Jaman tushauriane. Graduates kila mwaka wanamwagika, na ajira hazipatikani.
Watu wanadhani nchi hii ilikuwa hivi tangu zamani. Miaka ya 80 tulipo hitimu A Level na Chuo kazi zilikuwapo si kwa wahitimu wa vyuo tu bali hata kwa wahitimu wa secondari na mwajiri alikuwa serikali na mashirika ya umma.
Sasa hivi kuna waajiri wengi zaidi ya miaka ya 80 lakini ajira ni chache zaidi. Tukubali kwanza kwamba ajira ni chache na pili tujiulize kwa nini.
Kumshauri mtu atoe rushwa ili apate kazi ni ajabu mkubwa.
Mwajiri anaye hitaji mtu wa kumfanyia kazi yenye kuingiza TSHS 200M kwa malipi ya Tshs 90M hahitaji rushwa ya namna yeyote.Anachohitaji ni mtu mwenye ujuzi anao utaka.
Kwa maoni yangu; Tatizo la ajira linatokana na tofauti kubwa kati ya Kile mwajiri anachohitaji na Aina ya Elimu inayo tolewa na vyuo. Mitaala yetu ya elimu ni ile ile ya zamani wakati Typewriter zilipokuwa zinatamba maofisini.
Klamu za Epica zilipokuwa kitendea kazi kikubwa. Leo hii naamini kila msomi anahitaji kujua kwa undani Microsoft Word Excel Powerpoint na programme nyingine kwani vitu hivi sasa hivi ni sawa na Epica na Typewriter za enzi zile.
Mentally Elimu yetu inalenga kuwajenga wahitimu kuajiriwa. Ni wakati sasa wa Vyuo vyote kutengeneza mazingira ya elimu yatakayo mfanya mhitimu ajae mawazo ya kujiajiri.
Tuna matatizo mengi sana nchini Tanzania yanayohitaji kutatuliwa na Watanzania wenyewe. Matatizo haya kamwe hayawezi kutatuliwa na WAKUJA.
Juzi hapa nilikuwa naongea na Rafiki yangu kutoka Gambia akaniambia kwamba nchini Gambia Maganda ya Karanga yanatumika kutengenezea Mkaa tena mkaa mzuri sana na ni Biashara ya Mabilioni.
Sisi huwa tunachoma mikaa ya Mikorosho ambayo kwa ubora ni nyanya kabisa na hakuna anayependa kutumia mkaa wa myi wa korosho.
Endapo wenzetu wanatumia maganda ya karanga kutengenezea mikaa yenye ubora wa kimataifa kwa nini sisi tunashindwa kufanya utafiti YAKINIFU wa kutengeneza mkaa bora kwa kutumia miti ya mbaazi, mikorosho au aina nyingine ya miti inayiokua upesi na ambayo ni migumu mara 4 au tano ukilinganisha na maganda ya karanga?
Kwa nini hatufanyi utafiti wa kutumia vipande vya mbao matawi ya miti marandio ya mbao nk kutengeneza mkaa wenye hadhi na ubora wa kimataifa???
Tunahitaji ku introduce somo jipya katika Level ya Vyuo lenye lengo la kuwafunua macho na bongo vijana wetu ili waukwae uwezo wa kuona mianya yenye kuleta tija iliyo kila kona ya nchi yetu.
Wasomi inabidi kuanzisha tafiti zenye lengo la ku refine products zetu za ndani ili ziweze kupambana na zile za nje huku zikituletea kipato.
Kuna kufyatua tofari za sementi kwa kutumia udongo wa kawaida kabisa. UTAFITI unahitajika. Ku refine namna ya kutengeneza Meza coffee Table zenye ubora wa juu kabisa kwa kutumia mbao laini Utafiti ni Muhimu.
Kuchonga mawe ya kawaida kabisa kwa ajiri ya mapambo ya nje na ndani kwa kutumia Technolojia rahisi na iliyopo tayari.
Geuzeni frustration ya mtu kuwa changamoto siyo kumchamba mtu
We need toThink Critically.