Itikadi,falsafa na misingi ya ACT-Tanzania

Itikadi,falsafa na misingi ya ACT-Tanzania

Wiston Mogha

Senior Member
Joined
Feb 13, 2014
Posts
168
Reaction score
141
1ITIKADI
ACT-Tanzania inaamini katika elimu, uadilifu, kujitegemea na bidii katika kazi kama njia kuu ya kujikomboa dhidi ya umaskini, ujinga na maradhi. Hii ndio misingi iliyoasisi Taifa la Tanzania. Hivyo basi falsafa ya ACT Tanzania ni UNYERERE, ikiwa ni ishara ya dhamira ya kurudisha na kuhuisha misingi iliyoasisi taifa la Tanzania. Kiitikadi ACT Tanzania imejikita katika MRENGO WA KATI KUSHOTO (Center Left Party) na itasimamia Demokrasia Jamii kama dira ya sera za maendeleo ya uchumi nchini Tanzania.

MISINGI YA CHAMA
1.Uzalendo
Ili wananchi waweze kushiriki katika utumishi wa umma na kutoa michango yao mbalimbali kwa dhati na kwa moyo, ni muhimu mazingira yawepo ya kuhakikisha kwamba wananchi wanakuwa na mapenzi yasiyotikisika kwa nchi yao. Kwa msingi huu, ACT-Tanzania itajenga mazingira mwafaka ya wananchi kuipenda nchi yao ili wajitoe kikamilifu katika kuijenga na kuilinda.

2.Usawa
ACT-Tanzania inaamini katika usawa katika nyanja zote. Tunaamini kwamba mafanikio ya mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla yatatokana na bidii katika kazi. Kwahiyo, ACT Tanzania kitapigania kuwepo usawa wa fursa na mazingira mazuri kwa watu wote katika kuhakikisha kwamba kila mtu na kila kundi katika jamii linakuwa na fursa sawa ya kufanya kazi za kujiajiri au kuajiriwa, na kwamba kipato kitokanacho na kazi halali ndicho kitakuwa kipimo cha mchango wake katika jamii na taifa.

3.Uadilifu
Uadilifu katika maisha binafsi na katika jamii utakuwa ndio msingi na mwongozo mkuu wa viongozi na wanachama wa ACT-Tanzania. ACT-Tanzania inaamini kwamba uadilifu ndio msingi na nguzo kuu ya mapambano dhidi ya rushwa na maovu mengine katika jamii. Kama wanachama wa ACT-Tanzania tutajitahidi wakati wote kutumikia na kuishi kwa uadilifu uliotukuka siyo tu kama taasisi bali pia katika maisha yetu binafsi.

4.Uwazi

ACT Tanzania inaamini katika uwazi kwenye mambo yote ya kijamii na kitaifa. Hivyo basi viongozi na wanachama wa ACT-Tanzania wana wajibu wa kupigania uwazi katika mambo yote wanayofanya kwa ajili ya umma. Uwazi huu ni msingi wa kupambana na vitendo vya ukosefu wa maadili na ufisadi na hivyo tunaamini njia sahihi ni kuhakikisha kuwa wanachama na wananchi waliotupa dhamana ya uongozi wanajua yanayofanywa na chama na serikali yao.

5.Uwajibikaji
Sambamba na uwazi, ACT- Tanzania inaamini kwamba kila mwananchi na kiongozi mwenye dhamana katika umma ana wajibu katika jamii na Taifa kwa ujumla na ni jukumu lake kutekeleza wajibu huo bila kinyongo. Aidha, mwanachama na kiongozi atokanaye na ACT Tanzania anapaswa kuwajibika kwa maneno na matendo yake katika utumishi au nje ya utumishi wa chama au taasisi yeyote ya umma.

