jaxonwaziri
JF-Expert Member
- Feb 17, 2010
- 375
- 195
Watanzania tumeshuhudia mbinu chafu za kila namna za kuharibu uwezo wa watanzania kutathmini na kufanya uamuzi sahihi juu ya kiongozi anayefaa kuongoza taifa hili ifikapo October 31.
Wametumia rushwa, wametumia kashfa juu ya maisha binafsi, wametoa hela ili magazeti yachapishwe na kugawiwa bure n.k
Watanzania wenzangu, tuinuke kwa pamoja kuhamasishana kwamba hatuitaki CCM tena, maana kwa sasa huu ni muamko thabiti kudai nchi yetu, utu wetu kutoka mikononi mwa mafisadi hawa! Tumedhalilika vya kutosha, tumevumilia vya kutosha. Tushikamane, tuikomboe nchi yetu, tummpigie kampeni na mwishowe tumchague Dk Slaa kuwa rais wetu ifikapo October 2010.
Ni kweli hatuna fedha za kutosha kuweka mabango kila pahala, lakini pia hata nyerere alipokuwa anaikomboa nchi hii wakati wa ukoloni, hakuweka mabango kila pahala! Watu walihamasishana, wakahamasika, wakafanya maamuzi magumu na thabiti.
INUKA MTANZANIA, HATMA YA TAIFA LAKO IPO MOKONONI MWAKO LEO.....!
Wametumia rushwa, wametumia kashfa juu ya maisha binafsi, wametoa hela ili magazeti yachapishwe na kugawiwa bure n.k
Watanzania wenzangu, tuinuke kwa pamoja kuhamasishana kwamba hatuitaki CCM tena, maana kwa sasa huu ni muamko thabiti kudai nchi yetu, utu wetu kutoka mikononi mwa mafisadi hawa! Tumedhalilika vya kutosha, tumevumilia vya kutosha. Tushikamane, tuikomboe nchi yetu, tummpigie kampeni na mwishowe tumchague Dk Slaa kuwa rais wetu ifikapo October 2010.
Ni kweli hatuna fedha za kutosha kuweka mabango kila pahala, lakini pia hata nyerere alipokuwa anaikomboa nchi hii wakati wa ukoloni, hakuweka mabango kila pahala! Watu walihamasishana, wakahamasika, wakafanya maamuzi magumu na thabiti.
INUKA MTANZANIA, HATMA YA TAIFA LAKO IPO MOKONONI MWAKO LEO.....!