction score
63
Wiki mbili zilizopita waziri mkuu alikutana na bodi mpya ya mishahara na moja kati ya mambo ambayo bodi inayafanyia kazi ni mashirika na taasisi za umma kujipangia mishahara hali iliyopelekea kuwa na tofauti kubwa ya mishahara kati ya mashirika na watumishi wengine wa umma hasa TAMISEMI. Mfano muhasibu wa halmashauri analipwa 7k wakati huo huo muhasibu wa tasisi X anakunja 2mill na wote wana elimu sawa na umri sawa kazini.
Bodi hii imeagizwa akashughulike na tatizo ili ilete usawa kwa watu wa kada moja.
Maswali ninayojiuliza
1. Je kuna watu watapunguzwa mishahara au kuna wengine wataongezwa ?
2. Je serikali ina uwezo wa kulipa watumishi wote kwa mishahara ya mashirika ?
3. Hii tume itafanikiwa au ni siasa tu kisha ripoti iwekwe kabatini.
 
Hata wakiongeza shilingi moja, watasema wameongeza mishahara. Sasa ubishe uonje kipigo cha mbwa koko.
 
Hao ni waajiriwa wapya au ni wale wale aliowakuta tangu enzi?? Wanaendelea kuvuta muda huku mkiwa mnatarajia nyongeza tu. Tangu uhuru, tofauti ya Private sector na Government ipo na itaendelea kuwepo. Hata tukimaliza chuo kimoja na kupata alama sawa. Private sector lazima akuzidi tu wewe wa serekalini
 
Ha
Hao ni waajiriwa wapya au ni wale wale aliowakuta tangu enzi?? Wanaendelea kuvuta muda huku mkiwa mnatarajia nyongeza tu. Tangu uhuru, tofauti ya Private sector na Government ipo na itaendelea kuwepo. Hata tukimaliza chuo kimoja na kupata alama sawa. Private sector lazima akuzidi tu wewe wa serekalini
Hapa sio private na government bali ni TAMISEMI na Mashirika ya umma.Mfano
Mwanasheria wa halmashauri na mwanasheria wa TANROAD
 
Ha
Hapa sio private na government bali ni TAMISEMI na Mashirika ya umma.Mfano
Mwanasheria wa halmashauri na mwanasheria wa TANROAD
Aksante kwa kunifafanulia. Hao wote sawa kwani ni watoto wa mama mmoja
 
Back
Top Bottom