6.Demokrasia Raslimali
ACT-Tanzania inaamini kuwa demokrasia ndiyo msingi wa kujenga fikra pevu na kueneza uhuru wa mtu, jamii na Taifa kwa ujumla. Hivyo basi, viongozi na wanachama wa ACT-Tanzania watapigania uwepo wa demokrasia ya kweli katika kila ngazi, ndani na nje ya chama. Hata hivyo, ACT Tanzania inaamini kwamba umaskini na ufukara ni kikwazo kikubwa katika kufikia fikra huru. ACT Tanzania inaamini kwamba wananchi kuwa na sauti katika umiliki na uendeshaji wa raslimali za Taifa ndio njia sahihi na ya haraka ya kumaliza umaskini. Chama kinaamini katika demokrasia raslimali ikiwa ni imani kuwa utajiri wa Maliasili ya Afrika kwa ujumla na Tanzania hususani; ni lazima utumike kwa maendeleo ya watu wa Afrika na Tanzania. Hivyo basi, sera za chama zitaelekeza mfumo wa umiliki wa utajiri wa Nchi kuwa ni mali ya wananchi na uendelezwaji wake utafanywa kwa faida ya wananchi kwa ruhusa yao, yaani demokrasia raslimali.

7.Haki ya Kupata Hifadhi ya Jamii
Chama cha ACT - Tanzania kinaamini kuwa kila mtanzania ana haki ya kupata hifadhi ya jamii na hivyo sera zake zitaelekeza serikali kuwajibika katika kutoa haki hii kikatiba. Hifadhi ya jamii ni pamoja na pensheni, bima ya afya, ulinzi wa kijamii kwa wazee, watu wenye ulemavu na wananchi waliofukarishwa na mfumo wa uchumi wa kibeberu.

8.Utu
ACT-Tanzania inaamini kuwa sera, mipango na shughuli zozote za kichama au za kiserikali zitakuwa hazina mafanikio ya kudumu kama hazitatambua, kuheshimu na kulinda utu wa kila Mtanzania. Ni kwa sababu hiyo tunu kuu itakayotuongoza katika utumishi wa umma ni kuheshimu, kutambua na kulinda utu wa kila mtu bila kujali tofauti zozote ambazo zinawatofautisha watu.

9.Umoja wa Afrika
Chama cha ACT - Tanzania kinaamini katika umoja wa bara la Afrika na itikadi ya umajumui wa Afrika. Sera za chama zitajengwa katika kuelekeza nchi yetu inachukua uongozi katika kujenga Shirikisho la Afrika Mashariki kama msingi wa kujenga Afrika moja imara na yenye sauti kwenye mataifa ya ulimwengu.

10.Kujitegemea, Bidii na Weledi katika Kazi
ACT Tanzania inaamini kwamba kujitegemea, bidii na weledi katika kazi ndiyo njia pekee ya kujipatia maendeleo. Hivyo basi wajibu mkuu wa mwanachama wa ACT Tanzania utakuwa ni: BIDII NA WELEDI KATIKA KAZI.
 
Act-tanzania
 

Attachments

  • 1410385094686.jpg
    1410385094686.jpg
    80.7 KB · Views: 102
ACT maana yake IGIZA. Hawa jamaa wanafanya mchezo wa kuigiza! SHAME!!!!!!
 
Ni chama gani kimewahi kusimama jukwaani na kueleza Itikadi yake,Falsafa na misingi kwa uwazi kabisa kama sio ACT maana hivyo vyama vyenu hata viongozi wenu hawajui itakidi zao
 
Act haina tofauti na bunge la posho kule Dodoma.
 
Ni chama gani kimewahi kusimama jukwaani na kueleza Itikadi yake,Falsafa na misingi kwa uwazi kabisa kama sio ACT maana hivyo vyama vyenu hata viongozi wenu hawajui itakidi zao

wekeni katiba yenu hapa ,au bado mnatumia ya anayewatuma?
 
Naona ni mwendo wa kuama vyama tu kwa sasa, kijana soma shule kwanza huku kwenye siasa fanya baadae, unakimbia shule kisa siasa? Tena kwa wasaliti?
 
Nimakosa sana kusema usichokijua ndg yangu,nimekimbia shule gani?
 
