Je, ajali zinazosababishwa na taa zinazokuja na gari watu huwa hawafi?

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,039
40,701
Hivi kuna mantiki ipi ya kusema kwamba taa zilizoongezwa kwenye gari (sio toka kiwandani) zitolewe kwenye magari kwani zinasababisha ajali, ila zile zilizokuja na gari (originally toka kiwandani) ziachwe regardless zina mwanga mkali sana au la. Je, hii inamaanisha kwamba zile taa zinazokuja na gari ( na nyingi huwa zina mwanga mkali kuliko hata za kuongezea), ule mwanga ukisababisha ajali, watu huwa hawafi?! Naomba maelezo kidogo kutoka kwa mtaalam.

Juzi nilikamatwa tena na kupewa vitisho na traffic yule yule kwamba eti mi ni jeuri sitaki kutoa zile stip lights nilizoweka kwenye bumper la mbele ilihali nilishazi disable na hazifanyi tena kazi, lakini cha kushangaza magari mengi ya kisasa yanakuja na inbuilt stip lights ndani ya head lamps zake, na zina mwanga mkali maradufu! Je, ajali za hizo inbuilt strip lights watu huwa hawafi???!!!!

Exhibit 1.
Hii ndio aina ya accessory led light niliyofunga kwenye bumper la mbele.
Screenshot_2017-01-22-13-13-49.png

Exhibit 2.
Hii ni gari ya kisasa, Mercedes benz C300, ina inbuilt Led lights zenye mwanga mkali sana. Na zinaruhusiwa barabarani, regarless.
Screenshot_2017-01-22-13-21-25.png

Unless nikadhibitishiwa kwamba, Led lights za hiyo benz zikisababishaajali watu huwa hawafi wala kuumia, basi sitatoa za kwangu za kuongeza, na nitaendelea tu kulipa faini mpaka niridhishwe na majibu.

USHAURI: Traffic police wapewe vifaa maalum vya kupima 'Luminosity index' ya taa za gari ili kubaini risk factor ya kusababisha ajali, hicho ndio kipimo sahihi! Ni kama tunavyopima pumzi ya dereva ili kubaini alchol levels, hiki ndio kipimo sahihi! Vinginevyo tunachofanya ni sawa na kusema, mtu atakaelewa pombe iliyotengenezwa nyumbani na kuendesha gari akamatwe, ila yule atakaekunywa zile whisky kali za ulaya(toka nje) aachwe, as if pombe ya ulaya ajali zake watu huwa hawafi.
 
Ukiwa na tatizo moja haimaanishi ukubali na tatizo la pili, hizo taa za kuongeza zinazidi kuongeza tatizo haswa ukizingatia tayari tulishaona dili na wengine wameweka kila mahali kiasi kwamba imekuwa balaa.
Kuna wengine unakuta gari imefungwa mataa kama kiwanda! Binafsi nilishaingiza gari yenye mzigo katika mtaro kwa mataa ya namna hiyo, adha hii tunaielewa sana haswa sisi watu wa safari ndefu na tunaotembea zaidi usiku.
Hili la gari kuwa na taa zake za namna hiyo ni chache kuliko ule 'mlipuko' wa kila mtu kuweka mataa apendavyo.
 
Ukiwa na tatizo moja haimaanishi ukubali na tatizo la pili, hizo taa za kuongeza zinazidi kuongeza tatizo haswa ukizingatia tayari tulishaona dili na wengine wameweka kila mahali kiasi kwamba imekuwa balaa.
Kuna wengine unakuta gari imefungwa mataa kama kiwanda! Binafsi nilishaingiza gari yenye mzigo katika mtaro kwa mataa ya namna hiyo, adha hii tunaielewa sana haswa sisi watu wa safari ndefu na tunaotembea zaidi usiku.
Hili la gari kuwa na taa zake za namna hiyo ni chache kuliko ule 'mlipuko' wa kila mtu kuweka mataa apendavyo.

