Ishu ya dkt ulimboka yazima mjadala wa bajeti??

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
16,510
28,416
Katika kuthibitisha kuwa watanzania wengi bado ni watu wa kuongoza na matukio sana mjadala wa bajeti na matokeo yake sasa huwezi kuusikia japo nina imani huu ndio ulikua wakati wake.
Ni kweli kuwa ishu ya DR ULIMBOKA imekuja kama emergence lakini je mbona historia inatuhukumu, kuwa watanzania wengi aidha hawapendi kufuatilia mambo kwa kina au ni watu wa kuongozwa na matukio hasa kwa kuangalia what is next to discuss.Nina ushahidi na hili(fuatilia ishu kama za MILIPUKO YA MABOMU,DOWANS NA EPA,MIGOMO YA VYUO VIKUU,KATIBA MPYA,MAHAKAMA YA KADHI, WAISLAMU NA MADAI YAO YA SENSA na mengine ambayo yamewahi kulitikisa taifa hili)
Wabongo wengi wamekuwa kama wabunge wa MAGAMBA kwa kuangalia nini kiko mezani na kuunga mkono ili mradi wanaridhisha EGO zao.
JE kauli ya JK ya HUU NAO NI UPEPO UTAPITA haikua ya KIROPOKAJI zaidi bali ilikuwa na chembe za KUWAFAHAMU WABONGO wengi kuwa ni BENDERA FUATA UPEPO??
Je ishu ya DKT ULI ikiisha na bajeti itakuwa imepita vile vile?? Hatuoni kuwa yawezekana kuna intelligent institutions zinazo design matukio ili ku shift focus kwenye mambo yanayowabana WAKULU??

Nakaribisha mjadala wenye maoni ya kisomi...
 
Back
Top Bottom