1ITIKADI
ACT-Tanzania inaamini katika elimu, uadilifu, kujitegemea na bidii katika kazi kama njia kuu ya kujikomboa dhidi ya umaskini, ujinga na maradhi. Hii ndio misingi iliyoasisi Taifa la Tanzania. Hivyo basi falsafa ya ACT Tanzania ni UNYERERE, ikiwa ni ishara ya dhamira ya kurudisha na kuhuisha misingi iliyoasisi taifa la Tanzania. Kiitikadi ACT Tanzania imejikita katika MRENGO WA KATI KUSHOTO (Center Left Party) na itasimamia Demokrasia Jamii kama dira ya sera za maendeleo ya uchumi nchini Tanzania.

MISINGI YA CHAMA
1.Uzalendo
Ili wananchi waweze kushiriki katika utumishi wa umma na kutoa michango yao mbalimbali kwa dhati na kwa moyo, ni muhimu mazingira yawepo ya kuhakikisha kwamba wananchi wanakuwa na mapenzi yasiyotikisika kwa nchi yao. Kwa msingi huu, ACT-Tanzania itajenga mazingira mwafaka ya wananchi kuipenda nchi yao ili wajitoe kikamilifu katika kuijenga na kuilinda.

2.Usawa
ACT-Tanzania inaamini katika usawa katika nyanja zote. Tunaamini kwamba mafanikio ya mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla yatatokana na bidii katika kazi. Kwahiyo, ACT Tanzania kitapigania kuwepo usawa wa fursa na mazingira mazuri kwa watu wote katika kuhakikisha kwamba kila mtu na kila kundi katika jamii linakuwa na fursa sawa ya kufanya kazi za kujiajiri au kuajiriwa, na kwamba kipato kitokanacho na kazi halali ndicho kitakuwa kipimo cha mchango wake katika jamii na taifa.

3.Uadilifu
Uadilifu katika maisha binafsi na katika jamii utakuwa ndio msingi na mwongozo mkuu wa viongozi na wanachama wa ACT-Tanzania. ACT-Tanzania inaamini kwamba uadilifu ndio msingi na nguzo kuu ya mapambano dhidi ya rushwa na maovu mengine katika jamii. Kama wanachama wa ACT-Tanzania tutajitahidi wakati wote kutumikia na kuishi kwa uadilifu uliotukuka siyo tu kama taasisi bali pia katika maisha yetu binafsi.

4.Uwazi

ACT Tanzania inaamini katika uwazi kwenye mambo yote ya kijamii na kitaifa. Hivyo basi viongozi na wanachama wa ACT-Tanzania wana wajibu wa kupigania uwazi katika mambo yote wanayofanya kwa ajili ya umma. Uwazi huu ni msingi wa kupambana na vitendo vya ukosefu wa maadili na ufisadi na hivyo tunaamini njia sahihi ni kuhakikisha kuwa wanachama na wananchi waliotupa dhamana ya uongozi wanajua yanayofanywa na chama na serikali yao.

5.Uwajibikaji
Sambamba na uwazi, ACT- Tanzania inaamini kwamba kila mwananchi na kiongozi mwenye dhamana katika umma ana wajibu katika jamii na Taifa kwa ujumla na ni jukumu lake kutekeleza wajibu huo bila kinyongo. Aidha, mwanachama na kiongozi atokanaye na ACT Tanzania anapaswa kuwajibika kwa maneno na matendo yake katika utumishi au nje ya utumishi wa chama au taasisi yeyote ya umma.

