Kweli beach ni kuzuli lakini sie wenzenu wa Kawe hatufaidi beach yetu kwani mafisadi wamejenga nyumba zao na kufunga njia zote za kuendea huko beach; kuna njia moja tu pale kwa Rupia ambayo nayo itakujafungwa mwenye kiwanja akijajenga!! Nawashauri wahusika kuzuia ujenzi haramu unaoendekea Kawe beach sehemu ya Sykes close ambao hata baada ya kuzuiwa na halmashauri hawa waraabu wameendela kujenga na sasa wanajenga gate kuzuia kabisa access ya beach. Sasa wakituzuia kwenda beach vijana wetu si ndio wataanza kufanya uhalifu ; wahusika wa wilaya ya Kinondoni akiwemo Mbunge wa Kawe walifuatilie jambo hili kwani ni la hatari huko mbele lisiposhuhulikwa.