Sijawai kusikia hapa nchini ajali iliyosababishwa na taa za LED.
 
Ukiwa na tatizo moja haimaanishi ukubali na tatizo la pili, hizo taa za kuongeza zinazidi kuongeza tatizo haswa ukizingatia tayari tulishaona dili na wengine wameweka kila mahali kiasi kwamba imekuwa balaa.
Kuna wengine unakuta gari imefungwa mataa kama kiwanda! Binafsi nilishaingiza gari yenye mzigo katika mtaro kwa mataa ya namna hiyo, adha hii tunaielewa sana haswa sisi watu wa safari ndefu na tunaotembea zaidi usiku.
Hili la gari kuwa na taa zake za namna hiyo ni chache kuliko ule 'mlipuko' wa kila mtu kuweka mataa apendavyo.
Hivi unaelewa hata ulichokiandika hapa? If such was the case, wangesema tu kwamba idadi ya Led lights iwe mwisho ni mbili, basi. Otherwise, unataka kuniambia wale watengenezaji wa magari kule ujerumani na Japan hawakufanya luminosity tests za hizo inbuilt led lights ili kubaini risk factor?! I don't think so, maana safety standards za huko ni za juu sana, sidhani kama wangeruhusiwa kufunga hizo led lights kama kweli zinasababisha ajali.
 
Kama hakuna majibu ya hii hoja basi nisione mtu ananisimamisha kuniuliza kuhusi taa zangu za urembo, tusitafutane ubaya
 
Hivi unaelewa hata ulichokiandika hapa? If such was the case, wangesema tu kwamba idadi ya Led lights iwe mwisho ni mbili, basi. Otherwise, unataka kuniambia wale watengenezaji wa magari kule ujerumani na Japan hawakufanya luminosity tests za hizo inbuilt led lights ili kubaini risk factor?! I don't think so, maana safety standards za huko ni za juu sana, sidhani kama wangeruhusiwa kufunga hizo led lights kama kweli zinasababisha ajali.
Umeelewa nilichoandika ndiyo maana ukajitahidi kujibu, kila Nchi inakuwa na sera na sheria zake na ndio maana kuna limit ya mwendo japokuwa gari yako inaweza kuwa hata na speed mia tatu hivyo ni vema kutii mamlaka.

Umeshawahi kusafiri kwa kuendesha gari mwendo mrefu usiku? Binafsi naendesha lori mwaka wa kumi huu na naelewa vema changamoto za hayo mataa unaweza kuta mwengine kafunga taa kama meli ili uone mbele inabidi usimame apite kwanza, yote ya nini?
Sio kila kitu ni cha kulalamika vitu vingine vina shida yake.
Umezungumzia kwamba kungewekwa sheria ya kuwa ziwekwe ngapi kwenye gari, hiyo haisaidii maana kuna nyingine ni ndogo sana lakini mwanga wake ni mkubwa mno hata kama ikiwekwa moja.....watu weupe walipoweka taa kwa utaratibu maalum kwamba ipi iwashwe wapi si wajinga.
 
Umeelewa nilichoandika ndiyo maana ukajitahidi kujibu, kila Nchi inakuwa na sera na sheria zake na ndio maana kuna limit ya mwendo japokuwa gari yako inaweza kuwa hata na speed mia tatu hivyo ni vema kutii mamlaka.