6.Demokrasia Raslimali
ACT-Tanzania inaamini kuwa demokrasia ndiyo msingi wa kujenga fikra pevu na kueneza uhuru wa mtu, jamii na Taifa kwa ujumla. Hivyo basi, viongozi na wanachama wa ACT-Tanzania watapigania uwepo wa demokrasia ya kweli katika kila ngazi, ndani na nje ya chama. Hata hivyo, ACT Tanzania inaamini kwamba umaskini na ufukara ni kikwazo kikubwa katika kufikia fikra huru. ACT Tanzania inaamini kwamba wananchi kuwa na sauti katika umiliki na uendeshaji wa raslimali za Taifa ndio njia sahihi na ya haraka ya kumaliza umaskini. Chama kinaamini katika demokrasia raslimali ikiwa ni imani kuwa utajiri wa Maliasili ya Afrika kwa ujumla na Tanzania hususani; ni lazima utumike kwa maendeleo ya watu wa Afrika na Tanzania. Hivyo basi, sera za chama zitaelekeza mfumo wa umiliki wa utajiri wa Nchi kuwa ni mali ya wananchi na uendelezwaji wake utafanywa kwa faida ya wananchi kwa ruhusa yao, yaani demokrasia raslimali.

7.Haki ya Kupata Hifadhi ya Jamii
Chama cha ACT - Tanzania kinaamini kuwa kila mtanzania ana haki ya kupata hifadhi ya jamii na hivyo sera zake zitaelekeza serikali kuwajibika katika kutoa haki hii kikatiba. Hifadhi ya jamii ni pamoja na pensheni, bima ya afya, ulinzi wa kijamii kwa wazee, watu wenye ulemavu na wananchi waliofukarishwa na mfumo wa uchumi wa kibeberu.

8.Utu
ACT-Tanzania inaamini kuwa sera, mipango na shughuli zozote za kichama au za kiserikali zitakuwa hazina mafanikio ya kudumu kama hazitatambua, kuheshimu na kulinda utu wa kila Mtanzania. Ni kwa sababu hiyo tunu kuu itakayotuongoza katika utumishi wa umma ni kuheshimu, kutambua na kulinda utu wa kila mtu bila kujali tofauti zozote ambazo zinawatofautisha watu.

9.Umoja wa Afrika
Chama cha ACT - Tanzania kinaamini katika umoja wa bara la Afrika na itikadi ya umajumui wa Afrika. Sera za chama zitajengwa katika kuelekeza nchi yetu inachukua uongozi katika kujenga Shirikisho la Afrika Mashariki kama msingi wa kujenga Afrika moja imara na yenye sauti kwenye mataifa ya ulimwengu.

10.Kujitegemea, Bidii na Weledi katika Kazi
ACT Tanzania inaamini kwamba kujitegemea, bidii na weledi katika kazi ndiyo njia pekee ya kujipatia maendeleo. Hivyo basi wajibu mkuu wa mwanachama wa ACT Tanzania utakuwa ni: BIDII NA WELEDI KATIKA KAZI.
Mnapoteza muda tafuteni kazi za kufanya nyie watu.

Usomi wako kitila unaishia kuandika ovyo ovyo tu
 
Nyie Anguko la Ccm Tanzania anzisheni tovuti na blogu zenu mjitangaze huko.Msijitangaze kwenye sebule za watu!
 
hivi ACT nao bado wapo? saiz tuko busy na chaguzi za chama makini hii thread ipigwe pending kidogo
 
Hivi ACT ina tawi huku JF?.Mbona hiki chama kinasifiwa tuu huku?.Huku Arusha wala hamna mtu anakitaka kwa sababu kuu mbili,
1.Chama cha wasaliti.Hiki chama kinaonekana ni chama cha wasaliti,wasaka madaraka,wapenda ujiko na watu hatari kwa chama,hata taifa kwa ujumla.
2.Ni tawi la CCM.Hawana jipya,kazi yao ni kupambana na CHADEMA.Wanapokea misaada na miongozo kutoka CCM.

Yako mengi,ila kwa leo,naona yanatosha.
 
MISINGI KUMI YA ACT
1.UZALENDO
2.Usawa
3.Uadilifu
4.Uwazi
5.Uwajibikaji
6.Demokrasia RASILIMALI
7.Hifadhi ya jamii
8.Utu
9.Umoja wa Afrika
10.KUJITEGEMEA,bidii na weledi katika kazi

Njano5
0784845394
 
Mkuu umesahau msingi mzito - huo unafaa uwe wa kwanza

1. Usaliti.
 
Back
Top Bottom