Kulikuwa na nchi moja huko Amerika ya Kati ambayo ilikuwa inajulikana kama 'Banana Republic', ilijulikana hivyo kwa sababu asilimia kubwa ya mapato yake na uchumi wake ulitegemea zao moja tu la ndizi.
Nina wasiwasi na nchi yetu ya Tanzania inaelekea kujulikana kama 'Mineral Republic'. A country whose economies largely dependent on single commodity.
Nasema hivyo kwa sababu sioni mipango mikakati yeyote 'tangible' ambayo serikali yetu imedhamiria kuifanya au inaifanya kuimarisha sekta zingine zaidi ya sekta ya madini. Nchi imegubikwa na suala moja tu la madini madini utadhani Watanzania hawawezi kuishi bila madini.
Kipindi cha Mwalimu Nyerere kulikuwa na mikakati ya kitaifa ambayo ilitekelezwa kwenye sekta mbalimbali. Tulizoea kusikia serikali ikihamasisha, Elimu Ni Msingi, Kilimo ni Uti wa Mgongo, Misitu ni Mali, 'Kilimo cha kufa na kupona', Maji ni Uhai, nk.
Kwa mfano, mkakati wa serikali ya Nyerere wa 'kilimo cha kufa na kupona' mwitikio na hamasa ilikuwa mkubwa, huko vijijini ilikuwa ni lazima mtu angalau awe na ekari moja ya shamba, na ilikuwa marufuku kuonekana ukizurula nyakati za asubuhi. Upandaji miti vile vile kila mjumbe wa Shina alitakiwa awe na mti wake wa mfano. Leo sioni mikakati yeyote ya maendeleo kuhamasisha wananchi zaidi ya kuhamasishwa kufanya usafi mara moja kwa mwezi.
Hata awamu zilizopita tuliona, mikakati mbalimbali ya maendeleo kitaifa kwenye sekta mbalimbali kama mipango ya , MKURABITA, MKUKUTA, SHULE KILA KATA, KILIMO KWANZA nk ambayo ilikuwa ni mipango ya serikali kuhamasisha wananchi kujihusisha na uzalishaji na maendeleo ya jamii katika maeneo tofauti.
Kipindi cha awamu hii sijasikia wala kuona waraka wowote wa serikali ukisambazwa kuhamasisha azimio au mkakati wowote wa kitaifa, labda nisiwe mchoyo wa fadhila kwenye mpango wa madawati ingawa sijui project hiyo imefanikiwa kwa asilimia ngapi.
Sioni mikakati ya Kilimo, sioni mikakati ya Maji na Uvuvi, Elimu, Misitu, sijaona press conference ya rais kuzungumzia mikakati ya umwagiliaji kila siku madini na miundombinu tuuu.
Naona ni kama serikali imepigwa na ganzi iko 'stagnant' isijue ni vitu gani vya msingi vinavyogusa maisha ya familia moja kwa moja badala ya kusubiri faida ya Madini ambayo wananchi wa kawaida wanaweza wasiipate wala kuiona kwa kipindi cha uhai wao.
Nina wasiwasi na nchi yetu ya Tanzania inaelekea kujulikana kama 'Mineral Republic'. A country whose economies largely dependent on single commodity.
Nasema hivyo kwa sababu sioni mipango mikakati yeyote 'tangible' ambayo serikali yetu imedhamiria kuifanya au inaifanya kuimarisha sekta zingine zaidi ya sekta ya madini. Nchi imegubikwa na suala moja tu la madini madini utadhani Watanzania hawawezi kuishi bila madini.
Kipindi cha Mwalimu Nyerere kulikuwa na mikakati ya kitaifa ambayo ilitekelezwa kwenye sekta mbalimbali. Tulizoea kusikia serikali ikihamasisha, Elimu Ni Msingi, Kilimo ni Uti wa Mgongo, Misitu ni Mali, 'Kilimo cha kufa na kupona', Maji ni Uhai, nk.
Kwa mfano, mkakati wa serikali ya Nyerere wa 'kilimo cha kufa na kupona' mwitikio na hamasa ilikuwa mkubwa, huko vijijini ilikuwa ni lazima mtu angalau awe na ekari moja ya shamba, na ilikuwa marufuku kuonekana ukizurula nyakati za asubuhi. Upandaji miti vile vile kila mjumbe wa Shina alitakiwa awe na mti wake wa mfano. Leo sioni mikakati yeyote ya maendeleo kuhamasisha wananchi zaidi ya kuhamasishwa kufanya usafi mara moja kwa mwezi.
Hata awamu zilizopita tuliona, mikakati mbalimbali ya maendeleo kitaifa kwenye sekta mbalimbali kama mipango ya , MKURABITA, MKUKUTA, SHULE KILA KATA, KILIMO KWANZA nk ambayo ilikuwa ni mipango ya serikali kuhamasisha wananchi kujihusisha na uzalishaji na maendeleo ya jamii katika maeneo tofauti.
Kipindi cha awamu hii sijasikia wala kuona waraka wowote wa serikali ukisambazwa kuhamasisha azimio au mkakati wowote wa kitaifa, labda nisiwe mchoyo wa fadhila kwenye mpango wa madawati ingawa sijui project hiyo imefanikiwa kwa asilimia ngapi.
Sioni mikakati ya Kilimo, sioni mikakati ya Maji na Uvuvi, Elimu, Misitu, sijaona press conference ya rais kuzungumzia mikakati ya umwagiliaji kila siku madini na miundombinu tuuu.
Naona ni kama serikali imepigwa na ganzi iko 'stagnant' isijue ni vitu gani vya msingi vinavyogusa maisha ya familia moja kwa moja badala ya kusubiri faida ya Madini ambayo wananchi wa kawaida wanaweza wasiipate wala kuiona kwa kipindi cha uhai wao.