Umeshawahi kusafiri kwa kuendesha gari mwendo mrefu usiku? Binafsi naendesha lori mwaka wa kumi huu na naelewa vema changamoto za hayo mataa unaweza kuta mwengine kafunga taa kama meli ili uone mbele inabidi usimame apite kwanza, yote ya nini?
Sio kila kitu ni cha kulalamika vitu vingine vina shida yake.
Umezungumzia kwamba kungewekwa sheria ya kuwa ziwekwe ngapi kwenye gari, hiyo haisaidii maana kuna nyingine ni ndogo sana lakini mwanga wake ni mkubwa mno hata kama ikiwekwa moja.....watu weupe walipoweka taa kwa utaratibu maalum kwamba ipi iwashwe wapi si wajinga.
1.) Indeed ni vyema na busara kutii mamlaka, lakini itakuwa ni upunguani mwenye mamlaka akikwambia usimpandishe mkeo seat ya mbele eti kisa ataleta mazungumzo ya kimahaba na kusababisha ajali, halafu wewe ukatekeleza bila kuhoji wala kukaribisha majadiliano +ve yenye kujenga kwa pande zote mbili, mkumbuke hii nchi sio ya baba yenu, ni yetu sote!

2.) Jadili hoja kwa kuzingatia exhibit 1 na exhibit 2, basi, maana exhibit 1 ndio niliyofunga na ninabughudhiwa na askari wenu. Hiyo taa kwenye exhibit 1, kwa specifications ilizonazo , zikifungwa mbili, na kwa luminosity iliyonayo inaweza kusababisha ajali?! Don't be ridiculous.
Msitake kukataza watu kula maharage eti kisa wengine huwa wanajamba sana, deal na hao wanaojamba, nyie vipi?

3.) Hilo suala la taa ipi iwashwe wapi lingeleta mashiko kama kwenye exhibit yangu ningeleta issue ya 'fog' lights ambazo huwashwa kwenye ukungu. Hapa nazungumzia 'daytime Led lights' ambazo ni subsidiary lights zinazosaidia gari kuonekana vizuri na mtu anaekuja mbele yako, pia zinapendezesha mno gari.
 
Kiukweli me naona hapo wamekurupuka maana kuna gari zina taa kali kama zile noah voxy na ni taa ambazo zinakuja na gari,,,kwahiyo kama taa za ziada zina sababisha ajali kwa mwanga mkali wakae wakijua kuwa kuna gar zina taa kali na ni taa za kuja na gari je watasema wazitoe wafunge koroboi,,,watu wanakurupuka tu ndio maana yule wa tanesco kibarua kiliota kwa kukurupuka kuongeza bei ya umeme
 
Kiukweli me naona hapo wamekurupuka maana kuna gari zina taa kali kama zile noah voxy na ni taa ambazo zinakuja na gari,,,kwahiyo kama taa za ziada zina sababisha ajali kwa mwanga mkali wakae wakijua kuwa kuna gar zina taa kali na ni taa za kuja na gari je watasema wazitoe wafunge koroboi,,,watu wanakurupuka tu ndio maana yule wa tanesco kibarua kiliota kwa kukurupuka kuongeza bei ya umeme
Mi nadhani wenye magari wanageuzwa ATM ya watu flani kuwakamua pesa kwa namna na kadri watakavyojisikia.., this is wrong!
 
Mi nadhani wenye magari wanageuzwa ATM ya watu flani kuwakamua pesa kwa namna na kadri watakavyojisikia.., this is wrong!
Me nahisi kutakuwa kuna kiongozi tu mshenzi alikutana na washenzi wenzie waliokuwa wamemuashia hizo taa usiku kwa hasira ndio kaja na hilo wazo,,bila kufikiria wale wauzaji wa hizo taa watazipeleka wap,,, aah kweli hii ni tanzagiza,,kuna baadhi ya mikoa wanatabia za kuteka magari sasa hizo taa huwa zinasaidia sana kuona mbali,,unakuta dereva anayaona magogo yaliyotegeshwa njian akiwa mbali na anageuza anakimbia bila kudhirika,,cjui hawa jamaa zetu huwa hawachambui mambo kwa upana zaidi,,kabla ya kuamua au ni ujeuri tu,,
 
Itasomeka mpaka kwenye sehem zetu za ccccccccyr!kesho itakuja ya matairi yenye kashata zenye mtindo huuu marufuku Kwa gari binafsi
 
Back
Top Bottom