Namcheki Siyoi akiongea kumbe hata kiswahili hajui vizuri,inawezekana kweli huyu jamaa ana passport mbili za kusafiria.Anatoa ahadi za uongo mtupu kama kutatua migogoro ya ardhi na kuwaletea maji wana Arumeru Mashariki wakati serikali ya CCM imeshindwa kueanya hivyo kwa miaka 50 sasa sijui kama wataweza kwa miaka hii michache iliyobaki.
Naona kwa mara nyingine tena ITV waanza kutumika tena,mtangazaji anadai CCM haijakodi watu kutoka mikoa ya jirani na wilaya za jirani, sijui anaushaidi gani na hili jambo?mtangazaji anadai ccm huwa haina utaratibu huo na ni chama cha kuleta maendeleo siku zote, mkapa ameanza na salamu ya mambooo zaidi ya mara 4 nadhani anatafuta pozi ya kuanza porojo, anadai kunawatu wamekwapua ardhi kwahiyo atamshauri raisi ayafanyie kazi, je Mkapa amekuwa raisi kwa muda gani hakujajua haya? kweli huyu mzee hana aibu.. anamalizia kwa kudai kuwa hao wanaomtuhumu Sioi kutoboa masikio ni wapumbavu tu.. anawashauri polisi kuwashughulikia wote watakao leta vurugu. Mkama alianza kwa kuwa amininisha watu kuwa hakuna maendeleo inje ya ccm yatakayopatika kama watachagua wapinzani. Kwa kweli ni tunasafri ndefu sana ya kuleta mageuzi katika nchi hii ili kuhakikisha mali asili Mungu alizotujaria zinatunufaisha watanzania.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.