Je, Hii Afrika Ni Yetu Kweli?...

Je, Hii Afrika Ni Yetu Kweli?...

JBravo_Bmlo

Member
Joined
Aug 22, 2011
Posts
9
Reaction score
1
Kulingana na Ukandamizwaji wa kikoloni uliopita miaka ile, nina mashaka hii Afrika bado sio yetu... Angalia Namna Rasilimali za Afrika zinavyohujumiwa tena in a good, smart and soft language na Bado hatuna jeuri ya kuzuia badala yake tunamulika tu mambo ya kihamiaji, mipaka na kubaguana huku wote tukiwa weusi tiiii!!! Sikatai Mtu aende au aishi nchi nyingine bila uhalali wala nyaraka, lakini tusidanganyike kuelekeza nguvu zetu dhidi ya mambo yasiyoiinua Afrika ya Waafrika... TUTOKOMEZE tabia ya Waafrika kuwa "REMOTE CONTROLLED" Waafrika Tunaweza....
 
Kwani nani anatu remote control??? Madini yetu tunayauza wenyewe, hatulazimishwi, tena huwa tunaenda kuwafuata na magoti waje kununua.
Tutatue tatizo la vichwa vyetu wa Afrika ndipo tutaweza kukwepa remote controls za races nyingine
 
Africa ni mfano wa nyumba yenye thamani iliyoachwa mikononi mwa watoto yatima wasio jua la kufanya na badala yake wanaongozwa na kaka zao ambao hawajui wanakoelekea ivo wanauza thamani yoyote ya nyumba iliyo mbele yao kwa maslahi yao binafsi na kuwatuliza wadogo zao kwa pipi za big bon. Maisha yanaendelea.
 
Back
Top Bottom