888I
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 445
- 553
Uchaguzi mkuu unakaribia na katika jimbo la Simanjiro wanatajwa wengi kuwania nafasi ya ubunge , Tunahitaji angalau wawakilishi wenye kiwango kikubwa cha Elimu ,si elimu itasaidia lakini angalau itawafanya wabunge kuwa waadilifu.
Huenda isifanye wawe waadilifu lakini basi itawafanya waweze kufikiria kikamilifu na si kupelekwa pelekwa kwasababu ya kutokua na uwezo wa kufikiri ama kuamua kwa mantiki.
Hatuhitaji wawakilishi wenye Njaa maana mwenye njaa Hana msimamo.
JK wa kwanza alisema Hatuhitaji wanasiasa Malaya Malaya ambao wananunulika,nami nasema tunahitaji wanasiasa wenye misimamo thabiti kwaajili ya wananchi anao wawakilisha.
Mwanasiasa anaye sifia tu jimboni hakuna barabara Wala maji lakini akisimama bungeni kuchangia bajeti ya wizara ya Uchukuzi anasifia sifia tu hapana hatuhitaji tunahitaji anayeweza kukosoa kushauri na kusifia bila kujali yupo wapi.
Tunahitaji muwakilishi anayefahamu kuwa anatuwakilisha si anawakilisha serikali, Kiongozi anayefahamu kuwa yeye si sehemu ya Serikali yeye ni muwakilishi wa wananchi kwahiyo anaisimamia serikali.
Ikiwa tutashiriki Uchaguzi basi tupate wawakilishi sahihi.
Huenda isifanye wawe waadilifu lakini basi itawafanya waweze kufikiria kikamilifu na si kupelekwa pelekwa kwasababu ya kutokua na uwezo wa kufikiri ama kuamua kwa mantiki.
Hatuhitaji wawakilishi wenye Njaa maana mwenye njaa Hana msimamo.
JK wa kwanza alisema Hatuhitaji wanasiasa Malaya Malaya ambao wananunulika,nami nasema tunahitaji wanasiasa wenye misimamo thabiti kwaajili ya wananchi anao wawakilisha.
Mwanasiasa anaye sifia tu jimboni hakuna barabara Wala maji lakini akisimama bungeni kuchangia bajeti ya wizara ya Uchukuzi anasifia sifia tu hapana hatuhitaji tunahitaji anayeweza kukosoa kushauri na kusifia bila kujali yupo wapi.
Tunahitaji muwakilishi anayefahamu kuwa anatuwakilisha si anawakilisha serikali, Kiongozi anayefahamu kuwa yeye si sehemu ya Serikali yeye ni muwakilishi wa wananchi kwahiyo anaisimamia serikali.
Ikiwa tutashiriki Uchaguzi basi tupate wawakilishi sahihi.