Je, BBC wamekosa weledi wa kitaaluma au dunia imempuuza Tundu Lissu dhidi ya shutuma zake zisizo na ushahidi?

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
2,590
4,601
Macho na masikio ya watanzania na dunia siku ya jana vilikuwa nikutaka kusikia stori ya shutuma ya Tundu Lissu dhidi ya serikali yake ina-balance kwa kusikiliza upande wa pili ambao ni serikali baada ya kiongozi wa serikali ambaye pia ni waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki prof. Kabudi kuhojiwa na kituo kilekile ambacho Tundu Lissu alikitumia kuishutumu serikali juu ya shambulio lake. Kwa shirika kubwa kama BBC kushindwa ku-balance shutuma hizo kwa kusikiliza utetezi wa serikali inatupa picha ya maswali yafuatayo:
  • Kama kweli BBC wana weledi wa kitaaluma na kazi zao, moja ya kazi hizo ni ku-balance stori kwa pande zote kwa kusikiliza utetezi wa upande mwingine. Je, kushindwa kusikiliza serikali hili kuondoa ile sintofahamu si kwenda kinyume na taaluma yao? Je, wameamua kuiamisha dunia kwamba Lissu kaongea ukweli kwa kwenda kinyume na taaluma? Au ni kwamba Lissu wamempuuza na shutuma zake?

  • Kama ni kweli shutuma za Lissu wamezipuuza, kwa nini wamepuuza? Huo si ni ushahidi wa kutosha kwamba Lissu kapuuzwa baada ya dunia kuona alikuwa anapotosha?
My take:
  • Mkoloni atabaki kuwa mkoloni tu na ukoloni wa BBC kwa Tanzania umeenda mbali Zaidi kwa wao kuanza kututawala kifikra hivyo ni jukumu letu sisi watanzania kusimama kwa ajili ya nchi yetu wenyewe.

  • Tumeona na kushuhudia weledi wa vyombo vya kimataifa juu ya nchi za Afrika na nina hakika ingekuwa ni Marekani imeshutumiwa hivyo BBC ingejitahidi kuihoji serikali ya Marekani ili ku-balance stori lakini kwa nchi za Afrika no balancing of story, shutuma tu zinatosha.

  • Hongera sana Prof.Kabudi na Rais Magufuli, heroic leaders of this generation and history makers of the future generations na mimi binafsi nina amini katika uzalendo, uadilifu na umakini wenu.
 
Kama wamempuuza nenda kaulize bunge la European Union. Kama amepuuzwa nenda kaulize wana congress wa Marekani. Kama amepuuzwa fikiria kwa nini misaada imepungua kwenye bajeti yetu.
 
KARLO MWILAPWA ,

..Kwenye suala la TL mnatakiwa mtangulize utu.

..hivi mnavyomuandama mnaonekana ni watu makatili.

..haya mnayoandika yanaichafua serekali kuliko hata lawama na tuhuma anazotoa TL.

..serekali ikiweza kueleza walinzi wa area D walikuwa wapi wakati TL anashambuliwa, suala hili litakuwa limekwisha.
 
Macho na masikio ya watanzania na dunia siku ya jana vilikuwa nikutaka kusikia stori ya shutuma ya Tundu Lissu dhidi ya serikali yake ina-balance kwa kusikiliza upande wa pili ambao ni serikali baada ya kiongozi wa serikali ambaye pia ni waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki prof. Kabudi kuhojiwa na kituo kilekile ambacho Tundu Lissu alikitumia kuishutumu serikali juu ya shambulio lake. Kwa shirika kubwa kama BBC kushindwa ku-balance shutuma hizo kwa kusikiliza utetezi wa serikali inatupa picha ya maswali yafuatayo:
  • Kama kweli BBC wana weledi wa kitaaluma na kazi zao, moja ya kazi hizo ni ku-balance stori kwa pande zote kwa kusikiliza utetezi wa upande mwingine. Je, kushindwa kusikiliza serikali hili kuondoa ile sintofahamu si kwenda kinyume na taaluma yao? Je, wameamua kuiamisha dunia kwamba Lissu kaongea ukweli kwa kwenda kinyume na taaluma? Au ni kwamba Lissu wamempuuza na shutuma zake?

  • Kama ni kweli shutuma za Lissu wamezipuuza, kwa nini wamepuuza? Huo si ni ushahidi wa kutosha kwamba Lissu kapuuzwa baada ya dunia kuona alikuwa anapotosha?
My take:
  • Mkoloni atabaki kuwa mkoloni tu na ukoloni wa BBC kwa Tanzania umeenda mbali Zaidi kwa wao kuanza kututawala kifikra hivyo ni jukumu letu sisi watanzania kusimama kwa ajili ya nchi yetu wenyewe.

  • Tumeona na kushuhudia weledi wa vyombo vya kimataifa juu ya nchi za Afrika na nina hakika ingekuwa ni Marekani imeshutumiwa hivyo BBC ingejitahidi kuihoji serikali ya Marekani ili ku-balance stori lakini kwa nchi za Afrika no balancing of story, shutuma tu zinatosha.

  • Hongera sana Prof.Kabudi na Rais Magufuli, heroic leaders of this generation and history makers of the future generations na mimi binafsi nina amini katika uzalendo, uadilifu na umakini wenu.

Bbc hawahitaji tena kuhoji ukweli ulio wazi kuhusu shambulizi la Lissu.
 
Naona mwaka huu vijana wa buku saba ,Lumumba mmesajili vijana Wengi JF, mmoja wao ni huyu Karl Mwilapwa.Hongereni Lumumba Kwa kutoa ajira kwa vijana!
 
Je nini nani amemuuwa Azzory?
kifo cha Gwanda kimetokea katika kipindi ambacho alikuwa anachunguza hali ya kibiti ambapo watu wengine wengi walikufa katika mazingira ya kuumiza, ni natural pia katika mazingira hayohayo inawezekana na Gwanda alipotea na kufa. hapo ni kwa jinsi nilivyomuelewa Prof.

kwa nini, Prof kahitimisha hivyo? sijui lakini inawezekana kwa taratibu za kiserikali kama mtu mtu asipoonekana kwa kipindi fulani wanachukulia kama kafa lakini inawezekana bado ni mzima ndio maana akasema uchunguzi bado unaendelea wa kujua alipo kama yupo hai.

kama serikali ikipata majibu ya kiuchunguzi ni nani aliyehusika na mauaji ya wale askari kule kibiti na wale watumishi wa serikali kule mkuranga, itasaidia kujua nani aliyehusika na Gwanda.
 
kwa mfano upo darasani, mwalimu akasema 1+1=2 wewe na wenginge wengi bahati mbaya mkasikia 1+1=11, je utakuwa sahihi?
Nilichosikia ni kuwa 1+1 =2,nikasema ngoja nidese kwa wanazengo,nao wana majibu kama hayo isipokuwa wawili watatu ambao ni lumumba FC!!!!
Hawa lumumba fc,hata nyeupe wataiita nyeusi ilimradi wanatetea upande wao!
Mfano ahadi ya mil 50 kila kijiji,wao wamegeuza na kusema kuwa ahadi hiyo ilikuwa majumuisho ya elimu bure,maji na huduma za Afya,ndege,SGR na stiglers!Yaani mil 50 inajilipa humo humo!!Hahahaaaaaa!

Dissapeared and died!!!
 
Back
Top Bottom